
Vitendo anavyodaiwa kufanyiwa mtoto huyo ni kupigwa sehemu
mbalimbali za mwili wake, kisha kung’olewa jino, kujeruhiwa eneo la mdomo na
mguuni, pamoja na kuumizwa sehemu zake za siri hali iliyopelekea mwili wake
kudhoofu.
Mtoto huyo ambaye mama yake mzazi alikwishafariki dunia amedai
kuwa amekuwa akipigwa mara kwa mara na mama yake wa kambo na wakati mwingine na
baba yake hali inayomsababishia majeraha na kisha kumwacha ndani
bila kumpatia matibabu mpaka pale majirani walipobaini na kutoa taarifa kwenye
uongozi wa serikali za mitaa.
Nae Mjumbe wa serikali ya mtaa wa Airport,kata ya Ileya bi, Rehema
Mohamed amelaani tukio hilo na kusisitiza kuwa sio la mara ya kwanza na
ameziomba mamlaka husika kupita mitaani na kwa ajili ya kutoa elimu.
Hata hivyo juhudi za kumtafuta mtuhumiwa huyo hazikuzaa matunda
kwani amekimbia mara baada ya tukio hilo.