SIR ALEX FERGUSON Meneja wa klabu ya
Manchester United,anatarajia kustaafu kuinoa klabu
hiyo ifikapo mwishoni mwa msimu huu Katika mechi ya mwisho ya BPL dhidi ya West Bromich albion mei 18 mwaka huu baada ya kuifundisha kwa kipindi cha
miaka 26 yenye mafanikio makubwa. Ferguson
raia wa Scottland mwenye umri wa miaka 71 ameshinda mataji 38 tok
alipochukua mikoba ya Ron Atkinson Novemba 1986, likiwemo taji la Ligi
Kuu nchini Uingereza msimu huu. Mataji hayo yanajumuisha 13 ya ligi, mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, matano ya Kombe la FA na manne ya Kombe la Ligi.
Ferguson amesema uamuzi
huo wa kustaafu ni uamuzi ambao ameufikiria kwa kipindi kirefu na
kujiridhisha kwamba sasa ni muda muafaka wa kufanya hivyo. Kocha
huyo amesema amesema ilikuwa ni muhimu kwake kustaafu huku akiiacha
klabu hiyo ikiwa imara na anaamini amefanya hivyo na anategemea
itaendelea kuwa juu kwa kipindi kirefu kijacho kutokana na damu changa
atakazoziacha.
FERGUSON-MATAJI YAKE:
-PREMIER LEAGUE: 1993, 1994, 1996, 1997, 1999,
2000, 2001, 2003, 2007, 2008, 2009, 2011, 2013.
-FA CUP: 1990, 1994, 1996, 1999, 2004
-LEAGUE CUP: 1992, 2006, 2009, 2010
-UEFA CHAMPIONS LEAGUE: 1999, 2008
-UEFA CUP WINNERS CUP: 1991
-FIFA CLUB WORLD CUP: 2008
-UEFA SUPER CUP: 1992
-FIFA INTER-CONTINENTAL CUP: 1999
-FA CHARITY/COMMUNITY SHIELD: 1990, 1993, 1994, 1996, 1997, 2003, 2007, 2008, 2010, 2011