KLABU kongwe jijini Instabul ya Galatasaray wanatarajia kumteua kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Uturuki Hamza Hamzaoglu kuwa meneja mpya wa klabu hiyo baada ya kutimuliwa kwa Muitaliano Cesare Prandelli.

Hamzaoglu amekuwa akiitumikia Uturuki chini ya kocha mkuu Fatih Terim toka mwaka 2013, na uamuzi wake huo umekuja baada ya kufanya mazungumzo na kocha huyo.

Prandelli alitua katika klabu hiyo Julai mwaka huu akichukua nafasi ya Muitaliano mwenzake Roberto Mancini na kupewa mkataba wa miaka miwili uliokuwa na thamani ya euro milioni 2.3.