Friday, November 7, 2014

TFDA:MAMA NTILIE MBEYA WATAKIWA KUBORESHA MAENEO YA KAZI.

MAMLAKA  ya chakula na dawa TFDA, kanda ya nyanda za juu kusini imekiri kuwa mazingira wanayofanyia biashara baadhi ya mamantiliye jijini Mbeya, hayakikidhi viwango vya usafi hali inayoweza kuhatarisha afya za watumiaji wa vyakula.
Hayo yamebainishwa na kaimu meneja wa TFDA, wa kanda hiyo Rodney Analanga wakati akizungumza na Highlands fm radio ofisini kwake.
Analanga amesema kuwa mamlaka hiyo haitasita kuwachukulia hatua za kisheria mama ntiliye ambao hawafuati kanuni za usafi wa chakula ikiwa ni pamoja na kutumia maji safi na vyombo vilivyooshwa na maji safi na salama.
Kauli hiyo imekuja kufuatia Highlands fm, kufanya uchunguzi kwenye mabanda ya mama ntilie katika eneo la Sido jijini Mbeya na kubaini kuwa wafanyabiashara hao hawakidhi viwango vya usafi wa chakula.