Friday, February 14, 2014

TFF YAWATAKA WANACHAMA WAKE KUFAVYA MAREKEBISHO YA KATIBA KABLA YA MACHI 20

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeamuru wanachama wake wote kufanya marekebisho ya katiba zao kabla ya Machi 20, mwaka huu, hivyo kutengua tarehe ya mkutano mkuu wa Simba.

Simba iliyo chini ya mwenyekiti wake, Ismail Aden Rage, ilipanga kufanya mkutano wake huo Machi 23, mwaka huu kwa ajenda moja ya marekebisho ya katiba yao ambapo sasa imeamua kufanya mkutano huo mapema, Machi 16 ili kwenda sawa na maagizo ya TFF.
Ofisa Habari wa Simba, Asha Muhaji alisema kuwa walitumiwa barua ya maagizo hayo na TFF wiki hii na hivyo wameamua kuurudisha nyuma ili marekebisho hayo yafanyike kabla ya Machi 20.
“Mkutano wa marekebisho hautafanyika tena Machi 23 kama wanachama na wadau wote wa Simba walivyokuwa wakifahamu, tumepata barua kutoka TFF inayotuelekeza kufanya mkutano huo kabla ya Machi 20, hivyo sasa mkutano utakuwa Machi 16.