
Friday, July 12, 2013
KAMPUNI YA MADUKA NCHINI BRAZIL WATISHIA KWENDA MAHAKANI KUHUSU USAJILI NEYMAR

FIFA YA FUATILIA KWA KARIBU KASHFA YA UPANGAJI MATOKEO
SHIRIKISHO la Soka
Duniani-FIFA linafuatilia kwa karibu kashfa ya upangaji matokeo
inayozikabili vilabu viwili vya soka vya ridhaa nchini Nigeria
iliyotokea wiki iliyopita. Katika
matokeo ambayo yanaonekana kama ya mchezo wa kriketi, klabu ya Plateau
United Feeders iliibugiza Akurba FC kwa mabao 79-0 wakati Police Machine
wao waliitandika Bubayaro FC kwa mabao 67-0 mwishoni mwa wiki
iliyopita. Hatua uchunguzi kwa vilabu hivyo imekuja kutokana na timu hizo kuhitaji matokeo ya aina hiyo ili waweze kupanda daraja. Ambapo
katika taarifa yake FIFA imedai kuwa inafuatilia tukio hilo la tmu hizo
za Nigeria kwa karibu ili kuona jinsi gani Shirikisho la Soka la nchi
hiyo, NFF litatatua tatizo hilo. FIFA
inafanya hivyo kwa kutambua kuwa suala hilo ni la ndani hivyo NFF ina
wajibu wa kufanya uchunguzi na kuchukua hatua zinazostahiki kama
ikigundulika aina yoyote ya udanganyifu katika mechi hizo.
TAIFA STARS SASA MMEIVA KUPAMBANA- TENGA

Akizungumza
na wachezaji wa timu hiyo kambini kwao hoteli ya Tansoma, Dar es
Salaam, Rais Tenga aliwaambia kuwa kiwango walichoonesha kwenye mechi
zilizopita za mchujo za Kombe la Dunia dhidi ya Morocco na Ivory Coast
kimethibitisha hilo.
“Kiwango
mlichoonyesha katika mechi hizo kila Mtanzania anayewafuatilia
amekiona, hivyo hatuna shaka kuwa mtatuwakilisha vizuri kwenye mechi ya
kesho dhidi ya Uganda,” amesema Rais Tenga na kuwataka kupigana kwa
ajili ya Tanzania.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kesho (Julai 13 mwaka
huu) saa 9 kamili alasiri Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itacheza na
Uganda (The Cranes) katika mechi ya kwanza ya raundi ya mwisho kuwania
tiketi ya kucheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika
Kusini.
Rais
Tenga amesema TFF, mdhamini Kilimanjaro Premium Lager, Kamati ya
Ushindi na Watanzania kwa ujumla wanawaunga mkono kwani wamekuwa
wakiboresha kiwango chao kila wanavyozidi kucheza mechi tangu wake chini
ya Kocha Kim Poulsen, Mei mwaka jana.
Wakati
huo huo, Rais Tenga ameahidi kumpatia tiketi ya kwenda Uganda kwenye
mechi ya marudiano mshabiki Wiseman Mwakyusa Luvanda anayetembea kwa
miguu kutoka Mbeya kuja Dar es Salaam kushuhudia mechi ya kesho.
“Kama
ni kweli anakuja kwa kutembea, huyu ameonyesha kiwango kikubwa cha
uzalendo kwa timu ya Taifa, nitampatia tiketi ya kwenda Kampala
kuishangilia Taifa Stars kwenye mechi ya marudiano,” amesema Rais Tenga.
POULSEN, MICHO WATABIRI MECHI KALI

Wakizungumza
na Waandishi wa Habari leo, makocha wote waliezea ubora wa wapinzani
wao, lakini wakasisitiza kuwa wanaingia uwanjani kuhakikisha wanashinda
ili kujiweka katika mazingira mazuri kwa ajili ya mechi ya marudiano
itakayochezwa Kampala wiki mbili zijazo.
Kim
alisema Uganda ndiyo inayoongoza kwa ubora wa viwango vya FIFA katika
ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati, hivyo ni changamoto kwao ingawa
wachezaji wake tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya mechi hiyo.
Naye
Micho aliyefuatana na nahodha wake Hassan Wasswa alisema Taifa Stars
imekuwa ikifanya vizuri tangu iwe chini ya Kim, na itakuwa na wachezaji
tisa wa kikosi cha kwanza kinachocheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia
wakati kwa upande wake atakuwa na wachezaji wawili tu.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Thursday, July 11, 2013
DROGBA ATANGAZA KUJENGA HOSPITAL 5 ZA KINA MAMA NA WATOTO"NCHINI IVORY" COAST
Uamuzi huu umetangazwa huko Mjini
Abidjan na Katibu wa Didier Drogba Foundation, Guy Roland Tanoh, ambae
amesema itajengwa Hospitali moja katika Miji mitano ya Ivory Coast
ambayo ni Abidjan, Yamoussoukro, Man, Korhogo na San Pedro.
Kwenye Tafrija huko
London tulichangisha na kukusanya Dola Milioni 4 na zilizobaki si tatizo
ili kukamilisha Mradi huu ambao uko moyoni kabisa mwa Drogba.”
Taasisi ya Didier Drogba ilianzishwa
Mwaka 2007 na ilipanga kujenga Hospitali yenye gharama ya Pauni Milioni 3
lakini hadi leo ilikuwa haijajengwa na Tanoh hakufafanua kama Hospitali
hiyo ni moja ya hizo tano zitakazojengwa.
Wakati huo, Drogba, mwenye Miaka 35 hivi
sasa na ambae anachezea Klabu ya Turkey Galatasaray, alisema ujenzi wa
Hospitali hiyo utatokana na malipo ya Picha na Matangazo yake na Kampuni
ya Pepsi.
TIMU YA AFRICAN LYON ILIYOSHUKA DARAJA YAPATA HASARA YA SH.180.3
TIMU
ya soka ya African Lyon ya jijini Dar es Salaam imetangaza hasara ya
sh. milioni 180.3 kutokana na ushiriki wake katika msimu uliopita wa
Ligi Kuu Tanzania Bara.
Lyon ni miongoni mwa timu tatu
zilizoshuka daraja kutoka katuika ligi hiyo kubwa ya soka nchini,
nyingine ni Toto African na Polisi Moro.
Salim
amesema katika makusanya na matumizi yao, walilazimika kutumia kiasi
cha sh. milioni 268.09 katika mzunguko wa kwanza, kabla ya kutumia sh.
123.6.
"Katika matumizi yote haya, fedha ambayo tumeiingiza kama
klabu kupitia viingilio na vyanzo vingine ni sh. milioni 207.6, na hapo
ndipo unapopata tofauti ya sh. milioni 180.3, ambayo ni hasara," Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Lyon, Rahim Kangezi,
alisema soka ya Tanzania inaendeshwa kwa hasara huku wenye dhamana ya
kusaidia wakiwa hawatendi haki kwa baadhi ya vipengele.
Kangezi alisema timu yake imeingia katika hasara ya sh. milioni 180.3 kutokana na uendeshaji, lakini bado wameshuka daraja, huku akisisitiza kuwa hakuna anayeshutumiwa kwa kushuka kwa timu hiyo"Unaweza kuona changamoto ambayo tunakumbana nayo katika uendeshaji wa taasisi kamam a hizi, tunapopiga kelele kwa wadhamini kutuwahishia fedha tunamaanisha."Angalieni mfano mdogo kwa fedha za wadhamini (Vodacom), ambazo awamu ya mwisho zimetufikia Mei mwaka huu, tukiwa tumebakiza mechi moja ya Ligi Kuu, sasa zingetusaidia katika nini? Alihoji mmiliki huyo.
Kangezi alisema timu yake imeingia katika hasara ya sh. milioni 180.3 kutokana na uendeshaji, lakini bado wameshuka daraja, huku akisisitiza kuwa hakuna anayeshutumiwa kwa kushuka kwa timu hiyo"Unaweza kuona changamoto ambayo tunakumbana nayo katika uendeshaji wa taasisi kamam a hizi, tunapopiga kelele kwa wadhamini kutuwahishia fedha tunamaanisha."Angalieni mfano mdogo kwa fedha za wadhamini (Vodacom), ambazo awamu ya mwisho zimetufikia Mei mwaka huu, tukiwa tumebakiza mechi moja ya Ligi Kuu, sasa zingetusaidia katika nini? Alihoji mmiliki huyo.
Akizungumzia
kuhusu uendeshwaji wa Ligi Kuu na changamoto walizokutana nazo, Kangezi
alisema bado hakujakuwa na usimamizi mzuri katika kuhakikisha kuwa ligi
hiyo inakuwa bora.
"Tulifanikiwa pia kuileta timu kubwa ya Ligi
Kuu ya Brazil (Atletico Parenese) kwa ziara ya kimichezo nchini, tulitoa
wachezaji watano kwa ajili ya kujaribu soka ya kulipwa sambamba na
kufanya semina mbili juu ya uongozi wa michezo," aliongeza.
Subscribe to:
Posts (Atom)