Tuesday, April 29, 2014

UEFA CHAMPIONZ LIGI LEO UWANJA KUWAKA MOTO

NUSU FAINALI:
Marudiano
[Mechi zote Saa 3 Dakika 45 Usiku]
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
UCL-NUSU_FAINALI-MARUDIANOJumanne Aprili 29
Bayern Munich v Real Madrid [0-1]
Jumatano Aprili 30
Chelsea v Atletico Madrid [0-0]

DONDOO MUHIMU:
-Rekodi ya Bayern Munich wakiwa Nyumbani kwao dhidi ya Real Madrid ni Ushindi: 8, Sare: 1 Kufungwa: 0.
-Real Madrid wameshinda mara 2 tu katika safari zao 27 Nchini Germany, mojawapo ikiwa ni ushindi wa Bao 6-1 dhidi ya FC Schalke katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16 Msimu huu.

Monday, April 28, 2014

KLABU AFRIKA: DROO ZA MAKUNDI KUFANYIKA KESHO

DROO za kupanga Makundi ya CAF CHAMPIONZ LIGI na Kombe la Shirikisho itafanyika Jumanne Aprili 29 huko Makao Makuu ya CAF Jijini Cairo Nchini Misri.
CAF_DROO
Kwenye CAF CHAMPIONZ LIGI zipo Timu 8 zilizofuzu hatua hii na Droo hiyo itapanga Makundi mawili ya Timu 4 kila moja ambayo yatacheza mtindo wa Ligi, Nyumbani na Ugenini, ili kupata Timu mbili za juu toka kila Kundi kucheza Nusu Fainali.
Timu hizo 8 ni:
-Al-Ahly Benghazi ya Libya
-Al-Hilal ya Sudan
-AS Vita Club ya Congo DR
-CS Sfaxien ya Tunisia
-Espérance de Tunis ya Tunisia
-ES Sétif ya Algeria
-TP Mazembe ya Congo DR
-Zamalek ya Egypt
Mechi za Makundi zitaanza Wikiendi ya Mei 16 hadi 18.
CAF Kombe la Shirikisho
Kwenye CAF Kombe la Shirikisho, Droo ya hapo kesho Jumanne pia itashirikisha Timu 8 ambazo nazo zitagawanywa Makundi mawili ya Timu 4 kila moja ambayo yatacheza mtindo wa Ligi, Nyumbani na Ugenini, ili kupata Timu mbili za juu toka kila Kundi kucheza Nusu Fainali.
Timu hizo 8 ni:
-Sewe Sport - Ivory Coast
-Al Ahly – Egypt
-AS Real de Bamako – Mali
-AC Leopards de Dolisie – Congo
-ASEC Mimosas Abidjan - Ivory Coast
-Coton Sport FC – Cameroon
-E.S. Sahel – Tunisia
Mechi za Makundi zitaanza Wikiendi ya M
ei 16 hadi 18.
CAF Kombe la Shirikisho
Marudiano
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Jumamosi Aprili 26
Bayelsa United – Nigeria 0 Sewe Sport - Ivory Coast 1 [0-3]
Difaa Hassani El Jadidi – Morocco 2 Al Ahly – Egypt 1 [2-2, Al Ahly yasonga kwa Bao la Ugenini]
Jumapili Aprili 26
Djoliba AC – Mali 0 AS Real de Bamako – Mali 0 [1-2]
Medeama – Ghana 2 AC Leopards de Dolisie – Congo 0 [2-2, Penati 4-5]
ASEC Mimosas Abidjan - Ivory Coast 1 Kaizer Chiefs - South Africa 0 [3-1]
Petro Atlético de Luanda - Angola 2 Coton Sport FC – Cameroon 2 [3-4]
E.S. Sahel – Tunisia 1 Horoya Athlétique Club – Guinea 0 [1-0]
C. A. Bizertin – Tunisia 1 Nkana FC – Zamba 1 [1-1]

BRENDAN RODGRERS ASEMA CHELSEA WALIPAKI MABASI 2 GOLINI.

Wakati Jose Mourinho akijisifia kwamba timu bora imeshinda, kocha wa Liverpool Brendan Rodgers akiongea na waandishi wa habari ameipaka timu ya Chelsea kwa aina ya uchezaji wao.
morhoChelsea wamepunguza kasi za Liverpool kushinda taji la ubingwa wa EPL baada ya miaka mingi kwa kuwafunga magoli 2 bila huku wakililinda goli lao kwa idadi kubwa ya wachezaji wakiwa ndani ya 18.
Kocha wa Liverpool amesema Chelsea walipaki mabasi mawili golini kwao na ilikuwa ni vigumu kwa wao kupita kujaribu kupata goli.
Licha ya ushindi huo mashabiki wengi wa soka kwenye mtandao wa goal.com wakati post hii inawekwa wameipa nafasi kubwa Manchester city(44.4%) kuchukua taji hilo. Kura hizo zimeipa Liverpool(41%) nafasi ya pili na kumaliza na Chelsea(14.6%).

PFA-LUIS SUAREZ TUZO YA MCHEZAJI BORA WA MWAKA:

Mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez ametwaa Tuzo ya England ya Mchezaji Bora wa Mwaka ya PFA [Professional Footballers' Association], Chama cha Wanasoka wa Kulipwa, hapo Jana.
Msimu uliopita, kipindi kama hiki, Luis Suarez alikuwa akianza kutumikia Adhabu ya Kifungo cha Mechi 10 baada kumuuma Meno Mchezaji wa Chelsea, Branislav Ivanovic, lakini safari hii ni kidedea.
Suarez alikabidhiwa Tuzo yake Jana Usiku kwenye Hoteli ya Kifahari, Grosvenor House, Jijini London mara baada ya kuruka kutoka Jijini Liverpool baada ya Mechi yao Uwanjani kwao Anfield walikofungwa Bao 2-0 na Chelsea.
Msimu huu, Suarez amefunga Bao 30 katika Mechi 31 za Ligi licha ya k
uzikosa Mechi za mwanzo wa Msimu akiwa bado Kifungoni.
Mchezaji wa Chelsea, Eden Hazard, ambae hakucheza hiy
o Jana huko Anfield, alitwaa Tuzo ya England ya Mchezaji Bora Kijana wa Mwaka ya PFA.
Kwenye Timu Bora ya Mwaka ya PFA ya Ligi Kuu England, Suarez alijumuika na wenzake wa Liverpool, Daniel Sturridge na Nahodha wao Steven Gerrard.
Chelsea pia walikuwa na Wachezaji watatu ambao ni Petr Cech, Gary Cahill na Hazard.
Manchester City inawakilishwa na Vincent Kompany na Yaya Toure huku Southampton ikiwa na wawili, Luke Shaw na Adam Lallana.
Mabingwa Watetezi, Manchester United nar Arsenal, haina hata Mchezaji mmoja.
PFA-LIGI KUU ENGLAND-TIMU YA MWAKA: Petr Cech (Chelsea); Luke Shaw (Southampton), Vincent Kompany (Manchester City), Gary Cahill (Chelsea), Seamus Coleman (Everton); Eden Hazard (Chelsea), Yaya Toure (Manchester City), Steven Gerrard (Liverpool), Adam Lallana (Southampton); Luis Suarez (Liverpool), Daniel Sturridge (Liverpool)

WANASOKA BORA WA MWAKA ENGLAND

Mchezaji Bora wa Mwaka: Luis Suarez (Liverpool).
Mchezaji Bora Chipukizi wa mwaka: Eden Hazard (Chelsea).
Mchezaji Bora wa kike wa Mwaka: Lucy Bronze (Liverpool Ladies).
Mchezaji Bora chipukizi wanawake: Martha Harris (Liverpool Ladies).

Sunday, April 27, 2014

AFCON 2015-MOROCCO: DROO YAWEKWA HADHARANI

DROO ya Mashindano ya Mataifa ya Africa, rasmi kama Orange Africa Cup of Nations Morocco 2015, ambayo Fainali zake zitachezwa huko Morocco kati ya Tarehe 17 Januari hadi 8 Februari 2015, imefanyika hii Leo huko Cairo, Egypt.
Nchi 51 zitashiriki Mashindano haya ambapo Mauritania na South Sudan zilishinda toka Raundi ya Kwanza na kutinga Raundi ya Pili ya Mtoano ambayo Tanzania itacheza na Zimbabwe.
AFCON_2015_LOGO-MOROCCOWashindi 14 wa Raundi ya Pili ya Mtoano wataingia Raundi ya Tatu ya Mtoano ili kupata Timu 7 zitakazosonga kwenye Makundi ambayo hii Leo pia yamepangwa.
Ikiwa Tanzania itaitoa Zimbabwe basi kwenye Raundi ya Tatu ya Mtoano itacheza na Mshindi kati ya Mozambique na South Sudan na Tanzania ikipita hapo itaingia 
KUNDI F ambako ziko Zambia, Cape Verde na Niger.
Yapo Makundi 7 ambapo Mshindi wa Kila Kundi na Mshindi wa Pili wa Kila Kundi pamoja na Timu moja iliyofuzu Nafasi ya 3 Bora katika Makundi ndizo zitaingia Fainali kuungana na Morocco na kufanya idadi ya Timu 16 kwenye Fainali.
RATIBA/MAKUNDI:
Nchi ambazo zimeingia Makundi moja kwa moja: Nigeria, Ghana, Ivory Coast, Zambia, Burkina Faso, Mali, Tunisia, Algeria, Angola, Cape Verde, Togo, Egypt, South Africa, Cameroon, DR Congo, Ethiopia, Gabon, Niger, Guinea, Senegal and Sudan.
RAUNDI YA PILI YA MTOANO

Mechi Na 1: Liberia vs Lesotho

Mechi Na 2: Kenya vs Comoros
Mechi Na 3: Madagascar vs Uganda
Mechi Na 4: Mauritania vs Equatorial Guinea
Mechi Na 5: Namibia vs Congo
Mechi Na 6: Libya vs Rwanda
Mechi Na 7: Burundi vs Botswana
Mechi Na 8: Central African Republic vs Guinea Bissau
Mechi Na 9: Swaziland vs Sierra Leone
Mechi Na 10: Gambia vs Seychelles 
Mechi Na 11: Sao Tome e Principe vs Benin
Mechi Na 12: Malawi vs Chad
Mechi Na 13: Tanzania vs Zimbabwe
Mechi Na 14: Mozambique vs South Sudan

**Mechi za Kwanza 16,17,18 Mei 2014

**Mechi za Marudiano 30,31 Mei au 1 Jun1 2014

RAUNDI YA TATU YA MTOANO
**WASHINDI 14 wa Raundi ya Pili ya Mtoano watacheza Raundi hii
TIMU MECHI NA TIMU Mechi ya Kwanza Mechi ya Pili
Mshindi Mechi Na 1 1/2 Mshindi Mechi Na 2 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 3 3/4 Mshindi Mechi Na 4 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 5 5/6 Mshindi Mechi Na 6 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 7 7/8 Mshindi Mechi Na 8 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 9 9/10 Mshindi Mechi Na 10 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 11 11/12 Mshindi Mechi Na 12 18–20 Julai 1–3 Agosti
Mshindi Mechi Na 13 13/14 Mshindi Mechi Na 14 18–20 Julai 1–3 Agosti
MAKUNDI:
KUNDI A
-Nigeria
-South Africa
-Sudan
-Mshindi 5/6
KUNDI B
-Mali
-Algeria
-Ethiopia
Mshindi 11/12
KUNDI C
-Burkina Faso
-Angola
-Gabon
-Mshindi 1/2
KUNDI D
-Ivory Coast
-Cameroun
-Congo DR
-Mshindi 9/10
KUNDI E
-Ghana
-Togo
-Guinea
Mshindi 3/4
KUNDI F
-Zambia
-Cape Verde
-Niger
-Mshindi 13/14
KUNDI G
-Tunisia
-Egypt
-Senegal
-Mshindi 7/8

TANZANIA YAITWANGA KENYA U20 KUFUZU FAINALI ZA AFRIKA

TIMU ya soka ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes imeitoa Kenya katika Raundi ya Kwanza ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika mwakani nchini Senegal kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya jumla ya bila kufungana nyumbani na ugenini.
Kwa matokeo hayo, Ngorongoro inayofundishwa na kocha mzalendo John Simkoko sasa itamenyana na Nigeria katika hatua inayofuata.
Penalti za Tanzania zilikwamishwa nyavuni na Mohammed Hussein, Kevin Friday, Mange Chagula na Iddi Suleiman, wak
ati Mudathir Yahya alikosa.
Penalti za Kenya zilifungwa na Geoffrey Shiveka, Timonah Wanyonyi na Victor Ndinya, wakati Evans Makari na Harison Nzivo walipoteza.
Hakuna kipa aliyeokoa penalti bali wapigaji waliokosa walipiga nje.
Ilikuwa mechi kali na ya ushindani na makipa wa timu zote mbili, Aishi Manula wa Tanzania na Farouk Shikhalo wa Kenya aliyeanza kabla ya kumpisha Boniface Barasa dakika ya 88 walifanya kazi nzuri ya kuokoa michomo ya hatari.

MART NOOIJ AONGEZA 9 TAIFA STARS, KUIVAA MALAWI HUKO MBEYA!!

Kocha mpya wa Taifa Stars, Mart Nooij ameongeza wachezaji tisa katika kikosi hicho kinachojiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Malawi (The Flames) itakayochezwa Mei 4 mwaka huu katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Wachezaji walioongezwa ni Edward Charles Manyama (JKT Ruvu), Elias Maguli (Ruvu Shooting), Hassan Dilunga (Yanga), Hussein Javu (Yanga), John Bocco (Azam), Kelvin Friday (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na Shomari Kapombe (AC Cannes, Ufaransa).
Martinus_Ignatius_Maria_maarufu_kama_Mart_Nooij
Naye beki Kelvin Yondani wa Yanga ambaye aliitwa awali ameondolewa katika kikosi hicho kwa vile ameshindwa kuripoti kambini.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Pemium Lager inaingia kambini kesho (Aprili 28 mwaka huu) jijini Mbeya kujiandaa kwa mechi dhidi ya Malawi.
Wakati huo huo, Tanzania (Taifa Stars) imepangiwa kucheza na Zimbabwe katika raundi ya pili ya mechi za mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika (AFCON) zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.
Stars itaanzia nyumbani ambapo mechi ya kwanza itachezwa kati ya Mei 16 na 18 wakati ile ya marudiano itachezwa Harare kati ya Mei 30 na Juni 1 mwaka huu.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)