Thursday, February 13, 2014

ENGLAND YAPOROMOKA VIWANGO VYA FIFA VS SPAIN 1

FIFA_LOGO_BESTShirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA leo limetoa Listi ya Ubora Duniani  huku Nchi 3 za Juu, Spain, Germany na Argentina, bado ziko pale pale na Portugal kupanda nafasi moja na kukamata Nambari ya 4 huku Tanzania ikipanda Nafasi mbili na kushika Nafasi ya 116.
Brazil, Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia hapo Juni, wamekwea Nafasi moja hadi Nafasi ya 9 lakini England imezidi kuporomoka na safari hii imeanguka Nafasi mbili na kuwa wa 15.
Nchi ya Afrika ambayo iko Juu kabisa ni Ivory Coast ambayo iko Nafasi ya 23 baada ya kuanguka Nafasi 6.
Listi nyingine ya Ubora itatolewa hapo Machi 13.
20 BORA:
1. Spain
2. Germany
3. Argentina
4. Portugal (+1)
5. Colombia (-1)
6. Switzerland (+2)
7. Uruguay (-1)
8. Italy (-1)
9. Brazil (+1)
10. Netherlands (-1)
11. Belgium
12. Greece
13. United States (+1)
14. Chile (+1)
15. England (-2)
16. Croatie
17. Bosnia-Herzegovina (+2)
18. Ukraine
18. France (+2)
20. Denmark (+5)