![]() |
Diamond vs Zari |
Mitandao ya kijamii na
vyombo vya habari vya Uganda vimemgeuka nyota wa vipindi vya runinga na
Mwanamuziki Zari ‘The Boss Lady’ kwa madai kwamba amemganda mwanamuziki wa
Tanzania Diamond Platnumz.
Gazeti la udaku la Red
Pepper, mitandao ya ugvision.com, bigeye.ug na mingineyo, imedai kuwa nyota
huyo amemganda mwanamuziki huyo tangu alipopata upenyo wa kurekodi naye singo
jijini Dar es Salaam.
![]() |
Mama Diamond,Diamond na Zari |
Mitandao hiyo imeponda kuwa
Zari ana tabia ya kuwanadi wanaume anaotoka nao.
![]() |
Zari akiwa na Tuzo za Diamond Channeo o' |
Diamond ambaye alinyakua
tuzo tatu za Channel O 2014, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla
inayoandaliwa na Zari, ijulikanayo kama ‘Zari All White Ciroc Party’,
itakayofanyika Desemba 18, mwaka huu.