Thursday, February 13, 2014

MESSI AWEKA REKODI FC BARCA JANA ATUPIA 1

Mshambuliaji mahiri wa argentina na club ya barcelona Lionel Messi amefanikiwa kuweka rekodi nyingine ya mabao wakati Barcelona ikitinga fainali ya Kombe la Hispania kuelekea mechi na Manchester City wiki ijayo Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Messi alifanikiwa kuifungia timu yake jana katika sare ya 1-1 na Real Sociedad na kufikisha mabao 335 hivyo kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika klabu hiyo ya Hispania.

Barca imeingia fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-1 baada ya awali kushinda 2-0 na sasa itakutana na Real Madrid katika mechi ya kuwania Kombe.
COPA del REY
NUSU FAINALI

{Saa za Bongo}

Marudiano

Jumanne Februari 11

Atletico de Madrid 0          Real Madrid CF 2 {0-5}

Jumatano Februari 12

Real Sociedad 1 FC Barcelona 1 {1-3}

FAINALI

Aprili 19

Real Madrid v Barcelona