Saturday, June 29, 2013

ARSENAL WAMTAKA KIPA JULIO CESAR WA QPR ILIYOSHUKA DARAJA"

Wanted: Julio Cesar is set to join Arsenal following Queens Park Rangers' relegation to the Championship WASHIKA Bunduki wa jiji London Club ya Arsenal itaangalia uwezekano wa kukamilisha usajili wa kipa namba wa Brazil na klabu ya Queens Park Rangers, Julio Cesar baada ya Kombe la Mabara.
Arsene Wenger anataka kipa mzoefu atengeneze ushindani kwa Lukasz Fabianski na Wojciech Szczesny.
Mazungumzo baina ya wawakilishi wa Cesar na viongozi wa Gunners tayari yamefanyika, lakini hayajamalizika kwa kuwa kipa huyo yupo kwenye majukumu ya kimataifa.
Wanted: Julio Cesar is set to join Arsenal following Queens Park Rangers' relegation to the Championship
ARSENAL sasa inatarajiwa kumaliza dili hilo mara moja tu, baada ya kubainika Roma ya Italia nayo imeingia kwenye mbio za kuwania saini ya Cesar.
Kipa huyo wa kimataifa wa Brazil ambaye yupo huru kuondoka Loftus Road kufuatia kushuka kwa QPR hadi Championship, anataka kubaki London ambako amezoea maisha tangu awasili msimu uliopita akitokea Inter Milan.
Na The Gunners – ambayo inatumai kukamilisha pia usajili wa Gonzalo Higuain wiki ijayo, baada ya kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti kufungua njia kwa mshambuliaji huyo kuondoka  Hispania – inajiamini dili hilo litakamilishwa baada ya Fainali ya Kombe la Mabara Jumapili.
Wenger alitaka kusajili kipa wa Stoke, Asmir Begovic na wa Liverpool, Pepe Reina lakini, licha ya kuwa na fungu la bajeti ya usajili la Pauni Milioni 70, kocha huyo wa Arsenal ameona  hana sababu ya kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kipa.
Rangers itasikiliza ofa ya kiasi cha Pauni Milioni 2 kwa Cesar, wakati mshahara wake wa Pauni 70,000 kwa wiki halitakuwa tatizo kwa The Gunners, ambayo imetuma waangalia vipaji wake nchini Brazil kumuangalia Cesar anachokifanya katika Kombe la Mabara.
Pamoja na mpango wa kuwasajili Cesar na Higuain, The Gunners pia wanataka kumsajili beki wa Swansea, Ashley Williams na kiungo wa Everton, Marouane Fellaini. Lakini masuala ya kifedha yanatia saka kama Arsenal itaweza kusajili wachezaji wote hao.
Hadi sasa, Arsenal imegoma kumpa Fellaini mshahara wa Pauni 100,000 kwa wiki na pia imeshindwa kufika dau la Pauni Milioni 24 za kumnunua.
Missing out? Arsenal look set to be priced out of moves for Marouane Fellaini and Ashley Williams (below) Amekosekana? Arsenal inataka kuwasajili Marouane Fellaini

MBEYA MWENYEJI WA NETIBOLI TENA KWA MARA YA PILI MFULULIZO".

Jiji la Mbeya kwa mara ya pili mfululizo,litakuwa mwenyeji wa ligi kuu ya Netiboli taifa ambapo  naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo anatarijiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi kuanzia Agosti 24 hadi Septemba 7.
Mwenyekiti wa chama cha Netiboli Mkoa wa Mbeya, Mary Mung’ong’o ameumabia mtandao huu kuwa ligi hiyo inafanyika kwa mara nyingine kutokana na ombi la Waziri Mulugo kwa vile ligi hiyo haikuwa imefana, hivyo akaiomba CHANETA kuwapa Mbeya fursa nyingine ya uwenyeji.
Alisema maandalizi ya ligi yameanza na kusema zinahitajika sh milioni 16 kufanikisha na kuongeza kuwa hadi sasa, hawajajua timu ngapi zitashiriki kutokana na jukumu hilo kuwa chini ya Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA).
Hata hivyo, mwenyekiti huyo ametoa wito kwa viongozi wa ngazi mbalimbli wakiwemo wadau wenye mapenzi na mchezo kutoka mkoani hapa kujitoa kwa hali na mali kuyafanikisha ili yawe chachu ya kukua kwa mchezo huo nchini kwa maslahi ya vijana na taifa.
Aidha, mwenyekiti huyo alitamtambulisha Nwaka Mwakisu kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano hayo.
Akizungumzia mashindano hayo, Mwakisu alisema ni fursa kwa watu wa Mbeya kujitangaza kibiashara kupitia mchezo huo na kufuta makosa yaliyofanyika mwaka jana.
Alisema katika kufakisha mashindano hayo, nguvu ya pamoja inahitajika kuanzia viongozi wa kisiasa, serikari na vyombo vya habari.

MBASPO FC YATWAA UBINGWA WA AIRTEL RISING KWA MKOA WA MBEYA"

Kama kawaidaTimu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Mbaspo imefanikiwa kuwa mabingwa wa Airtel Rising Stars mkoa wa Mbeya baada ya kukusanya pointi nne sawa na mahasimu wao Mbosa fc lakini wakiwa na magoli mengi ya kufunga. Timu ya Mbeya Secondari haikupata hata pointi moja katika michuano hiyo ya kusaka vipaji

Mbaspo walianza mbio zao za kutwaa ubingwa kwa kutoshana nguvu ya 3-3 dhidi ya Mbosa siku ya Jumatatu Juni 24 kabla ya kufanya mauaji makubwa ya 6-0 dhidi ya timu dhaifu ya Mbeya Sekondari siku ya Jumanne. Michezo yote imefanyika kwenye uwanja wa Magereza jijini Mbeya.
Mbosa walifikisha point nne juzi Jumatano walipoitandika Mbeya Sekondari 3-0 hivyo kumaliza wakiwa na point nne na magoli sita wakati wapinzani wao Mbaspo wakifikisha jumla ya magoli tisa ya kufunga. Katika mechi ya juzi, magoli ya Mbosa yalitiwa kwenye kamba na Michael Mwashilanga, Riziki Juma na Julius Landa.
Wakati huo huo, chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mbeya kimetangaza kikosi cha wachezaji 18 kuuwakilisha mkoa huo kwenye michuano ya Taifa ya Airtel Rising Stars inayoanza kutimua vumbi kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 2.

Wachezaji hao ni Ismail Yesaya, Emmanuel Alex, Gift Sanga, Jackson Mwaibambe, Boaz Mwangole, Costa Sanga, Seif Zubery, Stanley Angelo, Enock Sikaonga, Kaunda Malata, Joel Kasimila, Hamprey Nyeo, Elia Salengo, Peter Noah, Emmaneul Mtimbi, Michael Bosco, Richard Kalinga na Zamoyoni Mwashambwa. 

Katika mkoa wa Morogoro, mji kasoro bahari, timu ya Moro Kids imetoka sare ya bila kufungana na Techfort katika mchezo wa kushambuliana kwa zamu uliopigwa kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Morogoro juzi Jumatano na kushuhudiwa na mashabiki wengi wa mji huo
Airtel Rising Stars vile vile imeanza kutimua vumbi katika jiji la Mwanza ambapo timu ya Marsh Athletical imedhihirisha umwambe wake katika soka baada ya kuifunga Nyamagana United 2-0 kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana.
Timu za mikoa zimepangwa kuanza kuwasili jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki tayari kwa ajili ya kindumbwe ndumbwe cha Airtel Rising Stars ngazi ya taifa katika uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. Wachezaji 16 watachaguliwa wakati wa mashindano hayo ili kuunda timu itakayoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars. Nchi mwenyeji wa michuano hiyo itatangazwa baadaye mwezi ujao.

Friday, June 28, 2013

YANGA YAITAKA TFF IWALIPE KABLA JUMAPIL

YANGA_MJENGOWAKATI inasemekana TFF walishalipwa Shilingi Milioni 200 toka kwa Wadhamini wa Ligi Kuu ya Bara, VODACOM, tangu Mwezi uliopita zikiwa ni Zawadi kwa Washindi mbali mbali wa Ligi hiyo, Klabu zimelalamika kutolipwa Zawadi zao na Yanga wametaka walipwe Milioni 70 zao kabla Jumapili.
Zawadi hizo ni kwa ajili ya kumtunukia Bingwa, Yanga, pia wengine wanaostahili ni ni Azam FC, Simba, Kagera Sugar pamoja na Wachezaji mbali mbali wakiwemo Kipa Bora, Mfungaji Bora, ambae ni Kipre Tcheche wa Azam FC, Refa Bora, Kocha Bora na kadhalika.
Hata hivyo, Vodacom inasemekana wameshatangaza Zawadi hizo zitagawiwa mapema Mwezi ujao na hilo limegusiwa pia na TFF ambao wamesema wanaandaa Siku maalum ya kutoa Zawadi hizo ikiwa ni pamoja na kualika Maafisa wa Serikali pamoja na wale kutoka Wizara husika hasa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Msimu uliopita hata Simba walicheleweshwa kupata Zawadi yao kama Bingwa baada ya kusubiri karibu Miezi miwili tangu Ligi imalizike ili kupata Tuzo yao.
Yanga walitwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Vodacom kwa Msimu wa 2012/13 uliomalizka Mwezi Mei lakini wao walitwaa Ubingwa huo mapema kabla Msimu huo haujafika tamati.

WAWILI WALA SHAVU WACHAGULIWA KITUO CHA VIPAJI ASPIRE

Wachezaji wawili kutoka Tanzania wamechaguliwa miongoni mwa 50 waliofanyiwa majaribio nchini Uganda kwa ajili ya kuingia katika kituo cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) kilichoko Doha nchini Qatar kupitia mpango wa kukuza vipaji wa Aspire Football Dream.
Abdulrasul Tahir Bitebo (15) ambaye ni mshambuliaji kutoka Kituo cha Uwanja wa Karume, na Martin Omela Tangazi (14) ambaye ni beki kutoka Kituo cha Ukonga ndiyo waliochaguliwa kutoka Tanzania kuingia katika kituo ambapo watakaa kwa mwezi mmoja kabla ya kusaini mkataba rasmi wa kuendelezwa.

Wachezaji wengine walikuwa wakitoka katika nchi za Uganda na Kenya. Mchezaji mwingine aliyefuzu katika nafasi tatu zilizokuwepo ni kutoka nchini Kenya.

Mpango wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar katika nchi 16 duniani, na kwa hapa nchini uko chini ya Idara ya Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

TFF ina jumla ya vituo 14 vya kuendeleza vipaji kupitia mpango huo wa Aspire Football Dream. Vituo hivyo ni Karume, Kigamboni, Tandika, Kawe, Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni, Makongo, na Tabata vilivyo katika Mkoa wa Dar es Salaam. Vingine ni Bagamoyo kilichopo mkoani Pwani, Morogoro, Arusha na Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kituo kingine cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) cha Aspire kipo Dakar nchini Senegal.

TFF KUENDESHA KOZI SITA KATI YA JULAI- SEPTEMBA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaendesha kozi sita tofauti za mpira wa miguu kati ya Julai na Septemba mwaka huu.

Kozi hizo ni FIFA 11 For Health itakayofanyika Hombolo mkoani Dodoma kuanzia Julai 8 hadi 19 mwaka huu. Julai 6 hadi 15 mwaka huu kutakuwa na kozi ya mpira wa miguu wa ufukweni (Beach Soccer) itakayofanyika jijini Dar es Salaam.

Waamuzi wa FIFA nao watakuwa na kozi itakayofanyika kati ya Agosti 22 hadi 26 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati kozi ya ukocha kwa ajili ya Copa Coca-Cola itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Agosti 12 na 17 mwaka huu.

Vilevile kutakuwa na kozi ya mpango wa grassroots unaolenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12 itafanyika kuanzia Septemba 9 hadi 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati tamasha (festival) la grassroots litafanyika Uwanja wa Karume, Septemba 14 mwaka huu.

RCL KUKAMILISHA HATUA YA NNE JUMAPILI
Mechi za marudiano za hatua ya nne ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zitachezwa Jumapili (Juni 30 mwaka huu) kwenye viwanja vya Sokoine jijini Mbeya, na Kambarage mjini Shinyanga.

Friends Rangers ya Dar es Salaam ambayo katika mechi ya kwanza ilifungwa nyumbani mabao 3-0 itakuwa mgeni wa Stand United FC mjini Shinyanga wakati Kimondo SC itaikaribisha Polisi Jamii ya Mara jijini Mbeya. Katika mechi ya kwanza timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.

Hatua ya mwisho ya RCL itachezwa Julai 3 mwaka huu kwa mechi za kwanza wakati zile za marudiano zitafanyika Julai 7 mwaka huu. Timu tatu za kwanza zitapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MAN UNITED USO KWA USO NDANI YA EVERTON WATAKA KUIBOMOA

Mabingwa wa BPL msimu uliopita Club ya soka ya Manchester United imeamua kumtengea kitita cha paundi milioni 15 kwa ajili ya kumnasa beki wa Everton, Leighton Baines. Baada ya kukataa ofa ya awali ya United ya Pauni Milioni 12, Everton imesisitiza kuwa beki huyo wa kushoto wa kimataifa wa England hauzwi. Lakini United imepania kupanda dau hadi paundi milioni 20 katika kuwania saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. Mrithi wa Moyes, Everton, Roberto Martinez anataka kumbakzia beki huyo na klabu hiyo inataka kumpa mkataba mpya ikimuongezea mshahara hadi paundi 70,000 kwa wiki. Mpango huu unamuweka shakani beki Mfaransa, Patrice Evra juu ya mustakabali wake Old Trafford na wazi sasa anaweza kuhamia Monaco au Paris Saint-Germain.

WAMSHANGAA MESSI BAADA YA KUTUA NCHIN SENEGAL-WAKANYAGANA

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Argentina Lionel Messi ametua nchini Senegal jana kwa ndege binafsi na kulakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Dakar na mashabiki wa soka na vijana wadogo waliotoka pembe mbalimbali za nchi hiyo. Nyota huyo anayecheza katika klabu ya Barcelona alialikwa na shule ya soka ya Qatar Aspire ambao wana tawi lao nchini humo kwa ajili ya kwenda kwenye kampeni ya kupiga vita ugonjwa wa malaria. Kwa mujibu wa waratibu ya ziara hiyo maelfu ya neti ambazo zitakuwa na picha ya Messi zitasambazwa kwa watoto na familia katika vijiji mbalimbali nchini humo. Messi atasafiri kwa helikopta kwenda Saly eneo la karibu na mji wa Dakar ambapo atatembelea nyumba za yatima na kuongea na wenyeji wa hapo jinsi watakavyoweza kujikinga na malaria.