Thursday, June 13, 2013

TAFAKARI YA LEO BARCA ILIVYOFANYA JEURI KUMTAFUTIA MESSI COMBINATION JE KWA NEYMA ITAKUWAJEEEE??

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Barcelona imetumia jumla ya Euro 205 milioni kwa ajili ya kusaka mshambuliaji ambaye anaweza kumpunguzia Messi mzigo wa ustaa alioubeba kwa muda mrefu klabuni hapo.
Hivyo kuwasili kwa mshambuliaji wa Santos na timu ya taifa ya Hispania, Neymar, katika kikosi cha Barcelona, inamaanisha kuwa Barcelona imeendelea kutumia fedha nyingi kusaka mshambuliaji ambaye anaweza kung’ara vyema kwa pamoja na staa wao, Lionel Messi.

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Barcelona imetumia jumla ya Euro 205 milioni kwa ajili ya kusaka mshambuliaji ambaye anaweza kumpunguzia Messi mzigo wa ustaa alioubeba kwa muda mrefu klabuni hapo.
Thierry Henry
Katika msimu wake wa kwanza tu ndipo Henry alifikia matarajio ya mashabiki wa Barcelona. Baadaye kuibuka kwa kinda wa Kihispaniola, Pedro Rodriguez, kulimfanya Henry apate nafasi finyu ya kucheza katika kikosi cha kwanza na mwisho aliamua kutimkia Marekani katika klabu ya New York Bulls.
Hata hivyo Henry hakufikia kiwango alichokuwanacho wakati anachezea Arsenal chini ya Arsene Wenger ingawa katika kipindi chake na Barcelona alishinda mataji kadhaa.
Zlatan Ibrahimovich
Ukitazama hapa katika hali ya kawaida kilikuwa kipindi kibaya katika harakati za maisha ya soka ya Ibrahimovich. Tofauti na matarajio ya wengi, licha ya kusajiliwa kwa Euro 46 milioni huku pia Barcelona wakimtoa  Samuel Eto’o kwenda Inter Milan, bado Ibrahimovich hakutamba sana Nou Camp.
Mwishowe alijikuta akiingia katika mgogoro mkubwa na kocha wa wakati huo, Pep Guardiola. Ibrahimovich alimshutumu Guardiola kwamba alikuwa anampendelea zaidi Messi huku wakati mwingine akimchezesha nafasi ya kati wakati yeye yuko benchi.
Baada ya msimu mmoja tu, Zlatan aliondoka akarudi Italia ambako alijiunga na AC Milan.
David Villa
Alionekana mmoja kati ya wachezaji ambao wangeweza kumpunguzia mzigo wa mabao staa huyu wa Argentina. Alianza vema, lakini baadaye aliumia katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia, ilikuwa Desemba 2011.
Mbali na hilo tangu hapo kasi yake imepungua uwanjani na sasa inasemekana ataondoka zake Barcelona katika kipindi hiki cha uhamisho wa wachezaji.

LIONEL MESSI NA MZAZI WAKE WA KIUME WAINGIA MATATANI.

Mshambuliaji nyota  wa Barcelona  na timu ya Taifa ya Argentina Lionel Messi na babake wanatuhumun kwa tuhuma za kukwepa kulipa kodi nchini Hispania huivyo serikali ya nchi hiyo ipo katika zaidi ambapo inasadikika kuwa na deni la paundi milioni tatu nukta nne.

Mchezaji huyo kutoka Argentina na babake, Jorge wanatuhumiwa kuibia serikali ya nchi hiyo, kwa kujaza fomu zisizokuwa za ukweli za marejesho ya kodi kati ya mwaka wa 2007 na 2009.Hata hivyo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hajasema lolote kuhusiana na madai hayo.
Messi hulipwa Euro milioni kumi na sita kila mwaka na ndiye mchezaji anayelipwa kiasi cha juu zaidi duniani.Lakini mwendesha mashtaka Raquel Amado, aliwasilisha nyaraka za mahakama nyumbani kwa mchezaji huyo katika mtaa wa kifahari wa Gava mjini Barcelona.
Jaji mjini humo ni sharti waidhinisha malalamishi dhidi ya mshukiwa yeyote kabla hajafunguliwa mashtaka.Messi na babake wanashukiwa kutumia kampuni katika mataifa ya ng’ambo, mjini Belize na Uruguay kuuza haki za kutumia picha ya mchezaji huyo.
Mchezaji huyo na babake wanatuhumiwa kutumia kampuni hizo zilizoko nje ya Hispania, ambako anaishi na kucheza soka ya kulipwa, kukwepa kulipa kodi inayokisiwa kuwa paundi milioni tatu na nusu.

MASCHERANO AOMBA RADHI KUMPIGA TEKE DAKTARI WA TIMU:

KIUNGO nyota wa Club ya Barcelona na timu ya  taifa ya Argentina Javier Mascherano ameomba radhi baada ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kosa la kumpiga teke daktari wakati wa mechi ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia kati ya timu ya taifa ya nchi yake na Ecuador.
Kiungo huyo ambaye kucheza katika vilabu vya Liverpool na West Ham United alitolewa baada ya kumpiga teke dereva wa gari maalumu la kubebea wachezaji walioumia dakika ya 87 ya mchezo huo. 
Nyota huyo ambayo alikuwa nahodha katika mchezo huo aliomba radhi kwa tukio hilo na kudai kuwa alimuonya dereva kwa kwenda kasi mpaka kutaka kumdondosha ingawa amedai alichokifanya hakikubaliki.
Katika mchezo huo Argentina ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi Ecuador na kuendelea kubakia kileleni wakiwa na alama 27 wakifuatiwa na Colombia waliopo nafasi ya pili wakiwa na alama 26 huku Ecuador wakibakia nafasi ya tatu wakiwa na alama 22.

ESSIEN ASEMA NIPOM TAYARI KUCHEZA NAFASI YOYOTE UWANJANI:

KIUNGO nyota wa Chelsea na timu ya Taifa ya Ghana Michael Essien amesema kuwa amejiandaa kucheza nafasi yoyote chini ya kocha mpya wa klabu hiyo Jose Mourinho. Kiungo huyo wa kimataifa wa Ghana alikuwa akipewa nafasi kidogo ya kucheza chini Roberto Di Matteo baada kusumbuliwa na majeraha ya mguu lakini alipata ahueni wakati Mourinho alipomwita kwa mkopo wakati akifundisha Real Madrid. Mourinho amekuwa akimchezesha Essien kama beki au kiungo wakati akiwa Santiago Bernabeu na sasa yuko tayari kucheza nafasi yoyote ambayo Mreno huyo atamchezesha. Essien mwenye umri wamiaka 30 alisajiliwa na Mourinho wakati akiwa Chelsea mwaka 2005 kwa ada ya paundi milioni 29 akitokea klabu ya Lyon ya Ufaransa.

Wednesday, June 12, 2013

MWAIKIMBA KATIKA HARAKATI ZA MAISHA YA SOKA:

JINA KAMILI: Gaudence Mwaikimba
KUZALIWA: Oktoba 5, 1984

ALIPOZALIWA: Kyela, Mbeya 
KLABU YAKE: Azam FC

NAFASI UWANJANI; Mshambuliaji

UREFU; 189 cm

UZITO; 85 kg

KLABU ZA AWALI:

MWAKA              CLUB 

2003-2004:        Tukuyu Stars

2004- 2005:       Kahama United

2005- 2006:       Ashanti United

2006- 2009:       Yanga SC 
2009-2010:        Sur (Oman)

2010:                 Prisons FC

2011- 2012:        Kagera Sugar

2012:                  Moro United

2012 hadi sasa     Azam FC 

WASIFU 
Baadhi ya Picha Zikimuonyesha Gaudence Mwaikimba akiwa n

DAVID VILLA KATIKA ULIMWENGU WA SOKA JE WAMJUA?

David Villa
David Villa2 (cropped).jpg
Villa in 2008
Personal information
Full nameDavid Villa Sánchez[]
Date of birth3 December 1981 (age 31)]
Place of birthLangreo, Spain
Height1.75 m (5 ft 9 in)[2]
Playing positionStriker
Club information
Current clubBarcelona
Number7
Youth career
1991–1999Langreo
Senior career*
YearsTeamApps(Gls)
1999–2001Sporting Gijón B65(25)
2001–2003Sporting Gijón80(38)
2003–2005Zaragoza73(32)
2005–2010Valencia166(108)
2010–Barcelona77(33)
National team
2000–2003Spain U217(0)
2005–Spain88(53)
2002Asturias1(0)

CLUB MATAJI

Real Zaragoza
Valencia
Barcelona


SIMBA NA YANGA YAZIWEKEA NGUMU KUSHIRIKI MICHUANO YA KAGAME-SERIKALI


SERIKALI imesisitiza kuwa timu za Simba na Yanga hazitashiriki katika michuano ya klabu Bingwa Afrika Mashariki na kati maarufu kama kombe la Kagame. Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Amos Makala ametoa taarifa hiyo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Sumve Mheshimiwa Richard Ndasa. Katika swali lake mheshimiwa Ndasa ametaka kujua msimamo wa Serikali juu ya timu za Simba na Yanga kushiriki michuano ya Kagame inayotarajia kuanza Juni 18 hadi Julai 2, mwaka huu huko Sudan Kusini. Akijibu swali hilo mheshimiwa MAKALA amesema kumekuwa na taarifa za hali ya usalama katika Nchi ya Sudan kuwa sio nzuri. Amesema kumekuwa na taarifa kulingana na hali ya usalama nchini Sudan na kwamba Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mheshimiwa Benard Membe tayari amelitolea taarifa na ndani ya Serikali kuna taarifa za kutosha kuwa Sudan hakuna usalama. Amesema msimamo wa Serikali ni kuwa hawawezi kupeleka timu mahali ambapo hakuna usalama.