Friday, November 28, 2014

DR SHEIN ASEMA KATIKA KUKUZA MPANGO WA UCHUMI NA KUONDOA UMASKINI ZANZIBAR SECTA YA UTALII NDIO SECTA YAKUUNGWA MKONO.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dokta, Ali Mohamed Shein amesema kuwa katika Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini Zanzibar (MKUZA), sekta ya utalii ndio sekta mama na nyegine zimekuwa zikiongeza nguvu hivyo inahitaji kuendelea kuungwa mkono ndani na nje ya nchi.
Dokta, Shein ameyasema hayo wakati alipofanya mazungumzo na Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada Jack Mugendi Zoka,  Ikulu mjini Zanzibar aliyefika kwa ajili ya kuaga kwenda katika kituo chake kipya cha kazi nchini humo  kufuatia uteuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete hivi karibuni.
Katika maelezo yake Dokta Shein amemueleza Balozi huyo mpya wa Tanzania nchini Cadana kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imekuwa ikifanyaa juhudi za makusudi katika kuhakikisha sekta ya utalii inaimarika na inaendelea kuwa sekta mama na muhimu hapa nchini.
Akieleza juu ya sekta ya uwekezaji Dokta, Shein amemueleza Balozi Zoka kuwa mbali ya kutilia mkazo uwekezaji katika ujenzi wa mahoteli pia, Serikali imekuwa ikitilia mkazo uwekezaji katika Hospitali za kisasa za binafsi ambazo zinatibu maradhi maalum.