Tuesday, April 30, 2013

LIGI KUU VODACOM TANZANIA BARA DIMBANI KESHO YANGA USO KWA USO NA WAGOSI


.

LIGI KUU YAINGIA RAUNDI YA 25
 Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea katika raundi yake ya 25 kesho (Mei Mosi) kwa mechi tano zitakazochezwa katika miji ya Dar es Salaam, Turiani, Morogoro na Mlandizi. Licha ya kuwa tayari Yanga imetawazwa kuwa mabingwa wa VPL msimu huu (2012/2013), mechi dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni moja kati ya zitakazovuta macho na masikio ya washabiki wa mpira wa miguu nchini. Mechi hiyo namba 172 itachezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara wakati mwamuzi wa mezani atakiwa Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni David Lugenge kutoka Iringa. Viingilio katik mechi hiyo itakayoanza saa 10.15 jioni ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 8,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000. Tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mchezo. Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa African Lyon katika mechi namba 170 itakayochezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana wa Dodoma kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro. Nayo Kagera Sugar iliyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam na wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 7,000 uko tayari kwa mechi kati ya JKT Ruvu na Tanzania Prisons. Nayo Ruvu Shooting itakuwa nyumbani kwenye uwanja wake Mabatini ulioko Mlandizi, Pwani kuikabili Oljoro JKT kutoka Arusha.

MTANZANIA APEWA ITC KUCHEZA MSUMBIJI Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Yusuf Kunasa kucheza nchini Msumbiji. Shirikisho la Mpira wa Miguu cha Msumbiji (FMF) lilituma maombi TFF kumuombea hati hiyo Kunasa anayekwenda kujiunga na timu ya Estrela Vermelha da Beira inayocheza Ligi Kuu nchini humo. Kunasa ambaye msimu huu hakuwa na timu (free agent) amejiunga na timu hiyo akiwa mchezaji wa ridhaa (amateur). Zaidi ya wachezaji kumi kutoka Tanzania hivi sasa wanacheza katika klabu mbalimbali nchini Msumbiji. 

MECHI YA SIMBA, POLISI MOROGORO YAINGIZA MIL 18/- Mechi namba 163 ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa juzi (Aprili 28 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Simba kuibuka ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi Morogoro imeingiza sh. 18,014,000. Watazamaji 3,145 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 3,564,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 2,747,898.31. Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 2,841 na kuingiza sh. 14,205,000 wakati idadi ndogo ya washabiki ilikuwa ya kiingilio cha sh. 20,000 kilichovutia washabiki 36 na kuingiza sh. 720,000. Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 1,812,331.75, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 1,087,399.05, Kamati ya Ligi sh. 1,087,399.05, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 543,699.53 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 422,877.41.

Monday, April 29, 2013

AZAM FC WATUA MOROCO KWA MCHEZO WA MARUDIANO


CLUB ya  azam FC imefika salama nchini Morocco tayari kwa mchezo wa marudiano dhidi ya wenyeji, FAR Rabat, Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho Afrika Jumamosi wiki hii.  

Azam, imewasili Cassablanca, majira ya saa 9:15 za huku Alasiri, sawa na saa 10:15 za Afrika Mashariki na kusafiri kwa basi kwa saa mbili kwenda Rabat, mji ambao mechi itachezwa.

Azam imetua Morocco ikitokea Dubai, UAE ambako ilifika usiku jana saa 6:00 kwa saa za huko sawa na saa 5:00 kwa saa za Afrika Mashariki, ikitokea Dar es Salaam.
Msafara huo unaouhusisha wachezaji na benchi la Ufundi, baada ya awali viongozi na wapenzi kadhaa kutangulia nchini humo, ili kuweka mazingira sawa, uliondoka Dar es Salaam kwa ndege ya shirika la Emirates, wadhamini wa Arsenal ya England saa 11:00 jioni kwa saa za Tanzania.
Ni safari ndefu iliyohusisha mabara mawili, kutoka Afrika, Tanzania kupitia Asia Dubai na kurudi Afrika nchini Morocco.
Azam walilala katika hoteli ya nyota tano ya Copthorne Dubai kabla ya kuunganisha ndege saa 7:35 asubuhi ya leo kuja Morocco kesho.
Azam imefikia katika hoteli ya Golden Tulip, maeneo ya Rabat, kaskazini mwa Cassablanca,  kilomita 120 kutoka Uwanja wa Ndege wa Cassablanca, umbali wa takriban saaa mbili.

Azam itaanza rasmi mazoezi kesho kujiandaa na mchezo huo, ambao wanatakiwa kutoa sare ya mabao au kushinda ili kusonga mbele, baada ya awali katika mchezo wa kwanza kulazimishwa sare ya bila kufungana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wiki iliyopita.
Azam, itakuwa Rabat kwa wiki nzima hadi Jumamosi itakapocheza mechi na imejipanga vema kuhakikisha inavuka hatua hii. 

DIMBANI UCL-NUSU FAINALI KUENDELEA LEO

MARUDIANO
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumanne Aprili 30
Real Madrid v Borussia Dortmund [1-4]
Jumatano Mei 1
Barcelona v Bayern Munich [0-4]
FAINALI
25 Mei 2013
UWANJA wa WEMBLEY, London.

MECHI ZILIZOBAKI KWA KUTAFUTA 4 BORA LIGI KUU UINGEREZA BPL
ARSENAL-Mechi zilizobaki:
4 Mei: QPR [Ugenini]
14 Mei: Wigan [Nyumbani]
19 Mei: Newcastle [Ugenini]
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
CHELSEA-Mechi zilizobaki:
5 Mei: Man United [Ugenini]
8 Mei: Tottenham [Nyumbani]
11 Mei: Aston Villa [Ugenini]
19 Mei: Everton [Nyumbani]
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
TOTTENHAM-Mechi zilizobaki:
4 Mei: Southampton [Nyumbani]
8 Mei: Chelsea [Ugenini]
12 Mei: Stoke [Ugenini]
19 Mei: Sunderland [Nyumbani] 

MSIMAMO
NA TIMU P GD PTS
1 Man Utd 35 43 85
2 Man City 34 30 71
3 Chelsea 34 33 65
4 Arsenal 35 30 64
5 Tottenham 34 17 62
6 Everton 35 14 59
7 Liverpool 35 25 54

MAKAMU M/KITI SIMBA AIPONGEZA YANGA KUTWAA UBINGWA


KLABU ya Simba imewapongeza watani zao Yanga kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara huku wakiapa kuwatibulia furaha kwa kuwafunga katika mechi ya kufunga pazia la ligi hiyo itakayochezwa Mei 18 kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Joseph Itang’ale ikiwa ni siku chache tangu Yanga itwae ubingwa wa ligi hiyo baada ya Azam kutoka sare ya bao 1-1 na Coastal Union ya Tanga, hivyo kutokewepo timu yenye ubavu wa kuzifikia pointi 56 ilizonazo hadi sasa.
Kinesi amesema pamoja na pongezi hizo, wajiandae kwani wamejipanga kutibua furaha hiyo kwa kuwafunga na kamwe hawawezi kukubali kuvuliwa ubingwa na kufungwa na mtani wao.
Kinesi ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo anayekaimu nafasi ya Makamu Mwenyekiti baada ya kujiuzulu kwa Geofrey Nyange  amesema japo watani zao wametwa ubingwa, wasitarajie ushindi Mei 18.
 ambapo wekundu hao ndio mabingwa wa msimu uliopita baada ya kuwachalaza watani hao bao 5-0 toka ligi kuu ianzishwe simba imetwaa taji hilo mara 18 huku yanga ikitwaa mara 24
Mwaka 1965, 1966 (as Sunderland)
1972, 1973, 1976, 1977, 1978, 1979, 1980, 1993, 1994, 1995, 2001/02, 2002/03, 2004/05, 2007/08, 2009/10, 2011/12 
Mwaka1968, 1969, 1970, 1971, 1972, 1974, 1981, 1983, 1985, 1987, 1989, 1991, 1992, 1993, 1996, 1997, 1998, 2002, 2005, 2006, 2008, 2009, 2011,2013

FERGUSON NASEMA LIVERPOOL WALIKUWA SAWIA SAWIA.


BOSI wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson amesema  kuwa nakuweka imani kuwa uongozi wa Liverpool ulikuwa sahihi kutochukua hatua dhidi ya mshambuliaji wao Luis Suarez kabla ya kufungiwa mechi 10 na Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa kumng’ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic. Ferguson amesema tukio hilo linamkumbusha jinsi walivyotendwa na FA baada ya mshambuliaji wake Eric Cantona kumpiga teke la kung-fu mshabiki wa Crystal Palace mwaka 1995. Ferguson amedai kuwa FA iliwahakikishia kuwa hatachukua hatua zaidi kama United watamuadhibu mchezaji huyo lakini pamoja na United kumfungia Cantona miezi minne, chama hicho kiliongeza adhabu na kufikia miezi nane. Kwa matokeo hayo yaliyowakuta United kipindi hicho Ferguson amesema ameelewa kwanini Liverpool hawakumuadhibu nyota huyo mapema.

GARETH BALE ATWAA UCHEZAJI BORA PFA.

KIUNGO machachali wa klabu ya Tottenham Hotspurs Gareth Bale amekuwa mchezaji wa tatu kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka kwa upande wa wakubwa na wachezaji wanaochipukia kwa msimu mmoja, tuzo ambazo hutolewa na Chama cha Wachezaji wa Kulipwa nchini Uingereza. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Wales mwenye umri wa miaka 23 ambaye pia alishinda tuzo ya wakubwa mwaka 2011, amefunga mabao 19 katika ligi msimu huu na kuwa nyuma ya kinara wa mabao Robin van Persie mwenye mabao 25 na Luis Suarez mwenye mabao 23. Akikabidhiwa tuzo hiyo Bale amesema ni heshima kubwa kwake kunyakuwa tuzo hizo mbili muhimu na kushukuru wapiga kura kwa kutambua mchango wake haswa ikizingatiwa kumekuwa na majina makubwa mengine katika orodha iliyokuwepo. Bale anaungana na wachezaji wengine walioshinda tuzo ya wakubwa mara mbili ambao ni Cristiano Ronaldo, Thierry Henry, Alan Shearer and Mark Hughes wakati walioshinda tuzo zote mbili kwa mwaka mmoja ni Ronaldo mwaka 2007 na Andy Gray mwaka 1977.


REKODI ZA BALE:


-2012-13 (Inaendelea): Mechi 29, Magoli 19, Amesaidia 4
-2011-12: Mechi 36, Magoli 9, Amesaidia 10
-2010-11: Mechi 30, Magoli 7, Amesaidia 1
-2009-10: Mechi 23, Magoli 3, Amesaidia 5
-2008-09: Mechi 16, Magoli 0, Amesaidia 0
-2007-08: Mechi 8, Magoli 2, Amesaidia 0

WASHINDI WALIOPITA:
2011-12: Gareth Bale (Tottenham)
2011-12: Robin van Persie (Arsenal)
2010-11: Gareth Bale (Tottenham)
2009-10: Wayne Rooney (Man Utd)
2008-09: Ryan Giggs (Man Utd)
2007-08: Cristiano Ronaldo (Man Utd)
Wanandinga wengine ambao walikuwa wakigombea na Bale ni 
Michael Carrick wa Man United, 
Wachezaji wa Chelsea Eden Hazard na Juan Mata, ambao wote hao pamoja na Suarez na Van Persie wapo Kwenye Timu Bora ya Mwaka ya Wachezaji 11.

Gareth Balle
Gareth Bale - Spurs vs Brighton.jpg
Kuhusu yeye
Full name Gareth Frank Bale
Date of birth 16 July 1989 (age 23)
Place of birth Cardiff, Wales
Height 1.86 m (6 ft 1 in)
Playing position Winger
Timu ya sasa
Current club Tottenham Hotspur
Number 11
Academy
2005–2006 Southampton
Timu za ukubwa
Years Team mechi (Goli)
2006–2007 Southampton 40 (5)
2007– Tottenham Hotspur 142 (40)
Timu ya taifa
2005–2006 Wales U17 7 (1)
2006 Wales U19 1 (1)
2006–2008 Wales U21 4 (2)
2006– sasa Wales 41 (11)

MATAJI
Southampton Academy 

TUZO BINAFSI

Sunday, April 28, 2013

SAMWELI ETO'O KATIKA ULIMWENGU WA SOKA
Samuel 2011.jpg
Eto'o in 2011.
Kuhusu yeye
Full nameSamuel Eto'o Fils
Date of birth10 March 1981 (age 32)
Place of birthDoualaCameroon[1]
Height1.80 m (5 ft 11 in)[2]
Playing positionStriker
Timu
Current clubAnzhi Makhachkala
Number9
academy
1992–1997Kadji Sports Academy
Timu za ukubwa
YearsTeammechi(Goli)"
1997–2000Real Madrid3(0)
1997–1998→ Leganés (mkopo)30(4)
1999→ Espanyol (mkopo)0(0)
2000→ Mallorca (mkopo)19(6)
2000–2004Mallorca120(48)
2004–2009Barcelona145(108)
2009–2011Internazionale67(33)
2011–Anzhi Makhachkala43(21)


TIMU YA TAIFA CAMEROON 
YearmechiGoli
199730
199850
199910
200095
200192
2002135
200372
200494
200561
200655
200731
20081111
200985
2010128
201194
201220
201312
Total11255

TIMU NA MATAJI ALIYOCHUKUWA

Mallorca
Barcelona
Inter milan

kimataifa

Cameroon
Cameroon Olympic Team




TUZO BINAFSI
 1.Mchezaji wa Mwaka afrika: 2003, 2004, 2005, 2010
 2.mshambuliaji bora wa Mwaka UEFA: 2006
 3.FIFA World Cup - Golden mpira 2010
 4.2005 FIFA World Mchezaji wa Mwaka wa Tatu
 5.Vijana wa Afrika Mchezaji wa Mwaka: 2000
 6.ESM Timu ya Mwaka: 2004-05, 2005-06, 2008-09, 2010-11
 7.FIFPro World XI: 2005, 2006
 8.UEFA Timu ya Mwaka: 2005, 2006
 9.Kombe la Mataifa mfungaji bora: 2006, 2008
10.Kombe la Mataifa ya wakati wote mfungaji bora
11.RCD Mallorca ya wakati wote mfungaji bora
12.mfungaji bora Cameroon wakati wote
13.Ligi ya Mabingwa ya Final Man of the mechi 2006
14.CAF Kuanzia XI katika Kombe la Mataifa ya Afrika 2006 Misri