Wednesday, June 12, 2013

SIMBA NA YANGA YAZIWEKEA NGUMU KUSHIRIKI MICHUANO YA KAGAME-SERIKALI


SERIKALI imesisitiza kuwa timu za Simba na Yanga hazitashiriki katika michuano ya klabu Bingwa Afrika Mashariki na kati maarufu kama kombe la Kagame. Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Amos Makala ametoa taarifa hiyo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Sumve Mheshimiwa Richard Ndasa. Katika swali lake mheshimiwa Ndasa ametaka kujua msimamo wa Serikali juu ya timu za Simba na Yanga kushiriki michuano ya Kagame inayotarajia kuanza Juni 18 hadi Julai 2, mwaka huu huko Sudan Kusini. Akijibu swali hilo mheshimiwa MAKALA amesema kumekuwa na taarifa za hali ya usalama katika Nchi ya Sudan kuwa sio nzuri. Amesema kumekuwa na taarifa kulingana na hali ya usalama nchini Sudan na kwamba Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mheshimiwa Benard Membe tayari amelitolea taarifa na ndani ya Serikali kuna taarifa za kutosha kuwa Sudan hakuna usalama. Amesema msimamo wa Serikali ni kuwa hawawezi kupeleka timu mahali ambapo hakuna usalama.

KIKOSI CHA IVORY COAST KUWASILI JUNI 13


Msafara wa timu ya Taifa ya Ivory Coast (The Elephants) wa watu 80 wakiwemo wachezaji 27 unatarajiwa kuwasili nchini kesho (Juni 13 mwaka huu) kwa ndege maalum kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa Stars.

Mechi hiyo itachezwa Jumapili (Juni 16 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 9 kamili alasiri, na itachezeshwa na Charef Mehdi Abdi kutoka Algeria.

Kikosi hicho kitawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 2.50 usiku na kitafikia hoteli ya Bahari Beach iliyoko nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Timu hiyo inatarajia kuondoka saa chache baada ya mechi hiyo.

Wachezaji walioko katika kikosi hicho ni Abdoul Razak, Akpa Akpro Jean-Daniel Dave Lewis, Angoua Brou Benjamin, Arouna Kone, Aurier Serge Alain Stephane, Bamba Souleman, Barry Boubacar, Boka Etienne Arthur, Bolly Mathis Gazoa Kippersund, Bony Wilfried Guemiand, Cisse Abdoul Karim, Diarrassou Ousmane Viera na Dja Djedje Brice Florentin.

Doumbia Seydou, Gbohouo Guelassiognon Sylvain, Gosso Gosso Jean-Jacques, Kalou Salomon Armand Magloire, N’dri Koffi Christian Romaric, Sangare Badra, Serey Die Gnonzaroua Geoffroy, Sio Giovanni, Tiote Cheik Ismael, Toure Yaya Gnegneri, Traore Lacina, Ya Konan Didier, Yao Kouassi Gervais na Zokora Deguy Alain Didier.

Taifa Stars iko kambini hoteli ya Tansoma tangu iliporejea kutoka Marrakesh, Morocco ambapo leo na kesho itafanya mazoezi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 9 kamili alasiri. Ijumaa itapumzika, na itafanya mazoezi ya mwisho Jumamosi kwenye uwanja huo huo kuanzia saa 10 kamili.

Makocha wa timu zote mbili (Taifa Stars na The Elephants) watakutana na waandishi wa habari Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF kuzungumzia jinsi walivyojiandaa kwa mechi hiyo.

KIINGILIO MECHI YA STARS, IVORY COAST 5,000/-
Kiingilio cha chini katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Ivory Coast (The Elephants) itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani.

Viti vya kijani katika uwanja huo wenye uwezo wa kumeza watazamaji 60,000 viko 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu ambavyo viko 17,045 ni sh. 7,000. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 ni sh. 10,000.

Viingilio vya daraja la juu ni kama ifuatavyo; VIP C yenye watazamaji 4,060 ni sh. 15,000 wakati sh. 20,000 ni kwa VIP B yenye watazamaji 4,160. VIP A yenye watazamaji 748 kiingilio chake ni sh. 30,000.

Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo itakayoanza saa 9 kamili alasiri zitaanza kuuzwa siku mbili kabla ya mchezo (Ijumaa na Jumamosi) katika vituo vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.

Katika vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari hayo pia yatafanya mauzo ya tiketi uwanjani siku ya mechi. Tunapenda kuwakumbusha watazamaji kutonunua tiketi mikononi mwa watu au katika maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua tiketi bandia, hivyo kukosa fursa ya kushuhudia mechi hiyo.

Utaratibu katika mechi hiyo utakuwa kama ilivyokuwa katika mchezo wa Simba na Yanga, ambapo hayataruhusiwa kuingia uwanjani isipokuwa kwa yale yatakayokuwa na sticker maalumu kutoka TFF.

HATUA YA TATU RCL KUCHEZWA JUMAMOSI
Mechi za kwanza za hatua ya tatu ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu za kupanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao zitachezwa Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) wakati za marudiano zitachezwa Jumatano ya Juni 19 mwaka huu.


Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ilikutana jana (Juni 11 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za michezo iliyopita na kufanya uamuzi mbalimbali ikiwemo mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars na Machava FC ambayo haikuchezwa.

Machava FC ambayo ilishinda mechi ya kwanza iliyochezwa mjini Moshi kwa mabao 2-0 inaendelea katika hatua ya tatu kwa vile haikuhusika katika kukwamisha mchezo wa marudiano uliopangwa kuchezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA) kiliuhamishia mchezo huo kwenye Uwanja wa Mgambo mjini Mpwapwa kinyume na maelekezo ya Kamati ya Mashindano ya TFF. Kamati katika kikao chake cha awali iliekeleza kuwa mechi zote za RCL zitachezwa makao makuu ya mikoa isipokuwa kwa Morogoro ambapo timu ya Techfort FC iliruhusiwa kutumia Uwanja wa CCM Mkamba mjini Ifakara.

Hivyo timu nane zilizofuzu kucheza raundi hiyo ni Friends Rangers ya Dar es Salaam, Kariakoo ya Lindi, Katavi Warriors ya Katavi, Kimondo SC ya Mbeya, Machava ya Kilimanjaro, Njombe Mji ya Njombe, Polisi Jamii ya Mara na Stand United FC ya Shinyanga.

Wakati timu nyingine zimefuzu kwa kushinda mechi zao za raundi ya mbili, Njombe Mji imeingia hatua hiyo kwa kuwa timu yenye uwiano mdogo wa kufungwa (best looser) katika hatua ya pili.

Katika hatua hiyo mechi ni ifuatavyo; Kariakoo vs Friends Rangers, Machava FC vs Stand United FC, Polisi Jamii vs Katavi Warriors, na Kimondo SC vs Njombe Mji. Timu zilizoanza kutajwa ndizo zinazoanzia nyumbani.

Vilevile Kamati ya Mashindano imeagiza Kamishna wa mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars vs Machava FC, Mwijage Rugakingira wa Tanga ambaye alikwenda Uwanja wa Mgambo badala ya Uwanja wa Jamhuri kinyume na maelekezo ya TFF aondolewe kwenye orodha ya makamishna.

Pia waamuzi wa mechi hiyo ambao nao walikwenda Mpwapwa badala ya Dodoma Mjini wamepelekwa Kamati ya Waamuzi ya TFF kwa ajili ya kuchukuliwa hatua kutokana na tukio hilo.

Kamati ya Mashindano imekumbusha kuwa RCL ni mashindano yanayosimamiwa na TFF, hivyo maelekezo yoyote kuhusiana na mashindano hayo pia yatatoka TFF na si mahali pengine popote. Hivyo, msimamizi wa kituoa hana mamlaka ya kubadili uwanja.

Hatua ya nne ya RCL itachezwa kati ya Juni 23 na 23 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 29 na 30 mwaka huu.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Tuesday, June 11, 2013

WAALGERIA KUCHEZESHA TAIFA STARS, IVORY COAST


Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limeteua waamuzi kutoka Algeria kuchezesha mechi kati ya Taifa Stars na Ivory Coast itakayofanyika Jumapili saa 9 alasiri kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Waamuzi hao watakaochezesha mechi hiyo ya kundi C kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil wataongozwa na Charef Mehdi Abid atakayepuliza filimbi. Atasaidiwa na Hamza Hammou na Bouabdallah Omari wakati mezani atakuwa Sofiane Bousseter.

Abdi na wezake wanatarajiwa kutua nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 12 asubuhi kwa ndege ya EgyptAir. Mtathmini wa waamuzi ni Athanase Nkubito kutoka Rwanda ambaye atatua nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya RwandAir.

Kamishna wa mechi hiyo ni Bernard Mfubusa kutoka nchini Burundi ambapo atawasili nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 3.35 asubuhi kwa ndege ya Kenya Airways. Maofisa wote hao wa mechi hiyo watarejea makwao Jumatatu (Juni 17 mwaka huu).

HATUA YA TATU RCL KUCHEZWA JUMAMOSI
Mechi za kwanza za hatua ya tatu ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu za kupanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao zitachezwa Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) wakati za marudiano zitachezwa Jumatano ya Juni 19 mwaka huu.


Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo (Juni 11 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za michezo iliyopita na kufanya uamuzi mbalimbali ikiwemo mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars na Machava FC ambayo haikuchezwa.

Machava FC ambayo ilishinda mechi ya kwanza iliyochezwa mjini Moshi kwa mabao 2-0 inaendelea katika hatua ya tatu kwa vile haikuhusika katika kukwamisha mchezo wa marudiano uliopangwa kuchezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA) kiliuhamishia mchezo huo kwenye Uwanja wa Mgambo mjini Mpwapwa kinyume na maelekezo ya Kamati ya Mashindano ya TFF. Kamati katika kikao chake cha awali iliekeleza kuwa mechi zote za RCL zitachezwa makao makuu ya mikoa isipokuwa kwa Morogoro ambapo timu ya Techfort FC iliruhusiwa kutumia Uwanja wa CCM Mkamba mjini Ifakara.

Hivyo timu nane zilizofuzu kucheza raundi hiyo ni Friends Rangers ya Dar es Salaam, Kariakoo ya Lindi, Katavi Warriors ya Katavi, Kimondo SC ya Mbeya, Machava ya Kilimanjaro, Njombe Mji ya Njombe, Polisi Jamii ya Mara na Stand United FC ya Shinyanga.

Wakati timu nyingine zimefuzu kwa kushinda mechi zao za raundi ya mbili, Njombe Mji imeingia hatua hiyo kwa kuwa timu yenye uwiano mdogo wa kufungwa (best looser) katika hatua ya pili.

Katika hatua hiyo mechi ni ifuatavyo; Kariakoo vs Friends Rangers, Machava FC vs Stand United FC, Polisi Jamii vs Katavi Warriors, na Kimondo SC vs Njombe Mji. Timu zilizoanza kutajwa ndizo zinazoanzia nyumbani.

Vilevile Kamati ya Mashindano imeagiza Kamishna wa mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars vs Machava FC, Mwijage Rugakingira wa Tanga ambaye alikwenda Uwanja wa Mgambo badala ya Uwanja wa Jamhuri kinyume na maelekezo ya TFF aondolewe kwenye orodha ya makamishna.

Pia waamuzi wa mechi hiyo ambao nao walikwenda Mpwapwa badala ya Dodoma Mjini wamepelekwa Kamati ya Waamuzi ya TFF kwa ajili ya kuchukuliwa hatua kutokana na tukio hilo.

Kamati ya Mashindano imekumbusha kuwa RCL ni mashindano yanayosimamiwa na TFF, hivyo maelekezo yoyote kuhusiana na mashindano hayo pia yatatoka TFF na si mahali pengine popote. Hivyo, msimamizi wa kituoa hana mamlaka ya kubadili uwanja.

Hatua ya nne ya RCL itachezwa kati ya Juni 23 na 23 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 29 na 30 mwaka huu.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MOYES AWEKA NIA YA DHATI KWA FABREGAS VS LEWANDOWSKI.

Mabingwa wa ligi kuu BPL nchini uingereza Msimu 2012-2013 hivi karibuni Club ya Manchester United imeongeza hali  na kasi ya kujiamini kuwa wanaweza kuwatwaa wachezaji Cesc Fabregas na Robert Lewandowski  kutua Old Trafford majira haya ya joto.
Kocha mpya wa United, David Moyes ametanabaisha kuwa angependa kuwasajili wote.
 kiungo wa Barcelona na mshambuliaji wa Kipoland wa Borussia Dortmund katika klabu yake kabla ya kikosi chake hakijakwenda katika ziara ya Asia na Australia katikati ya mwezi ujao.
Inafahamika kwamba, wachezaji wote hao wameonyesha nia zao za kuhamishia cheche zao kwa mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England, hivyo United wanaweza kufanikisha dili hizo.
Double strike: Man United believe they can land Cesc Fabregas and Robert Lewandowski (below)

Man United wanaamini wanaweza kumnasa Cesc Fabregas na Robert Lewandowski (chini)
Robert Lewandowski
Robert Lewandowski

Klabu yake ya zamani Fabregas, Arsenal haijaonyesha nia na malengo ya  kumsajili tena iwapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ataondoka Nou Camp, lakini United inafahamika wanamtaka kwa dhati kiungo huyo aliyeichezea kwa miaka nane timu hiyo ya London kabla ya kurejea Hispania miaka miwili iliyopita.
 
Lewandowski anaweza kuhamia England baada ya matumaini yake kuhamia kwa mabingwa wapya wa Ulaya, Bayern Munich kukatwa wiki hii.
United wamekuwa wakimfuatilia mshambuliaji huyo wa Poland kwa miezi kadhaa na wanaamini anaweza kuzalisha ushindani mzuri kwa Robin van Persie, ambaye atatimiza miaka 30 muda mfupi kabla timu haijaanza kutetea ubingw awake Agosti.

Changamoto: Robin van Persie anaweza kukabiliana na changamoto kubwa mwanzoni mwa msimu ujao Man United
Kuwasili kwake pia kunaweza kukuza shinikizo kwa Wayne Rooney ambaye ameomba kuondoka Old Trafford tangu mwishoni mwa msimu uliopita.

MOURINHO KWA MARA NYINGINE ATAMBULISHWA RASMI DARAJANI.

Kocha jose mourinho rasmi  ametambulishwa darajani ambapo amesisitiza  na kuweka wazi kuwa hajawahi kuwa na bifu na mmiliki wa club hiyo Roman Abramovich na lengo lake kuu ni kumrejesha John Terry uwanjani huku akiwataka wachezaji kucheza kwa uzalendo mkubwa.
mourinho2 7c61aMreno Jose Mourinho jana ametambulishwa rasmi kuwa kocha mpya wa wazee wa darajani, klabu ya Chelsea. 
Akizungumza na waandishi wa habari, Mourinho ambaye miaka ya nyuma akiwa na Chelsea alikuwa anajiita “The Speacial one” kwa tafsiri isiyo rasmi,  akimaanisha mtu maalumu, leo hii ametoa kali ya mwaka baada ya kubadili jina hilo na kujiita “The Happy One kwa tafsiri isiyo rasmi unaweza kusema “Mtu mwenye furaha pekee”.
Mreno huyo ambaye ametokea klabu ya Real Madridi ya Hispania leo mchana ametambulishwa jijini London na kujibu maswali mengi kutoka kwa wanahabari waliohitaji kujua mambo mengi kutoka kwake likiwemo suala la uhusiano na bosi wake Abramovich.
Mourinho ambaye miaka ya nyuma alitimuliwa na mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich baada ya kushindwa kuelewana, leo hii amesema kipindi cha nyuma alikuwa na mahusiano mazuri na bosi wake, endapo wangekuwa na mahusiano mabaya asingerejea kwa mara ya pili darajani.
Akiongea na wanahabari wapatao 250 leo katika uwanja wa Stamford Bridge, aliulizwa kama ataendelea kujiita “The Special one”, kocha huyo mwenye umri wa miaka 50 kwa sasa alisema “I am the Happy One” na kumalizia maneno yake kwa kusema “nina furaha sana”.
mourinho3 f5edf
Mourinho alisema ” Mambo mengi sana yametokea katika maisha yangu ya kufundisha soka na kazi yangu miaka tisa iliyopita, lakini ni mtu yule yule, nina moyo uleule, nina hisia zile zile za kupenda mpira na kazi yangu, lakini kwa sasa ni mtu mwingine kabisa baada ya kurudi nyumbani Chelsea, nina furaha sana”.

Mourinho amewataka wachezaji wake kujituma zaidi na kuongeza kuwa klabu ni muhimu kuliko wao, kwani isingekuwepo wao pia wasingekuwepo. Chanzo: Baraka Mpenja

SNEIJDER ASIKITISHWA KUNYANG'ANYWA UNAHODHA:

KIUNGO nyota wa klabu ya Galatasaray  na timu ya taifa ya Uholanzi Wesley Sneijder amekiri kusikitishwa na kitendo cha kunyang’anywa kitambaa cha unahodha wa timu yake ya taifa. Kiungo huyo alipewa unahodha wa Uholanzi wakati Louis van Gaal alipochukua nafasi ya Bert van Marwijk baada ya michuano ya Ulaya 2012. Akihojiwa Sneijder amesema ni jambo lililomuumiza sana na sio sababu hakutambua hilo ila kwasababu amekua akijitoa kwa uwezo wake wote toka akabidhiwe majukumu hayo lakini inabidi akubaliane na uamuzi wa kocha. Baada ya kumvua unahodha kiungo huyo kutokana na kutofurahishwa na kiwango chake, Van Gaal alimkabidhi majukumu hayo mshambuliaji nyota wa Manchester United Robin van Persie ambaye ameisadia klabu yake kushinda taji la Ligi Kuu msimu uliopita.

ZINEDINE ZIDANE AWEKA WAZI KUWA WATAKA KUVUNJA REKODI YA USAJILI.

Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya REAL MADRID ambaye alikuwa kiungo wa wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Real Madrid, Zinedine Zidane amekiri kuwa lengo kuu ni kuvunja rekodi ya uhamisho kama watkuwa na nia ya kumsajili Gareth Bale. 
Bale ambaye ni winga wa klabu ya Tottenham Hotspurs ya Uingereza amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Madrid ambapo kuna taarifa kuwa klabu hiyo imetenga kitita cha paundi milioni 85 kwa ajili yake.
Kama uhamisho huo ukifanyika utakuwa umevunja rekodi aliyoweka Cristiano Ronaldo wakati aliposajiliwa kutoka Manchester United kwa ada ya paundi milioni 80 miaka minne iliyopita. 
Zidane amesema kwa kiwango cha mchezaji huyo alichokionyesha msimu uliopita sio ajabu vilabu vingi kumuwania ndio maana anadhani itakuwa gharama kubwa kupata saini yake. 
Nyota huyo wa zamani aliendelea kusema kuwa kama klabu yoyote yenye uwezo wa kifedha itahitaji saini ya mchezaji huyo lazima watoe dau kubwa na hata kufikia kuvunja rekodi ili Tottenham waweze kumuachia.