
Hayo yamebainishwa na kaimu meneja wa TFDA, wa kanda hiyo Rodney Analanga wakati akizungumza na Highlands fm radio ofisini kwake.
Analanga amesema kuwa mamlaka hiyo haitasita kuwachukulia hatua za kisheria mama ntiliye ambao hawafuati kanuni za usafi wa chakula ikiwa ni pamoja na kutumia maji safi na vyombo vilivyooshwa na maji safi na salama.
Kauli hiyo imekuja kufuatia Highlands fm, kufanya uchunguzi kwenye mabanda ya mama ntilie katika eneo la Sido jijini Mbeya na kubaini kuwa wafanyabiashara hao hawakidhi viwango vya usafi wa chakula.