Thursday, May 29, 2014

CECAFA NILE BASIN CUP MBEYA CITY ROBO FAINALI KUUMANA NA WAKALI KUTOKA UGANDA

Timu ya Soka ya Mbeya city katika hatua ya Robo fainali itashuka dimbani kuonyeshana kazi na wababe kutoka Uganda, Victory University katika Robo Fainali ya michuano ya Nile Basin Jumamosi ya Mei 31, Uwanja wa Khartoum Sudan.
Hiyo itakuwa robo Fainali ya kwanza siku hiyo itakayoanza Saa 11:30 jioni na kufuatia na mchezo mwingine kati ya wenyeji El Ahli Shandi dhidi ya Malakia ya Sudan Kusini.
Awali, kesho zitachezwa Robo Fainali mbili za kwanza kati ya AFC Leopards ya Kenya na Defence  ya Ethiopia Saa 11:30 kabla ya wenyeji El Merreikh kuumana na Academie Tchite ya Burundi.
Mbeya City ilitinga Robo Fainali za michuano ya Nile Basin inayoendelea nchini Sudan kufuatia sare ya bila kufungana na Enticelles ya Rwanda usiku wa jana Uwanja wa Khartoum.
Matokeo hayo yanaifanya Mbeya City imaliz
e na pointi nne baada ya mechi tatu, ikiwa katika nafasi ya pili nyuma ya AFC Leopards ya Kenya walioongoza kundi kwa pointi zao tisa.
Enticelles imemaliza nafasi ya pil
i kwa pointi zake mbili na Academie Tchite ya Burudi imemaliza mkiani mwa Kundi B kwa pointi moja iliyovuna kwenye sare na timu ya Rwanda.
Michuano hii inayoshirikisha mabingwa wa Kombe la FA au washindi wa pili wa Ligi Kuu za nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), inafanyika kwa mara ya kwanza mwaka huu, Sudan wakiwa wenyeji wa kwanza.
CECAFA imeanzisha mashindano hayo kwa lengo la kuongeza changamoto kwa klabu za ukanda wake. 
MSIMAMO WA:
KUNDI ‘A’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
Al-Merreikh
3
2
1
0
7
2
+5
7
Victoria University
3
2
1
0
4
0
+4
7
Malakia
3
1
0
2
5
5
0
3
Police
3
0
0
3
0
9
-9
0
KUNDI ‘B’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
AFC Leopards
3
3
0
0
5
1
+4
9
Mbeya City
3
1
1
1
4
4
0
4
AcademieTchite
3
1
1
2
3
4
-1
3
Entincelles
3
0
0
2
0
3
-3
1
KUNDI ‘C’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
Al-Shandy
2
2
0
0
4
1
+3
6
Defence
2
1
1
0
2
3
-1
3
Dkhill
2
0
0
2
2
4
-2
0
ROBO FAINALI
TAREHE
M/No.
MECHI
MAHALA
SAA
30/05/14
16
AFC Leopards Vs Defence
MERREIKH
6:30pm

17
Al-MerreikhVs AcademieTchite
MERREIKH
8:30pm





31/05/14
18
Victoria University Vs Mbeya City
MERREIKH
5:30pm

19
Ahly Shandi Vs Malakia
MERREIKH
8:00pm





NUSU FAINALI
Jumatano Juni 2
[20]. Mshindi 16 Vs Mshindi 17
[21]. Mshindi 18 Vs Mshindi 19
Jumatano Juni 4
Mshindi wa Tatu
22]. Aliefungwa 20 Vs Aliefungwa 21
FAINALI[
23] Mshindi 20 Vs Mshindi 21