Mabingwa wa BPL msimu uliopita Club ya soka ya Manchester
United imeamua kumtengea kitita cha paundi milioni 15 kwa ajili ya
kumnasa beki wa Everton, Leighton Baines. Baada
ya kukataa ofa ya awali ya United ya Pauni Milioni 12, Everton
imesisitiza kuwa beki huyo wa kushoto wa kimataifa wa England hauzwi. Lakini United imepania kupanda dau hadi paundi milioni 20 katika kuwania saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. Mrithi
wa Moyes, Everton, Roberto Martinez anataka kumbakzia beki huyo na
klabu hiyo inataka kumpa mkataba mpya ikimuongezea mshahara hadi paundi
70,000 kwa wiki. Mpango
huu unamuweka shakani beki Mfaransa, Patrice Evra juu ya mustakabali
wake Old Trafford na wazi sasa anaweza kuhamia Monaco au Paris
Saint-Germain.
Friday, June 28, 2013
WAMSHANGAA MESSI BAADA YA KUTUA NCHIN SENEGAL-WAKANYAGANA
MSHAMBULIAJI nyota wa
kimataifa wa Argentina Lionel Messi ametua nchini Senegal jana kwa ndege
binafsi na kulakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Dakar na mashabiki wa
soka na vijana wadogo waliotoka pembe mbalimbali za nchi hiyo. Nyota
huyo anayecheza katika klabu ya Barcelona alialikwa na shule ya soka ya
Qatar Aspire ambao wana tawi lao nchini humo kwa ajili ya kwenda kwenye
kampeni ya kupiga vita ugonjwa wa malaria. Kwa
mujibu wa waratibu ya ziara hiyo maelfu ya neti ambazo zitakuwa na
picha ya Messi zitasambazwa kwa watoto na familia katika vijiji
mbalimbali nchini humo. Messi
atasafiri kwa helikopta kwenda Saly eneo la karibu na mji wa Dakar
ambapo atatembelea nyumba za yatima na kuongea na wenyeji wa hapo jinsi
watakavyoweza kujikinga na malaria.
HISPAIN YATINGA FAINALI SASA KUUMANA NA WENYEJI BRAZIL

Wataliano walifungwa na Waspanyola
katika Fainali ya Euro mwaka jana wameshindwa kulipa kisasi na sasa
Fainali ya michuano hiyo mwaka huu Jumapili Uwanja wa Maracana,
itawakutanisha wenyeji La Roja na Brazil wenyeji.
Leonardo Bonucci wa Italia alikosa moja
ya penalti 14 na Jesus Navas akaweka nyavuni mkwaju wa mwisho na
kuipeleka Hispania Fainali.
TUTAFAKARI KUELEKEA FAINALI JE NANI KUIBUKA NA UBINGWA"
USO KWA USO
JUMLA: Mechi 8
USHINDI: Brazil 4 Spain 2
SARE: 2
MAGOLI JUMLA: Brazil 11 Spain 8
Mechi zenyewe:
FIFA KOMBE LA DUNIA:
Jumla: Mechi 5
USHINDI: Brazil 3 Spain 1
SARE: 1
MAGOLI JUMLA: Brazil 10 Spain 5
1986 Spain 0 Brazil 1 {Guadalajara, Mexico}
1978 Brazil 0 Spain 0 {Mar Del Plata, Argentina}
1962 Brazil 2 Spain 1 {Vina Del Mar, Chile}
1950 Brazil 6 Spain 1 {Rio De Janeiro, Brazil}
1934 Spain 3 Brazil 1 {Genoa, Italy}
KIRAFIKI:
Jumla: Mechi 3
USHINDI: Brazil 1 Spain 1
SARE: 1
MAGOLI: Spain 3 Brazil 1
1999 Spain 0 Brazil 0 {Vigo, Spain}
1990 Spain 3 Brazil 0 {Gijon, Spain}
1981 Brazil 1 Spain 0 {Salvador, Brazil}
WAWILI WACHAGULIWA KITUO CHA VIPAJI ASPIRE
Wachezaji
wawili kutoka Tanzania wamechaguliwa miongoni mwa 50 waliofanyiwa
majaribio nchini Uganda kwa ajili ya kuingia katika kituo cha kuendeleza
vipaji (centre of excellence) kilichoko Doha nchini Qatar kupitia
mpango wa kukuza vipaji wa Aspire Football Dream.
Abdulrasul
Tahir Bitebo (15) ambaye ni mshambuliaji kutoka Kituo cha Uwanja wa
Karume, na Martin Omela Tangazi (14) ambaye ni beki kutoka Kituo cha
Ukonga ndiyo waliochaguliwa kutoka Tanzania kuingia katika kituo ambapo
watakaa kwa mwezi mmoja kabla ya kusaini mkataba rasmi wa kuendelezwa.
Wachezaji
wengine walikuwa wakitoka katika nchi za Uganda na Kenya. Mchezaji
mwingine aliyefuzu katika nafasi tatu zilizokuwepo ni kutoka nchini
Kenya.
Mpango
wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar
katika nchi 16 duniani, na kwa hapa nchini uko chini ya Idara ya Ufundi
ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
TFF
ina jumla ya vituo 14 vya kuendeleza vipaji kupitia mpango huo wa
Aspire Football Dream. Vituo hivyo ni Karume, Kigamboni, Tandika, Kawe,
Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni, Makongo, na Tabata vilivyo katika
Mkoa wa Dar es Salaam. Vingine ni Bagamoyo kilichopo mkoani Pwani,
Morogoro, Arusha na Moshi mkoani Kilimanjaro.
Kituo kingine cha kuendeleza vipaji (centre of excellence) cha Aspire kipo Dakar nchini Senegal.
TFF KUENDESHA KOZI SITA KATI YA JULAI- SEPTEMBA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaendesha kozi sita tofauti za mpira wa miguu kati ya Julai na Septemba mwaka huu.

Waamuzi
wa FIFA nao watakuwa na kozi itakayofanyika kati ya Agosti 22 hadi 26
mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati kozi ya ukocha kwa ajili ya Copa
Coca-Cola itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Agosti 12 na 17 mwaka
huu.
Vilevile kutakuwa na kozi ya mpango
wa grassroots unaolenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na
wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12 itafanyika kuanzia Septemba 9
hadi 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati tamasha (festival) la
grassroots litafanyika Uwanja wa Karume, Septemba 14 mwaka huu.
RCL KUKAMILISHA HATUA YA NNE JUMAPILI
Mechi
za marudiano za hatua ya nne ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL)
zitachezwa Jumapili (Juni 30 mwaka huu) kwenye viwanja vya Sokoine
jijini Mbeya, na Kambarage mjini Shinyanga.
Friends
Rangers ya Dar es Salaam ambayo katika mechi ya kwanza ilifungwa
nyumbani mabao 3-0 itakuwa mgeni wa Stand United FC mjini Shinyanga
wakati Kimondo SC itaikaribisha Polisi Jamii ya Mara jijini Mbeya.
Katika mechi ya kwanza timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
Hatua
ya mwisho ya RCL itachezwa Julai 3 mwaka huu kwa mechi za kwanza wakati
zile za marudiano zitafanyika Julai 7 mwaka huu. Timu tatu za kwanza
zitapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
TENGA ASEMA MKUTANO UPO PALEPALE"-MKUU WA TFF

Wadau wengi wamekuwa wakihoji kufanyika kwa Mkutano huo wakati Nchi inakabiliwa na Mechi muhimu Siku hiyo hiyo huku wengine wakidiriki kudai kuna walakini ndani yake.
Lakini Rais wa TFF, Leodegar Tenga, amefafanua kuwa vitu hivyo viwili haviwezi kuleta mgongano kwani Mechi itachezwa kwa Dakika 90 na Mkutano Mkuu umepangwa kuwa wa Siku mbili.
Tenga alisema: “Hamna njama zozote. Vitu hivyo viwili vitaendelea kama ilivyopangwa.”
Akifafanua, Tenga alisema Wajumbe wa Mkutano Mkuu wamezoea kujadili Ajenda hadi 12 katika Siku moja lakini safari hii Ajenda ni moja tu na imepangiwa Siku mbili.
Ajenda ya Mkutano Mkuu huo ni kujadili na kupitisha Mabadiliko ya Katiba ili kuruhusu Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho hilo ufanyike kama ilivyoagizwa na FIFA.
Awali Uchaguzi ulikuwa ufanyike hapo Februari 24 lakini ukatokea mgongano mkubwa baada ya baadhi ya Wagombea kufutwa na pia madai kuwa Katiba ilibadilishwa bila kufuata taratibu.
Akifafanua zaidi, Tenga alisema upo uwezekano mkubwa kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu kumaliza Kikao chao kabla hata Mechi kuchezwa.
Thursday, June 27, 2013
FEDERER ASEMA BADO ATAENDELEA KUCHEZA MCHEZO HUO".
Mchezaji tenesi mahiri wa
Switzerland, Roger Federer amesisitiza kuwa bado ataendelea kucheza
mchezo huo kwa miaka mingi ijayo pamoja na kutolewa mapema katika
michuano ya Wimbledon jana. Nyota
huyo ambaye anashika namba tatu katika orodha za ubora duniani amesema
hana hofu yoyote pamoja na kutolewa na Sergiy Stakhovisky wa Ukraine
katika mzunguko wa pili wa michuano hiyo. Katika
mchezo huo Federer aliburuzwa kwa kufungwa 6-7 7-6 7-5 7-6 na
Stakhovsky anayeshika namba 116 katika orodha za ubora duniani. Baadhi
ya wadau wa mchezo huo wamekuwa wakihoji kiwango cha Federer mwenye
umri wa miaka 31 na kudai kuwa amekwisha lakini mwenye amesisitiza kuwa
bado yuko fiti na ataendelea kucheza kwa miaka kadhaa ijayo. Kwa
upande wa wanawake mwanadada nyota anayeshika namba mbili kwa ubora kwa
upande wanawake Maria Sharapova wa Urusi naye aliyaaga mashindano hayo
baada ya kukubali kipigo cha 6-3 6-4 kutoka kwa Michelle Larcher de
Brito wa Ureno anayeshika namba 131 katika orodha hizo.
SCOLARI AMEKIRI KUWA TIMUYA BRAZIL BADO HAIKO FITI-DUNIA
KOCHA wa timu ya taifa ya
Brazil, Luis Felipe Scolari amekiri kuwa kikosi chake bado hakiwezi
kuanza kuweka matumaini ya kutwaa kombe lao la sita la Kombe la Dunia mwaka ujao
lakini wamebakisha mechi moja kunyakuwa taji lao la tatu la Kombe la
Shirikisho baada ya kuiengua Uruguay katika hatua ya nusu fainali. Scolari
amesema anafikiri kikosi hicho kimefikia mahali pazuri lakini bado kuna
vitu vingi vya kufanyia marekebisho mpaka kikamilike kwa ajili ya
michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Kocha
huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa wanahamishia nguvu zao katika mchezo
wa fainali na baada ya hapo wataangalia mapungufu yalijitokeza ili
kuhakikisha wanakuwa na kikosi imara kitakachoweza kulibakisha Kombe la
Dunia nyumbani. Brazil
kwasasa wanasubiri mshindi wa nusu fainali nyingine ya michuano hiyo
itakayopigwa baadae leo kati ya mabingwa wa Ulaya na Dunia Hispania
watakaochuana na Italia.
Subscribe to:
Posts (Atom)