Wednesday, August 27, 2014

AZAM FC KESHO YATARAJI KUANZA TIZI ZA VPL YA SEPT 20

Timu ya Azam fc Mabingwa wa Bara Kesho wanatarajiwa kuanza tena mazoezi Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam baada ya kurejea kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mjini Kigali, Rwanda.

Akizungumza na mkali wa dimba tz.blogspot.com afisa habari wa timu hiyo jaffari iddi maganga amesema kuwa wachezaji wote wataanza mazoezi kesho, kasoro wale ambao wameitwa timu ya taifa.

Maganga amesema kwamba wachezaji wawili, Aishi Manula na Kevin Friday japokuwa hawapo kwenye kikosi cha Taifa Stars, wao wamepewa mapumziko zaidi- hivyo si lazima waanze kesho.
Aidha Maganga amesema kwamba Simba SC waliomba mchezo wa kirafiki na wao wikiendi hii, lakini imeshindikana kwa sababu kocha Joseph Marius Omog amesema hawezi kuwa na mechi baada ya mazoezi ya siku mbili.
Mwalimu amesema mchezo wanaotaka Simba SC labda wiki ijayo, kwa sababu hawezi kufanya mazoezi Alhamsi na Ijumaa halafu baada ya hapo awe na mechi ngumu.

Mcamreoon huyo ambaye aliipatia azam Ubingwa msimu uliopita hivi karibuni ameifikisha Azam FC Robo Fainali ya Kombe la Kagame mjini Kigali kabla ya kutolewa na El Merreikh ya Sudan, iliyoibuka bingwa wa michuano hiyo mwaka huu.