Sunday, November 23, 2014

NFA YA ZAMBIA YAMNYEMEREA PHIRI KUIONOA TIMU YA TAIFA


Shirikisho la Soka la Namibia (NFA), limeendelea kuonyesha nia ya kumpata Kocha Patrick Phiri kukinoa kikosi chake cha timu ya taifa.
Mmoja wa mtandao wa michezo wa Namibia umeandika kuwa NFA imefanya mazungumzo na Phiri kumshawishi ajiunge na kuchukua nafasi ya kocha wa sasa.
Kwa sasa, Namibia inanolewa na nyota wake wa zamani, Ricarco Manetti ambaye aliwahi kung’ara na Santos ya Afrika Kusini.
Akizungumzia hilo Phili kutoka Lusaka Zambia amekiri kwa mara nyingi kuwa aliwahi kuzungumza na uongozi wa NFA lakini si hivi karibuni.
Phiri yuko mapumzikoni kwao nchini Zambia, anatarajiwa kurejea nchini siku chache zijazo kiuendelea na kazi.