
hivyo mpaka sasa
Coastal union imekamilisha usajili wa wachezaji wanne wapya, akiwemo mchezaji
bora wa Ligi Kuu ya Zanzibar msimu huu, Abdallah Othman Ally.
Ally anayecheza
upande wa pembeni juu kushoto mwenye speed na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira,
amesaini Mkataba wa miaka miwili na Coastal Union ambayo tangu ipande tena Ligi
Kuu mwaka juzi, imepania kurejesha makali yake. Mbali na Ally anayechezea pia
timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes.
Wagosi wa Kaya
wamemrejesha kiungo waliyemuibua mwaka 2000 kabla ya kufuata maslahi Moro
United, baadaye Simba SC na Geffle FF ya Sweden’.
Boban amerejea
Tanga alipoanzia kucheza soka ya ushindani mwaka 2000 chini ya kocha maarufu
zamani Mansour Magram, sasa marehemu akitokea sekondari ya Makongo, Dar es
Salaam.
Aidha wagosi hao
pia imesajili wachezaji wawili kutoka JKT Oljoro ya Arusha, kipa Said Lubawa na
sentahafu Marcus Ndehele ambapo Mwenyekiti wa Coastal Union Hemed Aurora
hmed akizungumza na mtandao huu ametanabaisha na kusema kuwa bado wanatazama
harakati za kuwanasa wachezaji watano zaidi kulingana na mapendekezo ya benchi
la ufundi.
Aidha Aurora
ameongeza na kusema kuwa huu ni usajili wa uliokuwa na malengo na si wa
kukurupuka na pia vilevile ni usajili unaotokana na mapendekezo ya benchi la ufundi
la timu chini ya kocha mkuu, Ahmed Morocco ambaye alitaka wachezaji tisa ambao
aliwapendekeza kwa majina yeye mwenyewe na sisi tumekuwa tukimfuata mmoja baada
ya mwingine na kumalizana naye.
Hivyo kwa wakati
huu bado tupo kwenye harakati za kumalizana na wengine watano ambpo Lengo letu
ni kuhakikisha kocha anakuwa na timu atakayoridhika nayo kulingana na
mapendekezo yake, hatutaki kuingilia kusajili hata mchezaji mmoja, alisema
Aurora.
Mbali na hilo
Aurora ameudokeza mtandao huu kuwa miongoni mwa wachezaji hao waliobaki mtazamo
zaidi ni kumnasa beki aliepatwa na misukosuko kama ya Boban yaani beki mwenye
nguvu na na uwezo wa kukaba Juma Nyoso.
Hata hivyo Aurora
ameongeza na kusema kuwa mazoezi ya Coastal Union yataanza wiki ya kwanza ya
mwezi Julai mwaka huu, nje kidogo ya mji ambako kikosi kitapiga kambi kujiandaa
kikamilifu kwa ajili ya msimu mpya.