Thursday, May 29, 2014

CECAFA NILE BASIN CUP MBEYA CITY ROBO FAINALI KUUMANA NA WAKALI KUTOKA UGANDA

Timu ya Soka ya Mbeya city katika hatua ya Robo fainali itashuka dimbani kuonyeshana kazi na wababe kutoka Uganda, Victory University katika Robo Fainali ya michuano ya Nile Basin Jumamosi ya Mei 31, Uwanja wa Khartoum Sudan.
Hiyo itakuwa robo Fainali ya kwanza siku hiyo itakayoanza Saa 11:30 jioni na kufuatia na mchezo mwingine kati ya wenyeji El Ahli Shandi dhidi ya Malakia ya Sudan Kusini.
Awali, kesho zitachezwa Robo Fainali mbili za kwanza kati ya AFC Leopards ya Kenya na Defence  ya Ethiopia Saa 11:30 kabla ya wenyeji El Merreikh kuumana na Academie Tchite ya Burundi.
Mbeya City ilitinga Robo Fainali za michuano ya Nile Basin inayoendelea nchini Sudan kufuatia sare ya bila kufungana na Enticelles ya Rwanda usiku wa jana Uwanja wa Khartoum.
Matokeo hayo yanaifanya Mbeya City imaliz
e na pointi nne baada ya mechi tatu, ikiwa katika nafasi ya pili nyuma ya AFC Leopards ya Kenya walioongoza kundi kwa pointi zao tisa.
Enticelles imemaliza nafasi ya pil
i kwa pointi zake mbili na Academie Tchite ya Burudi imemaliza mkiani mwa Kundi B kwa pointi moja iliyovuna kwenye sare na timu ya Rwanda.
Michuano hii inayoshirikisha mabingwa wa Kombe la FA au washindi wa pili wa Ligi Kuu za nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), inafanyika kwa mara ya kwanza mwaka huu, Sudan wakiwa wenyeji wa kwanza.
CECAFA imeanzisha mashindano hayo kwa lengo la kuongeza changamoto kwa klabu za ukanda wake. 
MSIMAMO WA:
KUNDI ‘A’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
Al-Merreikh
3
2
1
0
7
2
+5
7
Victoria University
3
2
1
0
4
0
+4
7
Malakia
3
1
0
2
5
5
0
3
Police
3
0
0
3
0
9
-9
0
KUNDI ‘B’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
AFC Leopards
3
3
0
0
5
1
+4
9
Mbeya City
3
1
1
1
4
4
0
4
AcademieTchite
3
1
1
2
3
4
-1
3
Entincelles
3
0
0
2
0
3
-3
1
KUNDI ‘C’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
Al-Shandy
2
2
0
0
4
1
+3
6
Defence
2
1
1
0
2
3
-1
3
Dkhill
2
0
0
2
2
4
-2
0
ROBO FAINALI
TAREHE
M/No.
MECHI
MAHALA
SAA
30/05/14
16
AFC Leopards Vs Defence
MERREIKH
6:30pm

17
Al-MerreikhVs AcademieTchite
MERREIKH
8:30pm





31/05/14
18
Victoria University Vs Mbeya City
MERREIKH
5:30pm

19
Ahly Shandi Vs Malakia
MERREIKH
8:00pm





NUSU FAINALI
Jumatano Juni 2
[20]. Mshindi 16 Vs Mshindi 17
[21]. Mshindi 18 Vs Mshindi 19
Jumatano Juni 4
Mshindi wa Tatu
22]. Aliefungwa 20 Vs Aliefungwa 21
FAINALI[
23] Mshindi 20 Vs Mshindi 21

MKUTANO MKUU WA UONGOZI WA YANGA NA WANACHAMA NI JUMAPILI


Baraka Kizuguto - Afisa Habari Young Africans SC
Mkutano Mkuu wa Wanachama wa mabadiliko ya baadhi ya Vipengele kwenye Katiba utafanyika siku ya jumapili Juni Mosi 2014 katika Ukumbi wa Bwalo la Polisi - Oysterbay kuanzia majira ya saa 3 kamili asubuhi huku wanachama wote hai wa klabu ya Young Africans wakiombwa kujitokeza kwa wingi.
Akiongea na waandshi wa habari makao makuu ya klabu, Afisa Habari wa Young Africans Bw Baraka Kizuguto amesema mkutano huo wa siku ya jumapili ni kwa ajili ya marekebisho ya katiba kama maagizo ya Shirikisho la Soka nchini TFF ilivyoagiza.
"Jumapili tunafanya makutano wa marekebisho ya katiba lengo ni kuhakikisha wanachama wanapata nafasi ya kutoa maoni yao na kupitisha hivyo vipengele ambavyo vitapelekea Yanga kupeleka katiba yake TFF na kisha kwa msajili ili shughuli zote za klabu ziweze kufanyika kwa kufuata katiba mpya" alisema Kizuguto.
Mara baada ya mabadiliko hayo nadhani tutakua tayari kuelekea kwenye mchakato wa Uchaguzi kwani tulikuwa tunasubiria marekebisho ya Katiba tu, TFF na msajili wakishaiptisha Katiba basi tutakua tayari kuelekea kwenye Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Viongozi.
Watakoruhusiwa kuhudhuria mkutano mkuu siku ya jumapili ni wanachama wa Yanga SC walio hai tu, kwa maana ambao wamelipia ada zao za uanachama mpaka kufikia kwa mwezi ujao wa Juni 2014.
Wanachama ambao bado hawajalipia Ada zao za uanchama wanaombwa kulipia mapema kabla ya siku ya mkutano, malipo yote yanafayika kwenye Idara ya Fedha makao makuu ya klabu kila siku muda wa kazi na siku ya jumamosi saa 3 asubuhi mpaka saa 7 mchana.

SAMATTA NA ULIMWENGU WAPATA KIBALI KWA TP MAZEMBE


Klabu ya TP Mazembe hatimaye imewaruhusu wachezaji wake Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu kujiunga na timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ambayo tayari imewasili Harare, Zimbabwe kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika.

Taifa Stars itacheza na Zimbabwe ‘Mighty Warriors’ katika mechi ya marudiano raundi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.  
Mechi hiyo itachezwa Jumapili (Juni 1 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa jijini Harare.Samatta na Ulimwengu watawasili Harare kesho Saa 3.40 usiku kwa ndege ya Kenya Airways na watajiunga na TP Mazembe mara baada ya mchezo huo ambapo Juni 2 mwaka huu, wakienda moja kwa moja Ndola, Zambia ambapo timu yao imepiga kambi kwa ajili ya mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Zamalek Juni 7.

Wednesday, May 28, 2014

TAIFA STARS KWENDA HARARE ALHAMISI KUIKABILI ZIMBAMWE

TFF_LOGO12Msafara wa watu 30 wa Taifa Stars unaojumuisha wachezaji, benchi la ufundi na viongozi unaondoka kesho alfajiri (Mei 29 mwaka huu) kwenda Harare, Zimbabwe kwa ajili ya mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika.
Mechi hiyo itachezwa Juni Mosi mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Harare, Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itatua jijini humo saa 5 asubuhi kwa ndege ya Kenya Airways.
Msafara wa Taifa Stars ambayo ambayo jana (Mei 27 mwaka huu) ilicheza mechi ya kujipima nguvu na Malawi na kushinda bao 1-0, na utarejea nchini Juni 2 mwaka huu unaongozwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi.
Wakati huo huo, mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Malawi (Flames) iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 8,380,000 kutokana na watazamaji 1,504 waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo.
Mgawo ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 1,278,305.08, gharama za kuchapa tiketi sh. 225,600, gharama za uwanja sh. 1,031,414.24, gharama za mechi sh. 1,375,218.98 na TFF/Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 4,469,461.69.
MWAMBUSI KOCHA BORA VPL 2013/2014
Kocha Mkuu wa timu ya Mbeya City, Juma Mwambusi ameshinda tuzo ya kocha bora wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kwa msimu wa 2013/2014.
Hafla ya kukabidhi tuzo kwa washindi mbalimbali ilifanyika jana (Mei 27 mwaka huu) jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Mbali ya tuzo hiyo, Kocha Mwambusi ambaye hivi sasa yuko nchini Sudan na timu yake kwenye michuano ya Nile Basin alipata pia zawadi ya kitita cha sh. milioni 7.8.
Aliyeshinda tuzo ya kipa bora ni Hussein Shariff wa Mtibwa Sugar aliyepata sh. milioni 5.2 wakati Amisi Tambwe wa Simba aliibuka na tuzo ya mfungaji bora. Tambwe naye alipata sh. milioni 5.2.
Mchezaji bora wa VPL kwa msimu wa 2013/2014 ni Kipre Tchetche wa Azam FC aliyejipatia sh. milioni 5.2. Tuzo ya refa bora imetwaliwa na Israel Mujuni aliyezawadiwa sh. milioni 7.8.
Yanga iliyoshika nafasi ya pili kwenye ligi na kupata sh. milioni 37, pia ilipata sh. milioni 16 baada ya kushinda tuzo ya timu yenye nidhamu ya hali ya juu. Sh. milioni 21 za mshindi wa nne zilikwenda kwa timu ya Simba.
Mabingwa wapya wa VPL, Azam FC walipata sh. milioni 75 wakati Mbeya City ilipata sh. milioni 26 kwa kushika nafasi ya tatu.
RAIS MALINZI ATUMA RAMBIRAMBI MSIBA WA KOCHA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Zambia (FAZ), Kalusha Bwalya kutokana kifo cha Kocha wa timu ya Nkana FC, Masauso Mwale.
Amesema amepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha ghafla cha Kocha Mwale, na kuongeza kuwa msiba huo si pigo kwa Zambia pekee bali Afrika kwa ujumla kwa vile ni mfano wa kuigwa kwa makocha wazalendo waliozipatia mafanikio makubwa klabu za Afrika.
Rais Malinzi amemuomba Rais Bwalya kutuma salamu zake za rambirambi kwa familia ya Mwale, na kuitaka kuwa na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito kwao.
Mwale (51) alifariki mwishoni mwa wiki kwa ajali ya gari aliyokuwa akiendesha katika barabara ya Kitwe- Ndola akienda kambini kujiunga na timu yake kwa ajili ya maandalizi ya mechi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Sewe San Pedro ya Ivory Coast.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

KUELEKEA MSIMU MPYA WA LIGI VP TIMU ZILIZO KAMILISHA USAJILI MPAKA SASA.


Katika harakati za kuelekea msimu mpya wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara timu mbalimbali tayari zimekwisha anza kufanya usajili wa hapa na pale
Tukianza na Wagomga Nyundo wa jiji la mbeya Timu ya Mbeya City kutoka Mkoani Mbeya, tayari imekamilisha usajili wa
Mshambuliaji kutoka Timu ya Kagera Sugar Themi Felix na Kiungo Peter Mwalianzi kutoka timu ya JKT Mgambo.
Safu ya Ushambuliaji ya Timu hiyo iliyofanikiwa kushika Nafasi ya Tatu kwenye Ligi Kuu Vodacom, VPL, Msimu huu, itakuwa sasa na Paul Nonga, Mwagane Yeya, Saad Kipanga na Themi Felix kuanzia msimu ujao na huku Peter Mwalianzi akiongeza nguvu kwenye safu ya Kiungo inayoongozwa na Steven Mazanda.

Tuwatazame Mabingwa wapya wa VPL, Azam FC, tayari walishakamilisha usajili wa Frank Domayo na Didier Kavumbagu kutoka Yanga na kumuongeza Beki Abdallah Heri kutoka Klabu ya Zimamoto ya kule Zanzibar.
Hivyo basi kwa sasa safu ya Kiungo ya Mabingwa hao itaundwa na Hi
mid Mao, Kipre Balou, Salumu Abubakary na Domayo Frank huku Brian Umony, Gaudence Mwaikimba, John Bocco, Kipre TcheTche na Kavumbagu wakikamilisha Safu ya Ushambuliaji.

Nao Timu ya Ruvu Shooting iliyomaliza Msimu kwenye Nafasi ya Tano baada ya kupata Alama 38, tayari imekamilisha usajili wa Zuberi Dabi kutoka Klabu ya Kagera Sugar. Timu hiyo pia imefanikiwa kumsajili Chagu Chagula mshambuliaji Raia wa Tanzania ambaye amecheza sana Nchini Burundi.
Kwa upande wa Wagosi wa Kaya Baada ya kuandaa mkakati na kuachana na Wachezaji wanaotemwa na Timu za Simba na Yanga, Klabu ya Coastal Union ya Tanga tayari imekamilisha usajili wa Bright Obina ambaye aliwahi kuzichezea African Lyon na Ashanti United zote za Dar es Salaam.
Timu hiyo pia imefanikiwa kumnasa Hussein Swed ambaye Msimu uliopita alikuwa na Timu iliyoshuka Daraja ya Ashanti United na sasa wote wametua kwa Wagosi wa Kaya.
Kwa upande wa Simba wekundu msimbazi mpaka sasa bado hawaja weka hadharani majina wachezaji waliowasajili licha ya kuwa na taarifa za kuwa bado wapo katika harakati za kufanya usajili na upo uwezakoano kutwaa wachezaji kutoka kadhaa kutoka nje ya boda Uganda au Kenya ili kuweza kuimarisha kikosi hicho ambacho kwa sasa kipo katika harakati za uchaguziwa viongozi unaotaraji kufanyika Juni 29 mwaka huu.
Yanga nao washindi wa pili wa ligi kuu msimu uliopita tayari wamefanikisha kumnasa Kiungo Omega Seme aliyekuwa kwa Mkopo kwa Wajelajela Tanzania Prison pamoja na kafinikisha kumbakisha Beki Kisiki Mbuyu Twite Baada ya Kuondoka kwa aliye kuwa kiungo chumvi Frank Domayo pamoja na Mshambuliaji Didier Kavumbagu.
Kwa mujibu wa TFF, Usajili wa Wachezaji kwa hatua ya kwanza Msimu mpya wa 2014/2015 unaanza Juni 15 hadi Agosti 3 Mwaka huu wakati Kipindi cha kutangaza Wachezaji walioachwa au kusitishiwa Mikataba ni kuanzia Juni 15 hadi 30.
Kipindi cha kwanza cha Uhamisho wa Wachezaji ni kuanzia Juni 15 hadi Julai 30.
Kupitia Majina na kutangaza pingamizi ni kati ya Agosti 4 na 11 na kuthibitisha Usajili hatua ya awali ni Agosti 12 hadi 14.
Usajili hatua ya pili utakuwa kati ya Agosti 14 na 29 wakati kupitia na kutangaza Majina ya pingamizi hatua ya pili ya usajili ni kuanzia Agosti 30 hadi Septemba 4. Uthibitisho wa Usajili hatua ya pili ni Septemba 5 na 6.
Ligi Kuu ya Vodacom, VPL, inatarajiwa kuanza Agosti 24 na Ratiba inatarajiwa kutoka Mwezi mmoja kabla hapo Julai 24.