Monday, June 24, 2013

FIFA YASEMA RAVSHAN AKIRI KUWAPA ITALY BAO LA PILI-KOMBE LA MABARA

SHIRIKISHO la Soka Dunia-FIFA limedai kuwa mwamuzi Ravshan Irmatov amekiri kuwapa Italia bao la pili kwa makosa wakati wa mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya timu hiyo na Brazil ambao ndio wenyeji hao walitoa dozi ya mabao 4-2. Mabao hayo yalitiwa kimianina Giorgio Chiellini.
aidha bao hilo lilikubaliwa ingawa mwamuzi alishapuliza filimbi kuashiria penati kwenda kwa Italia kitendo ambacho kiliwaudhi wachezaji wa Brazil na kuzonga mwamuzi juu ya uwamuzi wake huo. FIFA imesema kuwa mwamuzi huyo wa Uzbekstan baadae alikiri kufanya kosa hilo na kukiri kupuliza filimbi kuashiria penati. Lakini pamoja na kukiri kutenda kosa kwa mwamuzi huyo FIFA hawajathibitisha kama watamrudisha nyumbani au ataendelea kuchezesha mechi za nusu fainali ya michuano hiyo.