Monday, June 24, 2013

JE?UNAMFAHAMU KWA UZURI DAVID SILVA KATIKA ULIMWENGU WA SOKA TAFAKARI ZAIDI".

             DAVID SILVA
David Silva Euro 2012 vs France 01.jpg
Taarifa kuhusu yeye
Full nameDavid Josué Jiménez Silva
Date of birth8 January 1986 (age 27)
Place of birthArguineguín, Spain
Height1.70 m (5 ft 7 in)
Playing positionAttacking midfielder / Winger
Taarifa kuhusu club
Current clubManchester City
Number21
Timu za Ujana
1995–2000UD San Fernando
2000–2003Valencia
Timu za Ukubwa
Mwaka   TimuMechiGoli
2003–2004Valencia B14(1)
2004–2010Valencia119(21)
2004–2005 Eibar (mkopo)35(4)
2005–2006Celta Vigo (mkopo)34(4)
2010–Manchester City103(14)
Timu ya Taifa
2001–2002Spain U166(2)
2002–2003Spain U1720(5)
2004–2005Spain U1914(5)
2005Spain U205(4)
2004–2006Spain U219(7)
2006–Spain74(20)
David Josué Jiménez Silva alizaliwa 8 Januari 1986 Arguineguín huko Las Palmas Hispain ni mchezaji mpira mhispania ambaye kwa sasa anachezea timu ya Man city na timu ya taifa ya Uhispania.Silva ana uwezo wa kucheza upande wowote au kama namba 10  na wakati mwingine kama mshambulizi msaidizi.Ni mchezaji mwenye mwili mdogo, na mara nyingi hulinganishwa na Aimar Pablo, alipochukua nafasi yake huko Valencia, akivalia nambari iliyohusishwa sana na Aimar; namba 21.
WASIFU WA KLABU
Silva alianza kucheza mpira wa kulipwa msimu wa 2004-05 katika Ngazi ya pili katika timu ya SD Eibar, akiwa amekopwa kutoka Valencia CF na alicheza mechi 35 katika daraja hilimna kufunga mabao matano.Msimu uliofuatia, alikopwa tena, lakini wakati huu alikopwa na timu ya Celta de Vigo, ambapo alicheza mechi 34, na kufunga mabao manne. 
Baada ya kucheza mechi mbili ambazo aliingia uwanjani katika dakika za mwisho za mechi hizo, ambapo mechi ya kwanza iliisha kwa Celta de Vigo kushinda 2-0 nyumbani dhidi ya Malaga CF tarehe 28 Agosti 2005.
Silva akamaalizia msimu huo kama mshambulizi bora huku timu hii ya Kigalisia ikifuzu katika kombe la UEFA moja kwa moja kutoka daraja la pili.Katika misimu miwili, alikosa kucheza mechi sita tu ilhali alifunga mabao 14 (bao la kwanza alilifunga tarehe 5 Novemba 2006 katika tasa ya 1-1 ugenini RCD Espanyol). Baada ya kutocheza kwa muda wa miezi mitatu kutokana na jeraha la kisigino ambapo alifanyiwa upasuaji,
Silva alirejea kikosini katikati mwa Desemba.Silva aliwakilishwa Uhispania akiwa na Cesc Fabregas mara ya kwanza mwaka wa 2003 katika michezo ya ubingwa duniani ya FIFA ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 huko Finland, ambapo alifunga mabao matatu.
Mwaka wa 2006, alijiunga na timu ya Uhispania ya wachezaji wasiozidi umri wa 21 na alifunga mabao manne katika kombe la vijana duniani la FIFA mwaka 2005; hii ilimwezesha kunyakua nafasi ya 4 katika orodha ya wafungaji bora, pamoja na mshambulizi mwitaliano Graziano Pellè.
WASIFU WA TIMU YA TAIFA
Silva alichezea mara ya kwanza timu kuu ya Uhispania tarehe 15 Novemba 2006 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Romania ambapo timu yake ilishindwa 1-0 nyumbani. Aliendelea kutajwa katika orodha ya timu ya Uhispania baada ya kuchangia vizuri katika mechi zake za kwanza.
Tarehe 22 Agosti 2007, Silva aliifungia Uhispania mabao yake ya kwanza kikosini mwa Uhispania, na alifunga mara mbili katika mechi hiyo ambapo waliishinda Ugiriki 3-2 katika mechi ya kirafiki.
Baadaye aliitwa ajiunge na kikosi cha wachezaji 23 ambao wangeiwakilisha nchi yao katika dimba la Euro 2008.
Katika nusu fainali Silva alifunga bao la tatu la Uhispania dhidi ya Urusi baada ya ushambulizi wa haraka ambayo Cesc Fabregas alimpigia krosi Silva, ambaye alitia mpira ndani ya lango la Igor Akinfeev kwa kutumia mguu wake wa kushoto.
Katika fainali, Silva alihusika katika tukio fulani na mjerumani Lukas Podolski. Baada ya kumvuta Podolski chini, Podolski alimwenedea Silva na kuzua ubishi mkali ambao haukuadhibiwa na mwamuzi.
Muda mfupi baadaye, kocha wa timu ya Uhispania, Luis Aragonés, alimwondoa Silva na kuleta Santi Cazorla ili kuzuia wezekano la vita.