Saturday, December 6, 2014

WAWA BEKI MPYA WA AZAM FC ASEMA AMEKUJA KUTENGENEZA HESHIMA NA KUJIUZA KATIKA TIMU ZA ULAYA.

Pascal Wawa Beki mpya wa kati wa Azam FC ambae anaendelea na mazoezi na kikosi hicho ameweka wazi na kusema kuwa kilichomleta Tanzania ni kutengeneza heshima yake na timu kwa ujumla.
Raia huyo wa Ivory Coast ambaye majina ya wachezaji wa Yanga, Mrisho Ngassa na Juma Kaseja ndiyo yapo kwenye akili yake kutokana na namna anavyowafahamu.
Wawa anaamini Azam ndiyo itakuwa njia yake ya kutoka kwenda kucheza soka la kulipwa Ulaya baada ya kushindwa kufanikisha malengo yake hayo katika klabu ya El Merreikh ya Sudan alikocheza kwa miaka minne
Wawa amesema kwanza amekuja kucheza mpira Azam kwa malengo makubwa mawili, kwanza ni kujitangaza ili nisonge mbele na kupata timu katika nchi zilizoendelea Ulaya baada ya kuona nimecheza Sudani kwa miaka minne bila mafanikio.

Pili ni kuifanya Azam ifikie malengo yaliyokusudiwa kwa kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa, lakini yote hayo nataka kuyakamilisha kwa vitendo kimya kimya.
Wawa aliwahi kuja Tanzania kwa vipindi tofauti, kwanza akiwa na Ivory Coast iliyoshiriki CHAN mwaka 2010 na iliyocheza Kombe la Chalenji jijini Dar es Salaam pia amekuja na El Merreikh kwa vipindi tofauti kucheza mashindano ya Kombe la Kagame. Wawa ni Muivory Coast wa tatu kutua kikosini hapo baada ya Kipre Tchetche na Kipre Bolou