Wednesday, May 8, 2013

TIMU YA TAIFA YA BRAZIL KUZINDUA UWANJA WA MARICANA .

TIMU ya taifa ya Brazil inatarajiwa kuzindua rasmi uwanja wake uliokuwa katika matengenezo wa Maricana wakati watakapoikarinisha Uingereza katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki mwezi ujao. Mapema ilifahamika kuwa kabla ya mchezo huo kungekuwa na mechi ya majaribio Mei 15 lakini halmashauri ya jiji la Rio de Janeiro liliahirisha mchezo huo kutokana na sababu ambazo hazikuwekwa wazi. Uwanja huo ambao utatumika kwa ajili ya michuano ya Kombe la Shirikisho baadae mwezi ujao na Kombe la Dunia 2014 ulifunguliwa mwishoni mwa mwezi jana huku ukiwa umechelewa kwa miezi minne. Mechi baina ya Brazil na Uingereza mbayo itahezwa Juni 2 mwaka huu katika uwanja huo wenye uwezo wa kubeba mashabiki 78,000 ndio itakuwa pekee kabla uwanja huo haujatumika kwa ajili ya michuano ya Kombe la Shirikisho kuanzia Juni 15 hadi 30 mwaka huu. Ukarabati wa uwanja huo ambao umewahi kuweka historia ya kuingiza watu wengi zaidi wanaofikia 199, 858 katika mchezo wa fainali za Kombe la Dunia mwaka 1950, umegharimu kiasi cha dola milioni 448 huku ukipunguzwa na kuwa na uwezo wa kuingiza watu 78,838 kwasasa.