![]() |
Dimba la Uwanja wa Azam Complex Chamazi |
Yanga SC Kupitia Uongozi wake umetanabisha kuwa upo tayari kuweka kambi Chamazi kufuatia ofa
waliyoitoa Azam ya kuwataka wakaweke kambi maeneo hayo kwa ajili ya kujiweka sawa na
mchezo wa raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri.
KAama unakumbuka wiki iliyopita uongozi wa Azam FC ulikataa ombi la Al Ahly kuweka kambi
kwenye eneo lao hilo wakati watakapokuja nchini kucheza dhidi ya Yanga katika
hatua hiyo baada ya kufanikiwa kuitoa Komorozine ya morroco.
![]() |
Wachezaji Wa Yanga Wakiwa Katika Swimming Pool |
"Katika hali ya kawaida hakuna mtu anaeweza kukataa ofa kama hiyo, iwapo Azam wameamua kutusaidia sisi tupo
tayari ila tunamsikiliza upande wa benchi la ufundi kupitia Kocha Mkuu mwalimu Hans Van Pluijm anahitaji kambi ya aina gani
ili kuweza kujiandaa.
"Hata hivyo Bin Kleb amesema Kocha
ndiye anayejua aina ya timu anayotarajia kukutana nayo, hivyo uongozi
unamwachia kila kitu na yeye ndiye atakayetoa maamuzi.