Monday, June 24, 2013

ARSHAVIN SASA AFIKIRIA KURUDI ALIPOTOKA KISOKA CLUB YA "ZSP"

Baada ya kuitumikia Arsenal kwa muda wa miaka mitano nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Urussi, Andrei Arshavin anategemewa kukamilisha taratibu za kurejea klabu yake ya zamani ya Zenit Saint PetersburgKlabu hiyo ndio ilimuwezesha arshavin mwenye miaka 32 akiwa kinda kabla ya Arsenal kumuona na kumyakuwa. aidha Arshavin ambaye alikaa Zenit kwa mkopo kwa muda wakati wa msimu wa pili wa 2011-2012 kwa sasa yuko huru baada kuachwa na Arsenal mwishoni mwa msimu huu. hata hivyo nyotahuyo ni moja kati ya wachezaji waliokuwemo katika kikosi cha Zenit kilichonyakuwa taji la Europa League mwaka 2008 na pia katika kikosi cha Urusi kkilichoshiriki michuano ya Ulaya 2008 kabla ya kwenda Arsenal.