Thursday, July 10, 2014

SERENGETI BOYZ VS AFRICA KUSINI AZAM COMPLEX

index
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boyz) inacheza mechi ya kujipima nguvu kesho (Julai 11 mwaka huu) dhidi ya Azam U-20 kwenyeUwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Mechi hiyo ambayo ni maalumu kwa benchi la ufundi la Serengeti Boyz likiongozwa na kocha Hababuu Ali Omari kuangalia kikosi chao itaanza saa 2 kamili asubuhi.
Serengeti Boyz itacheza mechi yake ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika dhidi ya Afrika Kusini (Amajimbos) siku ya Ijumaa, Julai 18 mwaka huu kwenye uwanja huo huo wa Azam Complex kuanzia saa 10 kamili jioni.
Wachezaji wanaounda kikosi cha Serengeti Boyz ni Abdallah Shimba, Abdulrasul Bitebo, Abutwalibu Mshery, Adolf Bitegeko, Ally Mabuyu, Ally Mnasi, Amin Noren, Athanas Mdamu, Badru Othman, Baraka Baraka, Hatibu Munishi na Issa Athuman.
Wengine ni Juma Yusuf, Kelvin Faru, Kelvin Kamalamo, Martin Luseke, Mashaka Ngajilo, Mechata Mnata, Mohamed Abdallah, Mussa Vicent, Nazir Barugire, Omary Omary, Omary Wayne, Prosper Mushi, Seif Seif na Yahya Hafidh.

Wednesday, July 9, 2014

STARS, MSUMBIJI KIINGILIO 7,000/=, TIKETI KWA M-PESA.

TFF-MPESA-MALIPOKiingilio cha chini cha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 7,000.
Tiketi zinapatikana kwa mfumo wa elektroniki kupitia M-PESA. Kiingilio hicho kwa ajili ya viti vya rangi ya rangi ya chungwa, kijani na bluu. Viingilio katika maeneo mengine vitatangazwa baadaye.
TFF-TANZANIA-MSUMBIJIMshabiki ili apate tiketi anatakiwa kutumia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha bonyeza 4, ingiza namba ya kampuni 173399 kisha weka 7000 kwenye namba ya kumbukumbu ya malipo, na weka
7000 kama kiasi cha bei ya tiketi na mwisho weka namba yao ya siri.
Baada ya hapo utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo kwa ajili ya kuchukulia tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.
TFF-MPESAVituo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illutions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).
Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na ofisi za TFF (PPF Tower).
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

VPL:LIGI KUU KUANZA SEPTEMBA 20


Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu wa 2014/2015 itaanza kutimua vumbi Septemba 20 mwaka huu.
VPL_2013-2014-FPAwali michuano hiyo ilikuwa ianze Agosti 24 mwaka huu, lakini Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limelazimika kuisogeza mbele kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupitisha michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame).
Michuano ya Kombe la Kagame inayoshirikisha mabingwa wa nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) itafanyika Agosti mwaka huu nchini Rwanda.
Timu 14 zitashiriki Ligi Kuu msimu huu. Timu hizo ni mabingwa watetezi Azam, Coastal Union, JKT Ruvu Stars, Kagera Sugar, Mbeya City, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Ndanda FC, Polisi Morogoro, Ruvu Shooting, Simba, Stand United, Tanzania Prisons na Yanga.
Ratiba ya ligi hiyo itatolewa mwezi mmoja kabla ya michuano hiyo kuanza kutimua vumbi.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Friday, July 4, 2014

ROBO FAINALI KOMBE LA DUNIA

FULECO_NA_BRAZUCA
RATIBA
ROBO FAINALI
IJUMAA, JULAI 4 ,2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
1900
France v Germany [57]
ROBO FAINALI
Estadio do Maracanã.
2300
Brazil v Colombia [58]
ROBO FAINALI
Estadio Castelão.
JUMAMOSI, JULAI 5, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
1900
Argentina v Belgium [59]
ROBO FAINALI
Nacional, Brasilia.
2300
Netherlands v Costa Rica [60]
ROBO FAINALI
Arena Fonte.
NUSU FAINALI
JUMANNE, JULAI 8, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
2300
Mshindi 57 v Mshindi 58 [61]
NUSU FAINALI
Estadio Mineirão
JUMATANO, JULAI 9, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
2300
Mshindi 59 Mshindi 60 [62]
NUSU FAINALI
Arena Corinthians.
MSHINDI WA TATU
JUMAMOSI, JULAI 12, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
2300
Aliefungwa 61 v Aliefungwa 62
MSHINDI WA 3
Nacional, Brasilia.
FAINALI
JUMAPILI, JULAI 13, 2014
SAA
MECHI
KUNDI
UWANJA
2200
Mshindi Mechi 61 v Mshindi Mechi 62
FAINALI
Estadio do Maracanã.

BRAZIL-KIKOSI
Uso kwa Uso
Timu hizi zimekutana mara 25 na Brazil kushinda mara 15 Colombia 2 na Sare 8.
REFA: Carlos Ve
lasco [Spain]
KOMBE LA DUNIA
RATIBA
Saa za Bongo
VIKOSI VINATARAJIWA:
Brazil: Cesar, Marcelo, Silva, Alves, Luiz, Paulinho, Fernandinho, Hulk, Neymar, Fred, Willian.
Colombia: Ospina; Armero, Yepes, Zapata, Zunjiga; Guarin, Sanchez, Vargas, Martinez, Rodriguez; Teofilo.

Wednesday, July 2, 2014

KIRAFIKI GABORONE: BOTSWANA YAICHAPA 4 TANZANIA 2

TAIFA_STARS-BORA1Katika mechi ya kirafiki Wenyeji Botswana wamefanikiwa kuilaza taifa stars katika Uwanja wa Taifa Jijini Gaborone wameichapa Tanzania Bao 4-2 katika Mechi ya Kirafiki.
Taifa Stars ndio waliotangulia kufunga kwa Bao la Mcha Khamisi kufuatia Difensi ya Botswana kujichanganya lakini Timu hiyo, inayoitwa Zebras, ilisawazisha kabla Mapumziko kwa Bao la Kichwa la Jerome Ramatlhatwane.
Hadi Mapumziko, Zebras 1 Taifa Stars 1.
Kipidi cha Pili, Zebras walikuja moto na kupiga Bao 3 kupitia Lemponye Tshireltso, Bonolo Phuduhudu na Kijana wa Miaka 19, Karabo Phiri.
Taifa Stars walifunga Bao lao la Pili kwa Penati ya Dakika ya 76 ya John Bocco.
Mechi hii ilikuwa ya kujipima nguvu kwa Timu zote mbili kwa ajili ya Mechi za Mchujo za AFCON 2015 ambapo Taifa Stars wataivaa Msumbiji Jijini Dar es Salaam hapo Julai 20 na Zebras kucheza na Guinea Bissau Julai 19.
Taifa Stars, ambao wako chini ya Kocha Mart Nooij, waliwasili huko Gaborone kwa Kambi ya Mazoezi tangu Juni 24 na wamekuwa wakifanya Mazoezi Uwanja wa SSKB wakiwa na Kikosi kamili kasoro Wachezaji wawili wa TP Mazembe, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.
Jumamosi, huko huko Gaborone, Taifa Stars watajipima nguvu na Lesotho.

Friday, June 27, 2014

SIMBA SC YAWAALIKA WADAU KUONA MAENDELEO YA UWANJA BUNJU



SIMBA wekundu wa msimbazi wamesema kuwa sasa wapo katika kuondoa dhama kama club kongwe ilianzishwa mwaka 1936 kuhakikisha wanakamilisha uwanja huo.
hivyo basi wameamua kuwaalika wanachama wanahabari kuona maendeleo ya uwanja wa Bunju Jinsi unavyo endelea ambapo sasa umefika hatua nzuri kilicho baki ni kuanza kuweka nyasi.

Yote  kwa yote Azam fc kwa hapa tz ndio timu pekee ndio klabu ya Tanzania yenye uwanja wake wa kisasa kwa ajili ya mazoezi, mechi za ligi kuu na michuano yote inayosimamiwa na shirikisho la soka barani Afrika, CAF.
Katika historia ya soka la Tanzania, Azam fc haiwezi kunusa ukongwe wa klabu mbili za Simba na Yanga.
Hizi ni klabu zenye mafanikio ndani na nje ya uwanja. Ni klabu zenye mashabiki kila kona ya nchi hii.
Lakini licha ya kukaa miaka mingi katika soka la ushindani nchini Tanzania na michuano ya Kimataifa, Yanga na Simba hazijawahi kumiliki viwanja vyake vya mazoezi na mechi za ligi kuu.
Kwa miaka mingi sasa viongozi wanaopita katika klabu hizo wanakuja na ndoto za kujenga viwanja, lakini zinayeyuka kutokana sababu mbalimbali ikiwemo kuendekeza siasa kuliko vitendo.

RASMI" MAHAKAMA YAAMUA UCHAGUZI WA SIMBA SC KUFANYIKA JUNI 29

BAADA ya mvutano wa hapa na pale katika uchaguzi wa Simba sc sasa tamati imefika baada ya mahakamu kuu kuruhusu mchakato huo kuendelea kama kawaida.
Baadhi ya wanachama wa Simba walienda mahakama kuu wakihitaji chombo hicho cha dola kusimamisha uchaguzi wa Simba unaotarajia kufanyika juni 29 mwa
ka huu.
Sababu ya wanachama hao ilikuwa ni kupinga maamuzi ya kamati ya uchaguzi ya Simba, chini ya mwenyekiti wake, Wakili Damas Daniel Ndumbaro, kuliengua jina la aliyekuwa mgombe wa Urais, Michael Wambura kwa mara ya pili.
Hata hivyo, suala la wanachama kupelekea suala la michezo katika mahakama ya kawaida ilikuwa ni hatari zaidi kwa klabu ya Simba kwasababu sheria za mpira ziko wazi na hairuhusiwi kupeleka mambo ya mpira mahakama za dola.
FIFA wanataka masuala ya mpira yasuluhishwe katika mifumo yake ya haki na si vinginevyo.
Kupeleka mambo ya mpira mahakama za kawaida ilikuwa moja ya sababu iliyokuwa na nguvu kumuengua Wambura kwa mara ya kwanza.
http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/05/Wanachama-Simba1.jpgHata hivyo kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na katibu mkuu wa Simba, Kamwaga jioni ya leo imesema kamati ya Uchaguzi ya Simba SC imesema kuwa inapenda kuwaalika wanachama wote wa Simba katika Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Klabu uliopangwa kufanyika Keshokutwa Jumapili, Juni 29 mwaka huu, katika Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Kamwaga alifafanua kuwa katika uchaguzi huo, jumla ya wagombea 27 wanatarajiwa kushiriki na Kamati ya Uchaguzi imeazimia kwamba suala la muda litazingatiwa sana safari hii kutokana na ukweli wa kuwepo kwa wagombea wengi.