Friday, December 12, 2014

MANENO ALIYO YAANDIKA MH ZITTO KATIKA UKURASA WAKE WA TWITTER SOMA UFAIDIKE

Unyenyekevu {kuwa na kiasi }
Mwaka 2007 Agosti 14, nilisimamishwa Kuhudhuria vikao vya Bunge kwa kosa la kumwita Waziri wa Nishati na Madini Bwana Nazir Karamagi muongo. Kiukweli nilisimamishwa kwa sababu nilitoa hoja Bungeni iliyoiabisha Serikali - Hoja ya Buzwagi.
Wananchi walikasirishwa na kitendo hicho na kuamua kunipokea kwa maandamano makubwa sana nilipoingia Jijini Dar Es Salaam na kwenye mikoa mingine niliyofanya ziara.
Mawaziri waliotumwa kueleza maamuzi ya Bunge walizomewa na kumwagiwa mchanga. Mzee Samwel Sitta, Spika wa Bunge la Tisa, alikuwa anatumiwa sms za 'kifedhuli' kwa mujibu wa maneno yake; nyingine alinitumia kunisihi nizungumze na ' wafuasi' wangu ili waache kufanya hivyo. Hasira ya Wananchi ilikuwa kubwa sana na ilionekana wazi wazi.
Siku ya tarehe 19 Agosti nilitoka Dodoma kuelekea Dar Es Salaam. Kabla sijafika Chalinze ya Dodoma alinipigia simu kaka yangu Abdurahman Mbamba, akanisihi sana kuwa mnyenyekevu kwa maongezi yangu. Nasaha hizi kwa kweli zinaniongoza mpaka leo hii. Kwenye mafanikio ya jambo fulani au hata kutofanikiwa, nakumbuka maneno ya Abdurahman Mbamba.
Nilipokuwa nahutubia Jangwani siku hiyo, niliongea kwa ufupi sana. Watu wakapiga kelele niendelee kuongea. Ningeweza kuongea nitakavyo maana ndio nilikuwa ' star' wa nyakati. Mshale wa nasaha zile ukanichoma ' kuwa mnyenyekevu '!
Nikawaambia wananchi ' siwezi kuendelea kuongea, nina Viongozi wangu hapa'. Alikuwapo Mheshimiwa Freeman Mbowe, Dkt. Willibrod Slaa, Mheshimiwa Augustine Mrema, Maalim Seif Sharif Hamad, ndg. Ibrahim Lipumba na Bwana James Mbatia.
Kwa unyenyekevu nilishuka jukwaani na kutoa nafasi kwa Viongozi kuzungumza. Watu walitaka na ningetaka ningeendelea lakini la hasha, nilikataa.
Rais aliunda Kamati ya kupitia Mikataba ya Madini. Aliniteua katika Kamati ile iliyoongozwa na Jaji Mark Bomani. Watu wangu wengi ' wa karibu' walinisihi nisikubali kuingia kwenye kamati. Mmoja alithubutu kuniambia ' snubb him' akimaanisha Rais.
 Kwamba ningepata umaarufu zaidi. Ningeweza kukataa na kuwafurahisha watu waliotaka kumwaibisha Rais. ' kuwa mnyenyekevu' yakawa ni maneno yananirudia kila wakati.
Hilo na kiu ya kuijua Sekta ya Madini vilivyo yalinishawishi kukubali uteuzi ule. Walionishawishi kukataa hawakunisamehe mpaka leo. Utawasikia wakisema ' Kamati ya Bomani haikufanya lolote'.
Wakati huo huo wanakuwa mstari wa mbele kufurahia mabadiliko makubwa sana kwenye Sekta ya Madini ikiwemo kuongezeka Mapato ya kikodi, umiliki wa Serikali kwenye migodi, Madini ya Vito kuchimbwa na Watanzania pekee na hata kuanza kutozwa kwa Kodi ya ongezeko la mtaji ( capital gains tax ).
Yote hayo yametokana na mapendekezo ya Kamati ya Bomani yaliyozaa Sera mpya ya Madini ya mwaka 2009 iliyopelekea Sheria mpya ya Madini ya mwaka 2010.
Mwaka 2014 tunaufunga kwa suala la akaunti ya Tegeta Escrow. Bunge lilifanikiwa kupitisha maazimio 8 yaliyowasilishwa Serikalini kwa utekelezaji. Maazimio hayo yalipatikana kwa maridhiano ya Bunge zima. Ni mafanikio makubwa ambayo yanashawishi wahusika wakuu kufurahia au hata ku 'claim credit'.
Mbunge mmoja kijana rafiki yangu kutoka Mkoa wa Arusha akaniambia ' brother this is your resurrection ' na usiache. Mwandishi mmoja wa gazeti la kila wiki akaniambia ' it's a come back ' na kunitaka nifanye ziara Nchi nzima kuelezea suala hili.
Wenzangu kwenye Siasa wakaandaa maandamano Jijini Dar ambayo nilikataa. Shemeji yangu mmoja akaniambia ' kwenye ushindi jua pa kuishia'. Maneno haya hayana tofauti na nasaha za Abdurahman.
Sasa kuna juhudi kubwa za kutetea waliotajwa na Taarifa ya Kamati ya PAC. Magazeti, haswa ya Serikali yamekuwa yakiandika habari zenye mwelekeo wa kutetea.
Ikulu imeagiza Taarifa ya CAG ichapwe kwenye magazeti, jambo ambalo halijapata kutokea huko nyuma kwani sio mara ya kwanza PAC kutumia Taarifa ya CAG kuwajibishana.
Makala zinaandikwa kumshawishi Rais asitekeleze maamuzi ya Bunge. Nasaha za ' know where to stop ' na ' kuwa mnyenyekevu ' zinanivuta na kunishawishi kutosema lolote.
Hekima inataka kumwachia Mkuu wa Nchi kuamua kwa namna itakavyompendeza. Tumwache aamue. Unyenyekevu unataka hivyo. Wenye ushawishi tofauti walikuwa na nafasi Bungeni.
Walishindwa ndani ya Baraza la Taifa. Unyenyekevu ni kwa walioshindwa pia.

Sunday, December 7, 2014

MOURINHO AWALAUMU VIJANA WAOKOTA MIPIRA KWA KIPIGO CHA JANA

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amelalama kuhusu upotezaji wa wakati baada ya timu yake kufungwa kwa mara ya kwanza katika msimu huu ugani Newcastle.
Mabao mawili ya Papis Cisse yaliiweka Newcastle kifua Mbele lakini baadaye mshambuliaji Didier Drogba akifungia Chelsea lakini bao hilo halikutosha.
''Kuna mambo ambayo yalikuwa yakifanyika bila refa kuona.Hawezi kumwaadhibu kijana wa kubeba mpira ambaye alitoweka ghafla,ama mashabiki ambao wakipata mpira wanakaa nao ama hata kuutupa uwanjani wakati mechi inaendelea''.,alisema Mourinho.
Kilabu ya Newcastle iliona mlinzi wake Steven Taylor akionyeshwa kadi nyekundu wakati ambao Newcastle ilikuwa juu kwa mabao 2-0 lakini wakaendelea na kuvunja rekodi ya Chelsea ya kutofungwa msimu huu.

RAIS JAKAYA KIKWETE APIGA TIZI MARA TATU KWA SIKU KUIMARISHA AFYA YAKE


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazoezi leo katika viwanja vya Ikulu kufuatia ushauri wa madaktari waliomtaka afanye hivyo mara tatu kwa siku ili kuendelea kuimarisha afya yake baada ya kufanyiwa upasuaji mwezi uliopita katika hospitali ya Johns Hopkins nchini Marekani

DIAMOND AWASILI WASHINGTON, DC TAYARI KWA SHOW YA SHEREHE YA UHURU


 Diamond akiwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa Dulles muda huu tayari kwa makamuzi ya sherehe ya Uhuru itayofanyika muda si mrefu Sheraton, ya Downtown Silver Spring, Maryland.
 Diamond akimsalimia mwenyeji wake hayupo pichani mara tu alipowasili Dulles.

















 Kutoka kushoto ni Dj Romy Jones, Diamond na mmoja wa waratibu wa sherehe ya Uhuru Bwn. Phanuel Ligate

Saturday, December 6, 2014

TIMU NNE ZA TZ BARA ZAALIKWA KUSHIRIKI KOMBE LA MAPINDUZI.

Timu nne za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Azam FC, Mtibwa Sugar FC, Simba SC na Yanga SC zimealikwa kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi itakayofanyika Zanzibar Januari mwakani.
Kenyan Premier League (KPL) side AFC Leopards has for the second year in a row landed an invite to take part in the Mapinduzi Cup in January 2015.
Jumla ya timu 11 zinatarajiwa kushiriki michuano hiyo mwakani kama ilivyothibitishwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Zanzibra (ZFA), Kassim Haji Salum katika mkutano na waandishi wa habari visiwani hapa jana Ijumaa.
Endapo klabu za Azam, Mtibwa, Simba na Yanga zitashiriki michuano hiyo, ni wazi kwamba ratiba ya VPL italazimika kupanguliwa kwa mara ya tatu msimu huu baada ya kufanyiwa marekebisho na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Agosti na Oktoba mwaka huu.
Mashindano ya Kombe la Mapinduzi hufanyika kuanzia Januari 1-12/13 kila mwaka ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mapinduzi tukufu ya Zanzibar.
Ratiba ya VPL mwanzoni mwa mwaka ujao inaonesha kuwa Azam FC itawaalika Mtibwa Sugar FC kwenye Uwanja wa Azam jijini Dar es Salaam Januari 3, Yanga SC itakuwa mgeni wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Mbeya Januari 3 huku Simba SC itaalikwa na Mgambo Shooting Stars kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga Januari 4.
Salum aliweka wazi kuwa barua za mwaliko zinapaswa kujibiwa na klabu kufikia Jumatatu Desemba 15, mwaka huu na mashindano yataanza rasmi Alhamisi Januari Mosi, mwakani ambapo mbali na klabu nne za VPL, mabingwa watetezi KCCA ya Uganda pia wamealikwa.
Timu nyingine zilizoalikwa ni pamoja na mabingwa wa Zanzibar KMKM, Polisi, JKU, Mtende Rangers, Shaba FC na AFC Leopards ya Ligi Kuu ya Kenya inayonolewa na Kocha James Nandwa ikishiriki kwa mara ya pili baada ya kualikwa tena mwaka huu.
Mechi ya fainali itapigwa Uwanja wa Jumanne Januari 13  na Simba SC, ikiwa chini ya Kocha Mcroatia Zdravko Logarusic ilifungwa bao 1-0 dhidi ya KCCA katika mechi ya fainali mwaka huu

WAWA BEKI MPYA WA AZAM FC ASEMA AMEKUJA KUTENGENEZA HESHIMA NA KUJIUZA KATIKA TIMU ZA ULAYA.

Pascal Wawa Beki mpya wa kati wa Azam FC ambae anaendelea na mazoezi na kikosi hicho ameweka wazi na kusema kuwa kilichomleta Tanzania ni kutengeneza heshima yake na timu kwa ujumla.
Raia huyo wa Ivory Coast ambaye majina ya wachezaji wa Yanga, Mrisho Ngassa na Juma Kaseja ndiyo yapo kwenye akili yake kutokana na namna anavyowafahamu.
Wawa anaamini Azam ndiyo itakuwa njia yake ya kutoka kwenda kucheza soka la kulipwa Ulaya baada ya kushindwa kufanikisha malengo yake hayo katika klabu ya El Merreikh ya Sudan alikocheza kwa miaka minne
Wawa amesema kwanza amekuja kucheza mpira Azam kwa malengo makubwa mawili, kwanza ni kujitangaza ili nisonge mbele na kupata timu katika nchi zilizoendelea Ulaya baada ya kuona nimecheza Sudani kwa miaka minne bila mafanikio.

Pili ni kuifanya Azam ifikie malengo yaliyokusudiwa kwa kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa, lakini yote hayo nataka kuyakamilisha kwa vitendo kimya kimya.
Wawa aliwahi kuja Tanzania kwa vipindi tofauti, kwanza akiwa na Ivory Coast iliyoshiriki CHAN mwaka 2010 na iliyocheza Kombe la Chalenji jijini Dar es Salaam pia amekuja na El Merreikh kwa vipindi tofauti kucheza mashindano ya Kombe la Kagame. Wawa ni Muivory Coast wa tatu kutua kikosini hapo baada ya Kipre Tchetche na Kipre Bolou

MSHAMBULIAJI SAIDI BAHANUZI ATUA POLISI MOROGORO KWA MKOPO

Timu ya yanga african wazee wa jangwani imemtoa mshambuliaji Said Rashid Bahanuzi kwa mkopo katika klabu ya Polisi Morogoro.
Bahanuzi amechagua kwenda Polisi badala ya timu zote zilizokuwa zikimuhitaji, Stand United na Ruvu Shooting kwa kuwa anaamini huko ni sehemu sahihi kwenda kufufua makali yake.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar amejikuta katika wakati mgumu Yanga SC, baada ya kung’ara kwa msimu mmoja tu, 2012.
Bahanuzi aliingia kwa kishindo Yanga SC akiiwezesha timu hiyo kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kagame la Kagame 2012 naye pia kuwa mfungaji bora.
Baada ya hapo, Bahanuzi akaanza vizuri pia kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kabla ya kuumia katikati ya msimu na kuwa nje hadi msimu uliofuata.
Hata hivyo, tangu kuumia Bahanuzi hajaweza kurejea katika kiwango chake licha ya makocha wote aliofanya nao kazi Yanga SC baada ya Mbelgiji Tom Saintfiet kumpa nafasi.
Hao ni Waholanzi Ernie Brandts na Hans van der Pluijm pamoja na huyu wa sasa, Mbrazil Marcio Maximo. 
Tangu amejiunga Yanga SC, Said Bahanuzi amecheza mechi 48 na kufunga mabao 15, matatu kwa penalti.