Wednesday, May 8, 2013

YANGA KUJIWEKA SAWA KWA WATANI WA JADI SIMBA

WANDINGA wa Jangwani mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga, kinatarajia kuingia  kambini kesho kutwa Ijumaa kwa lengo i ya kujiweka sawa na mechi dhidi ya watani wao Simba utakaopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Mei 18.
Kwa mujibu wa habari tulizofanikiwa kuzipata kutoka ndani ya klabu hiyo, bado haijaamuliwa mahali timu itakapoweka machimbo  lakin sehemu hizi zinatazamwa sana kati ya Zanzibar na Bagamoyo mkoani Pwani.
Yanga kwa sasa inaendelea kujiweka  sawa katika dimba la uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola ulioko Mabibo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mtanange wao dhidi ya watani wao wa jadi simba sc mchezo utakaopigwa tarehe 18 mei 2013.
Vijana hao wa Jangwani, wametwaa ubingwa msimu huu baada kufikisha pointi 57 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine.