Florentino Perez rais wa club ya Real
Madrid ametanabaisha kuwa ana mategemeo kuwa mshambuliaji nyota wa klabu
hiyo Cristiano Ronaldo atabakia Santiago Bernabeu katika kipindi chote
cha maisha yake ya soka. Mshambuliaji
huyo wa kimataifa wa Ureno, mapema mwaka jana alidokeza kuwa hakuwa
anafurahia maisha ya Madrid na toka wakati huko amekuwa akihusishwa na
mpango wa kurejea Manchester United pamoja na Paris Saint-Germain-PSG. Lakini
Perez amedai kuwa atafanya kila awezalo ili nyota huyo aweze kuwa na
furaha katika klabu hiyo na kumalizika muda wake wa kucheza soka akiwa
hapo. Perez pia
aluzungumzia mustakabali ya mshambuliaji mwingine Gonzalo Higuain na
kudai kuwa hakuna yoyote aliyemwambia kwamba mchezaji huyo ataondoka
kwani klabu hiyo haijamuweka sokoni katika kipindi cha usajili. Ambapo
aliongeza kuwa kama mchezaji mwenyewe ndio anataka kuondoka basi klabu
itakayomhitaji itatakiwa kuwalipa lakini mpaka sasa ahkuna klabu yoyote
iliyojitokeza kumtaka mchezaji huyo.
Tuesday, June 4, 2013
KATIKA MISUKOSUKO YA HAPA NA PALE SASA ATUA COAST"

hivyo mpaka sasa
Coastal union imekamilisha usajili wa wachezaji wanne wapya, akiwemo mchezaji
bora wa Ligi Kuu ya Zanzibar msimu huu, Abdallah Othman Ally.
Ally anayecheza
upande wa pembeni juu kushoto mwenye speed na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira,
amesaini Mkataba wa miaka miwili na Coastal Union ambayo tangu ipande tena Ligi
Kuu mwaka juzi, imepania kurejesha makali yake. Mbali na Ally anayechezea pia
timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes.
Wagosi wa Kaya
wamemrejesha kiungo waliyemuibua mwaka 2000 kabla ya kufuata maslahi Moro
United, baadaye Simba SC na Geffle FF ya Sweden’.
Boban amerejea
Tanga alipoanzia kucheza soka ya ushindani mwaka 2000 chini ya kocha maarufu
zamani Mansour Magram, sasa marehemu akitokea sekondari ya Makongo, Dar es
Salaam.
Aidha wagosi hao
pia imesajili wachezaji wawili kutoka JKT Oljoro ya Arusha, kipa Said Lubawa na
sentahafu Marcus Ndehele ambapo Mwenyekiti wa Coastal Union Hemed Aurora
hmed akizungumza na mtandao huu ametanabaisha na kusema kuwa bado wanatazama
harakati za kuwanasa wachezaji watano zaidi kulingana na mapendekezo ya benchi
la ufundi.
Aidha Aurora
ameongeza na kusema kuwa huu ni usajili wa uliokuwa na malengo na si wa
kukurupuka na pia vilevile ni usajili unaotokana na mapendekezo ya benchi la ufundi
la timu chini ya kocha mkuu, Ahmed Morocco ambaye alitaka wachezaji tisa ambao
aliwapendekeza kwa majina yeye mwenyewe na sisi tumekuwa tukimfuata mmoja baada
ya mwingine na kumalizana naye.
Hivyo kwa wakati
huu bado tupo kwenye harakati za kumalizana na wengine watano ambpo Lengo letu
ni kuhakikisha kocha anakuwa na timu atakayoridhika nayo kulingana na
mapendekezo yake, hatutaki kuingilia kusajili hata mchezaji mmoja, alisema
Aurora.
Mbali na hilo
Aurora ameudokeza mtandao huu kuwa miongoni mwa wachezaji hao waliobaki mtazamo
zaidi ni kumnasa beki aliepatwa na misukosuko kama ya Boban yaani beki mwenye
nguvu na na uwezo wa kukaba Juma Nyoso.
Hata hivyo Aurora
ameongeza na kusema kuwa mazoezi ya Coastal Union yataanza wiki ya kwanza ya
mwezi Julai mwaka huu, nje kidogo ya mji ambako kikosi kitapiga kambi kujiandaa
kikamilifu kwa ajili ya msimu mpya.
MAN CITY YAMNASA WINGA WA SEVILLA JESUS NAVAS.

Navas, mwenye Miaka 27, anategemewa kununuliwa kwa gharama ya Pauni Milioni 17.
Navas yumo kwenye Kikosi cha Spain kitakachocheza Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara huko Brazil kuanzia Juni 15.
Hadi sasa Man City haijatangaza nani
Meneja wao mpya baada ya kumtimua Roberto Mancini ingawa wengi
wanategemea Manuel Pellegrini, aliekuwa Malaga, ndio atachukua nafasi
hiyo.
NEYMAR ASEMA MESS ATAENDELEA KUTISHA ZAIDI DUNIANI.

TAIFA STAR YATUA MORROCO RASMI KWA MAANDALIZI YA MECHI ITAKAYO PIGWA JUNE 8.
Taifa Stars imewasili hapa Marrakech, Morocco leo- Juni 3 mwaka huu tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itakayochezwa Jumamosi- Juni 8 mwaka huu.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefikia hoteli ya Pullman ambayo pia Ivory Coast ilifikia ilipokuja kucheza hapa dhidi ya Morocco. Stars imetua na wachezaji 21 huku Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu waliokuwa Maputo, Msumbiji kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho na timu yao ya TP Mazembe watawasili kesho- Juni 4 mwaka huu saa 8 mchana.

Mechi kati ya Stars na Morocco itachezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za hapa wakati nyumbani itakuwa ni saa 5 usiku.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Marrakech, Morocco
Monday, June 3, 2013
ALVES AMFAGILIA MSHAMBULIAJI MPYA WA TIMU HIYO NEYMAR
BEKI wa kimataifa wa Brazil na klabu ya Barcelona, Dani Alves amedai kuwa mshambuliaji mpya wa klabu hiyo Neymar atang’ara na hatahitaji muda mrefu wa kuzoea mazingira mapya msimu ujao. Neymar mwenye umri wa miaka 21 anatarajia kuondoka klabu ya Santos kwenda Barcelona baada ya kukubalia kusaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo ambapo Alves anaamini nyota huyo atapata mafanikio akiwa Camp Nou. Alves amesema nyota huyo ana kipaji cha hali ya juu ndio maana Barcelona wakaamua kumsajili kutoka Santos na ni mategemeo yao atazoea mazingira ya Barcelona haraka kwasababu atakuwa akifanya kitu anachokipenda nacho ni kucheza soka. Neymar anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya na Barcelona leo kabla ya kumalizia taratibu za uhamisho wake.
CHELSEA YAMTAMBULISHA RASMI MTU SPESHO"MOURINHO"

MAMENEJA WA CHELSEA CHINI YA ROMAN ABRAMOVICH:
-Claudio Ranieri: Sep 2000 mpaka Mei 2004
-Jose Mourinho: Jun 2004 mpaka Sep 2007
-Avram Grant: Sep 2007 mpaka Mei 2008
-Luiz Felipe Scolari: Jul 2008 mpaka Feb 2009
-Guus Hiddink: Feb 2009 mpaka Mei 2009
-Carlo Ancelotti: Jun 2009 mpaka Mei 2011
-Andre Villas-Boas: Jun 2011 mpaka Machi 2012
-Roberto Di Matteo: Machi 2012 mpaka Nov 2012
-Rafael Benitez: Nov 2012 mpaka Mei 2013
-Jose Mourinho: Juni 2013 -
Mourinho anarejea kwa mara nyingine Chelsea na kuwakuta tena baadhi ya Wachezaji aliokuwa nao mara ya kwanza kina Petr Cech, Ashley Cole, Frank Lampard, John Mikel Obi na John Terry pamoja na Michael Essien ambae alikuwa nae huko Real alikopelekwa kwa Mkopo na Chelsea.
Akizungumza kuhusu Mourinho, Mchezaji mkongwe wa Chelsea, Frank Lampard, alisema: “Ni Meneja Bora! Nimesema hili zaidi ya mara milioni, kiasi cha kuonekana kero kwa Watu, lakini nimebahatika kufanya nae kazi!”
Subscribe to:
Posts (Atom)