Tuesday, June 4, 2013

PEREZ AWEKA WAZI KUWA RONALDO ATABAKI REAL MADRID"

Florentino Perez rais wa club ya Real Madrid ametanabaisha kuwa ana mategemeo kuwa mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Cristiano Ronaldo atabakia Santiago Bernabeu katika kipindi chote cha maisha yake ya soka. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ureno, mapema mwaka jana alidokeza kuwa hakuwa anafurahia maisha ya Madrid na toka wakati huko amekuwa akihusishwa na mpango wa kurejea Manchester United pamoja na Paris Saint-Germain-PSG. Lakini Perez amedai kuwa atafanya kila awezalo ili nyota huyo aweze kuwa na furaha katika klabu hiyo na kumalizika muda wake wa kucheza soka akiwa hapo. Perez pia aluzungumzia mustakabali ya mshambuliaji mwingine Gonzalo Higuain na kudai kuwa hakuna yoyote aliyemwambia kwamba mchezaji huyo ataondoka kwani klabu hiyo haijamuweka sokoni katika kipindi cha usajili. Ambapo aliongeza kuwa kama mchezaji mwenyewe ndio anataka kuondoka basi klabu itakayomhitaji itatakiwa kuwalipa lakini mpaka sasa ahkuna klabu yoyote iliyojitokeza kumtaka mchezaji huyo.

KATIKA MISUKOSUKO YA HAPA NA PALE SASA ATUA COAST"


Baada ya kupata misukosuko ya hapa na pale katika Club ya wekundu wa msimbazi SC kiungo Haruna Moshi Shaaban ‘Boban hatimaye amefanikiwa kutua  ndani ya jiji la tanga kuichezea Coastal union mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
hivyo mpaka sasa Coastal union imekamilisha usajili wa wachezaji wanne wapya, akiwemo mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Zanzibar msimu huu, Abdallah Othman Ally. 
Ally anayecheza upande wa pembeni juu kushoto mwenye speed na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira, amesaini Mkataba wa miaka miwili na Coastal Union ambayo tangu ipande tena Ligi Kuu mwaka juzi, imepania kurejesha makali yake. Mbali na Ally anayechezea pia timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes.
Wagosi wa Kaya wamemrejesha kiungo waliyemuibua mwaka 2000 kabla ya kufuata maslahi Moro United, baadaye Simba SC na Geffle FF ya Sweden’.
Boban amerejea Tanga alipoanzia kucheza soka ya ushindani mwaka 2000 chini ya kocha maarufu zamani Mansour Magram, sasa marehemu akitokea sekondari ya Makongo, Dar es Salaam.
Aidha wagosi hao pia imesajili wachezaji wawili kutoka JKT Oljoro ya Arusha, kipa Said Lubawa na sentahafu Marcus Ndehele ambapo Mwenyekiti wa  Coastal Union Hemed Aurora hmed akizungumza na mtandao huu ametanabaisha na kusema kuwa bado wanatazama harakati za kuwanasa wachezaji watano zaidi kulingana na mapendekezo ya benchi la ufundi.  

Aidha Aurora ameongeza na kusema kuwa huu ni usajili wa uliokuwa na malengo na si wa kukurupuka na pia vilevile ni usajili unaotokana na mapendekezo ya benchi la ufundi la timu chini ya kocha mkuu, Ahmed Morocco ambaye alitaka wachezaji tisa ambao aliwapendekeza kwa majina yeye mwenyewe na sisi tumekuwa tukimfuata mmoja baada ya mwingine na kumalizana naye.
Hivyo kwa wakati huu bado tupo kwenye harakati za kumalizana na wengine watano ambpo Lengo letu ni kuhakikisha kocha anakuwa na timu atakayoridhika nayo kulingana na mapendekezo yake, hatutaki kuingilia kusajili hata mchezaji mmoja, alisema Aurora.
Mbali na hilo Aurora ameudokeza mtandao huu kuwa miongoni mwa wachezaji hao waliobaki mtazamo zaidi ni kumnasa beki aliepatwa na misukosuko kama ya Boban yaani beki mwenye nguvu na na uwezo wa kukaba Juma Nyoso.

Hata hivyo Aurora ameongeza na kusema kuwa mazoezi ya Coastal Union yataanza wiki ya kwanza ya mwezi Julai mwaka huu, nje kidogo ya mji ambako kikosi kitapiga kambi kujiandaa kikamilifu kwa ajili ya msimu mpya.

MAN CITY YAMNASA WINGA WA SEVILLA JESUS NAVAS.

Club ya soka ya Manchester City wamefikia makubaliano na Klabu ya Spain Sevilla ya kumnunua Winga wa Kimataifa wa Spain Jesus Navas.
Navas, mwenye Miaka 27, anategemewa kununuliwa kwa gharama ya Pauni Milioni 17.
Navas yumo kwenye Kikosi cha Spain kitakachocheza Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara huko Brazil kuanzia Juni 15.
Hadi sasa Man City haijatangaza nani Meneja wao mpya baada ya kumtimua Roberto Mancini ingawa wengi wanategemea Manuel Pellegrini, aliekuwa Malaga, ndio atachukua nafasi hiyo.

NEYMAR ASEMA MESS ATAENDELEA KUTISHA ZAIDI DUNIANI.

MSHAMBULIAJI nyota mpya wa klabu ya Barcelona, Neymar ametanabaisha anataka kumsadia nyota wa klabu hiyo Lionel Messi aendelee kung’ara duniani baada ya kukamilisha taratibu zote za uhamisho wake kutoka klabu ya Santos. Neymar mwenye umri wa miaka alikamilisha uhamisho wake wenye thamani ya euro million 57 na kumaliza utata wa miezi kadhaa juu ya mstakabali wa nyota huyo. Akihojiwa mara baada ya kutambulishwa rasmi mbele ya maelfu ya mashabiki katika uwanja wa Camp Nou, Neymar amesema anataka kuisaidia timu kwasababu Barcelona ni zaidi ya klabu na pia anataka kumsadia Messi aendelee kung’ara zaidi. Nyota huyo aliendelea kusema kuwa ilikuwa ni ndoto zake kucheza katika klabu ambayo inahesabika kama mojawapo ya klabu bora duniani huku akizungukwa na wachezaji nyota. Neymar anaondoka Santos akiwa ameshinda Kombe la Brazil mwaka 2010, Kombe la Klabu Bingwa ya Amerika Kusini mwaka 2011 huku akiwa amefunga mabao 138 katika mechi 229 alizocheza akiwa katika klabu hiyo.

TAIFA STAR YATUA MORROCO RASMI KWA MAANDALIZI YA MECHI ITAKAYO PIGWA JUNE 8.

Taifa Stars imewasili hapa Marrakech, Morocco leo- Juni 3 mwaka huu tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itakayochezwa Jumamosi- Juni 8 mwaka huu.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefikia hoteli ya Pullman ambayo pia Ivory Coast ilifikia ilipokuja kucheza hapa dhidi ya Morocco. Stars imetua na wachezaji 21 huku Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu waliokuwa Maputo, Msumbiji kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho na timu yao ya TP Mazembe watawasili kesho- Juni 4 mwaka huu saa 8 mchana.
Mechi kati ya Stars na Morocco itachezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za hapa wakati nyumbani itakuwa ni saa 5 usiku.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Marrakech, Morocco

Monday, June 3, 2013

ALVES AMFAGILIA MSHAMBULIAJI MPYA WA TIMU HIYO NEYMAR

BEKI wa kimataifa wa Brazil na klabu ya Barcelona, Dani Alves amedai kuwa mshambuliaji mpya wa klabu hiyo Neymar atang’ara na hatahitaji muda mrefu wa kuzoea mazingira mapya msimu ujao. Neymar mwenye umri wa miaka 21 anatarajia kuondoka klabu ya Santos kwenda Barcelona baada ya kukubalia kusaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo ambapo Alves anaamini nyota huyo atapata mafanikio akiwa Camp Nou. Alves amesema nyota huyo ana kipaji cha hali ya juu ndio maana Barcelona wakaamua kumsajili kutoka Santos na ni mategemeo yao atazoea mazingira ya Barcelona haraka kwasababu atakuwa akifanya kitu anachokipenda nacho ni kucheza soka. Neymar anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya na Barcelona leo kabla ya kumalizia taratibu za uhamisho wake.

CHELSEA YAMTAMBULISHA RASMI MTU SPESHO"MOURINHO"

KLABU ya soka ya Chelsea imemteua rasmi Jose Mourinho kuwa meneja wa klabu hiyo kwa mkataba wa miaka minne. Mourinho ambaye ni raia wa Ureno atachukua nafasi ya Rafael banitez aliyejiunga na Napoli baada ya kuinoa klabu hiyo kwa miezi sita. Hii ni mara ya pili kwa Mourinho kurejea Stamford Brigde kama kocha kocha baada ya kuondoka miaka sita iliyopita. Mourinho ndiye alikuwa chaguo la kwanza la mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich baada ya kuinunua klabu hiyo mwaka 2003 na ndiye kocha pekee kati ya tisa waliopita klabuni hapo kuanzia kipindi hicho aliyeipa mafanikio zaidi.
MAMENEJA WA CHELSEA CHINI YA ROMAN ABRAMOVICH:
-Claudio Ranieri: Sep 2000 mpaka Mei 2004
-Jose Mourinho: Jun 2004 mpaka Sep 2007
-Avram Grant: Sep 2007 mpaka Mei 2008
-Luiz Felipe Scolari: Jul 2008 mpaka Feb 2009
-Guus Hiddink: Feb 2009 mpaka Mei 2009
-Carlo Ancelotti: Jun 2009 mpaka Mei 2011
-Andre Villas-Boas: Jun 2011 mpaka Machi 2012
-Roberto Di Matteo: Machi 2012 mpaka Nov 2012
-Rafael Benitez: Nov 2012 mpaka Mei 2013
-Jose Mourinho: Juni 2013 -

Mourinho anarejea kwa mara nyingine Chelsea na kuwakuta tena baadhi ya Wachezaji aliokuwa nao mara ya kwanza kina Petr Cech, Ashley Cole, Frank Lampard, John Mikel Obi na John Terry pamoja na Michael Essien ambae alikuwa nae huko Real alikopelekwa kwa Mkopo na Chelsea.
Akizungumza kuhusu Mourinho, Mchezaji mkongwe wa Chelsea, Frank Lampard, alisema: “Ni Meneja Bora! Nimesema hili zaidi ya mara milioni, kiasi cha kuonekana kero kwa Watu, lakini nimebahatika kufanya nae kazi!”