Thursday, May 29, 2014

MKUTANO MKUU WA UONGOZI WA YANGA NA WANACHAMA NI JUMAPILI


Baraka Kizuguto - Afisa Habari Young Africans SC
Mkutano Mkuu wa Wanachama wa mabadiliko ya baadhi ya Vipengele kwenye Katiba utafanyika siku ya jumapili Juni Mosi 2014 katika Ukumbi wa Bwalo la Polisi - Oysterbay kuanzia majira ya saa 3 kamili asubuhi huku wanachama wote hai wa klabu ya Young Africans wakiombwa kujitokeza kwa wingi.
Akiongea na waandshi wa habari makao makuu ya klabu, Afisa Habari wa Young Africans Bw Baraka Kizuguto amesema mkutano huo wa siku ya jumapili ni kwa ajili ya marekebisho ya katiba kama maagizo ya Shirikisho la Soka nchini TFF ilivyoagiza.
"Jumapili tunafanya makutano wa marekebisho ya katiba lengo ni kuhakikisha wanachama wanapata nafasi ya kutoa maoni yao na kupitisha hivyo vipengele ambavyo vitapelekea Yanga kupeleka katiba yake TFF na kisha kwa msajili ili shughuli zote za klabu ziweze kufanyika kwa kufuata katiba mpya" alisema Kizuguto.
Mara baada ya mabadiliko hayo nadhani tutakua tayari kuelekea kwenye mchakato wa Uchaguzi kwani tulikuwa tunasubiria marekebisho ya Katiba tu, TFF na msajili wakishaiptisha Katiba basi tutakua tayari kuelekea kwenye Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Viongozi.
Watakoruhusiwa kuhudhuria mkutano mkuu siku ya jumapili ni wanachama wa Yanga SC walio hai tu, kwa maana ambao wamelipia ada zao za uanachama mpaka kufikia kwa mwezi ujao wa Juni 2014.
Wanachama ambao bado hawajalipia Ada zao za uanchama wanaombwa kulipia mapema kabla ya siku ya mkutano, malipo yote yanafayika kwenye Idara ya Fedha makao makuu ya klabu kila siku muda wa kazi na siku ya jumamosi saa 3 asubuhi mpaka saa 7 mchana.