Sunday, November 23, 2014

LIVERPOOL HOI VIPIGO MFULULIZO WAKAA 3-1 KWA C"PALACE

Majogoo wa Jiji la Landon Liverpool wakiwa katika dimba la Ugenini huko Selhurst Park Jijini London waliongoza baada ya Sekunde 90 tu Bao la Rickie Lambert lakini walijikuta wakiambulia kipigo cha Bao 3-1 na Crystal Palace katika Mechi ya Ligi Kuu England.
Palace walisawazisha Bao katika Dakika ya 17 kwa Bao la Dwight Gayle alienasa Shuti la Yannick Bolasie lililopiga Posti na kumrudia.
Kipindi cha Pili Dakika ya 78 Joe Ledley aliwapeleka Palace mbele 2-1 na kisha Dakika 3 baadae Frikiki ya Mita 25 ya Mile Jedinak ilitinga na kuwapa Palace Bao lao la 3.
Mechi hii imewaacha Wadau wa Liverpool wakihoji uchezaji wa Nahodha wao Steven Gerrard na Raheem Sterling ambao wameonyesha kufifia mno.
Kipigo hiki cha Leo kinawafanya Liverpool wawe wamechapwa Mechi 3 mfulilizo za Ligi na kushinda Mechi 1 tu kati ya 5 zilizopita na kuwaacha wakiwa Nafasi ya 12 wakiwa Pointi 18 nyuma ya Vinara Chelsea.
Katika Mechi zao 2 zilizopita, Liverpool wametandikwa 2-1 na Chelsea na 1-0 na Newcastle.
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA/MATOKEO:
Jumapili Novemba 23
Crystal Palace 3 Liverpool 1        
1900 Hull City v Tottenham  
Jumatatu Novemba 24
2300 Aston Villa v Southampton 
Jumamosi Novemba 29
1545 West Brom v Arsenal
1800 Burnley v Aston Villa          
1800 Liverpool v Stoke              
1800 Man Utd v Hull                 
1800 QPR v Leicester                
1800 Swansea v Crystal Palace            
1800 West Ham v Newcastle                
2030 Sunderland v Chelsea                     
MSIMAMO:
BPL-TEBO-23NOV-A