Sunday, November 23, 2014

WENGER ALAUMU SAFU YAKE YA ULINZI DHIDI YA MAN UNITED.

Kocha wa Arsenal Arsene wenger amesema kuwa safu ya ulinzi ya Arsenal ni hafifu baada ya kushindwa 2-1 na Manchester United katika uwanja wa Emirates.
Arsenal walipatikana wakiwa wazi katika safu ya nyuma walipojaribu kutafuta bao la kukomboa baada ya Kieran Gibs kujifunga.
Wenger amesema kuwa kwa sasa safu hiyo ya ulinzi haina uzoefu wa kutosha kuweza kusoma mechi.
Katika mechi hiyo Arsenal walifanya mashambulizi 23 katika lango la Manchester United.
Wenger amesema Mwisho wa mechi hatukuwa imara katika safu ya Ulinzi na tulifanya makosa ambayo walichukua fursa na kutuadhibu.