Friday, June 28, 2013

HISPAIN YATINGA FAINALI SASA KUUMANA NA WENYEJI BRAZIL

Close shave: Spain moved through to the Confederations Cup final after beating Italy on penalties in FortalezaTimu ya taifa ya hispain imefanikiwa kutinga hatua ya fainali baada ya kuitooa Italia katika Kombe la Mabara kwa ushindi wa matuta wa 7-6 mjini Fortaleza, kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 katika mchezo wa Nusu Fainali usiku huu.
Wataliano walifungwa na Waspanyola katika Fainali ya Euro mwaka jana wameshindwa kulipa kisasi na sasa Fainali ya michuano hiyo mwaka huu Jumapili Uwanja wa Maracana, itawakutanisha wenyeji La Roja na Brazil wenyeji.
Leonardo Bonucci wa Italia alikosa moja ya penalti 14 na Jesus Navas akaweka nyavuni mkwaju wa mwisho na kuipeleka Hispania Fainali.
 TUTAFAKARI KUELEKEA FAINALI JE NANI KUIBUKA NA UBINGWA"
USO KWA USO
JUMLA: Mechi 8
USHINDI: Brazil 4 Spain 2
SARE: 2
MAGOLI JUMLA: Brazil 11 Spain 8
Mechi zenyewe:
FIFA KOMBE LA DUNIA:
Jumla: Mechi 5
USHINDI: Brazil 3 Spain 1
SARE: 1
MAGOLI JUMLA: Brazil 10 Spain 5
1986  Spain 0 Brazil 1 {Guadalajara, Mexico}
1978  Brazil 0 Spain 0 {Mar Del Plata, Argentina}
1962  Brazil 2 Spain 1 {Vina Del Mar, Chile}
1950  Brazil 6 Spain 1 {Rio De Janeiro, Brazil}
1934  Spain 3 Brazil 1 {Genoa, Italy}
KIRAFIKI:
Jumla: Mechi 3
USHINDI: Brazil 1 Spain 1
SARE: 1
MAGOLI: Spain 3 Brazil 1
1999  Spain 0 Brazil 0 {Vigo, Spain}
1990  Spain 3 Brazil 0 {Gijon, Spain}
1981  Brazil 1 Spain 0 {Salvador, Brazil}