Tuesday, July 2, 2013

WEBB ASEMA WAAMUZI WANAIMANI KUBWA NA MFUMO MPYA WA TEKNOLOGIA YA MSTARI WA GOLI

Howard Webb Mwamuzi wa Uingereza amedai kuwa waamuzi wana imani kubwa na mfumo mpya wa teknologia ya kompyuta katika mstari wa goli ambao utatumika katika michuano ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil. Hakuna bao lolote kati ya mabao 68 yaliyofungwa katika michuano ya Kombe la Shirikisho lililohitaji teknologia hiyo ambayo ndio ilikuwa imeanza kutumika kwa mara ya kwanza kwenye michuano hiyo. Lakini Webb aliwaambia waandishi wa habari jijini Rio de Janeiro kwamba uhakika wa mfumo huo unawapa faida kubwa na waamuzi wana imani kwa kiasi kikubwa na mfumo huo ambao umefungwa na kampuni ya Kijerumani iliyoshinda zabuni hiyo ya GoalControl. Webb amesema hawana shaka na uthabiti wa mfumo huo na umeonekana kufanya kazi vyema hivyo anadhani utaendelea kufanya kazi hata katika michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Webb ambaye alichezesha mchezo wa fainali kati ya Kombe la Dunia mwaka 2010 kati ya Hispania na Uholanzi nchini Afrika Kusini ni mmoja katika orodha ya waamuzi 52 ambao watachujwa kwa ajili ya michuano hiyo mwakani.

UNDER-20 KOMBE LA DUNIA: RAUNDI YA MTOANO KUANZA KUTIMUA VUMBI

Kazi ipo Kweli Kweli Katika Hatua ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Vijana chini ya Miaka 20, U-20, yanayochezwa huko Nchini Turkey itaanza kutimua vumbi leo Jumanne julai 2 kwa Mechi 4 na Jumatano Mechi za mwisho 4.
FIFA_WORLD_CUP_U-20_TURKEY_LOGORATIBA:
RAUNDI YA MTOANO TIMU 16
Jumanne Julai 2
[Istanbul]
Spain v Mexico [Saa 12 Jioni]
Nigeria v Uruguay [Saa 3 Usiku]
[Gaziantep]
Greece v Uzbekistan [Saa 12 Jioni]
France v Turkey [Saa 3 Usiku]
Jumatano Julai 3
[Saa 12 Jioni]
Portugal v Ghana [Kayseri]
Croatia v Chile [Bursa]
[Saa 3 Usiku]
Colombia v Colombia [Trabzon]
Iraq v Paraguay [Antalya]
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Washindi wa Raundi hii watatinga Robo Fainali na Afrika imebakiza Timu mbili, Nigeria na Ghana, baada Mali na Egypt kutolewa hatua za Makundi.
RATIBA:
RAUNDI YA MTOANO TIMU 16
37      02/07 18:00 Istanbul Spain v Mexico
38      02/07 18:00 Gaziantep Greece v Uzbekistan
39      02/07 21:00 Istanbul Nigeria v Uruguay
40      02/07 21:00 Gaziantep France v Turkey
41      03/07 18:00 Kayseri Portugal v Ghana
42      03/07 18:00 Bursa Croatia v Chile
43      03/07 21:00 Trabzon Colombia v Colombia
44      03/07 21:00 Antalya Iraq v Paraguay
ROBO FAINALI
45      06/07 18:00 Rize W40 v W38
46      06/07 21:00 Bursa W39 v  W37
47      07/07 18:00 Kayseri W44 v W43
48      07/07 21:00 Istanbul W41 v W42
NUSU FAINALI
49      10/07 18:00 Bursa W45 v  W48
50      10/07 21:00 Trabzon W47 v W46
MSHINDI WA TATU
51      13/07 18:00 Istanbul L49 v L50
FAINALI
52      13/07 21:00 Istanbul W49 v W50

MWAMBUSI ASEMA TUPO TAYARI KWA LIGI KUU TZ BARA MSIMU UJAO.

Baada ya kumalizika kwa msimu wa ligi kuu tanzania bara kila timu imejipanga sawasawa katika harakati za usajili pamoja na maandalizi Kabambe ya msimu mpya wa ligi kuu  unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu.
Ambapo timu mpya katika ligi kuu na kipenzi kwa wakazi wa jiji la  mbeya Mbeya City ya jijini Mbeya wameanza kujiweka chimbo kujifua chini ya kocha wao mkuu Juma Mwambusi.
Akizungumza na mkali wa dimba Kocha Mwambusi amesema wachezaji kutoka mikoani wameanza kuwasili kuanzia jana, huku akitanabaisha kuwa anajipanga kuongeza wachezaji wachache katika kikosi chake alichotoka nacho  ligi daraja la kwanza msimu uliopita.
“Wachezaji wengi ni walewale, nina mpango wa kuongeza nyota wachache, wengi nitawapandisha kutoka kikosi B, lakini wachezaji wengi waliopandisha timu ligi kuu nimewaacha ila kuna nafasi chache nitaziba hivi karibuni”. Alisema Mwambusi.
Mwambusi amesema katika kikosi chake hana tabia ya kuwapa majina wachezaji kwa kuwapa uhakika wa namba, kwani falsafa yake ni kuchezesha wachezaji wote bila kujali majina yao.
“Mimi siku zote falasafa yangu ni ileile, wachezaji wote wanaofanya vizuri wameweza kupata nafasi hiyo kwa sababu walipewa nafasi ya kucheza, hivyo nitawapa wachezaji wote nafasi ya kucheza ili waongeze uzoefu”. Alisisitiza Mwambusi.
Kuhusu kusajili wachezaji wenye uzoefu mkubwa na mikikimikiki ya ligi kuu, Mwambusi alisema hana mpango wa kusajili wakongwe kutokana na kikosi chake kuwa na vijana wengi ambao wanafanya vizuri.
“Mbeya City ina kikosi bora cha vijana, ninavyozungumza hapa kipo mkoani Iringa wilaya ya Mufindi kushiriki michuano ya kombe la Muungano Mufindi, ni kikosi kizuri sana, kinaongozwa na kocha wangu msaidizi Maka Mwalwisyi ambaye anafanya kazi nzuri. Ni matumaini yangu hawa vijana ni msingi mkubwa wa klabu yangu na watapewa nafasi”.
Mwambusi alisema kikosi chake kinahitaji kujifua kwa nguvu kuhimili mitanannge ya ligi kuu, kwani ligi ya Tanzania bara imekuwa na ushindani mkubwa sana.
“Ligi imebadilika sana, niliifundisha Prisons miaka ya nyuma, sasa naona mambo yamebadilika sana, lakini nina uhakika kwa uzoefu wangu nitajipanga vizuri na kupambana hadi mwisho”. Alisema Mwambusi.
Mbeya City ni miongoni mwa timu tatu zilizopanda ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao, wakati nyingine ni Maafande wa Rhino Rangers ya Tabora, na Ashanti United ya Dar es salaam.
Msimu uliopita timu tatu za Africa Lyon ya Dar es salaam, Toto Africans ya Mwanza na Polisi Morogoro zilishuka daraja na sasa zinaendelea na mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi daraja la kwanza.

SERENA WILLIAMS ATOLEWA NJE KATIKA TENESI MICHUANO YA WIMBLEDON

MWANADADA nyota dunia katika tenisi kutoka Marekani, Serena Williams ametolewa nje katika michuano ya Wimbledon baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Sabine Lisicki wa Ujerumani kwa 6-2 1-6 6-4. Williams ambaye mbali na kupewa nafasi kubwa ya kunyakuwa taji hilo pia alikuwa bingwa mtetezi wa michuano hiyo aliyonyakuwa mwaka jana. Kwa upande mwingine bingwa wa zamani wa michuano hiyo Petra Kvitova alifanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo baada ya kumgaragaza Carla Suarez wa Hispania kwa 7-5 6-3. Mashindano ya Wimbledon mwaka huu yamekuwa sio mazuri kwa nyota wengi wanaoshika nafasi za juu katika orodha za ubora wa mchezo huo duniani baada ya Maria Sharapova anayeshika namba mbili kuenguliwa katika mzunguko wa pili huku Victoria Azarenka anayeshika namba tatu yeye akijitoa baada ya kupata majeraha.

Saturday, June 29, 2013

ARSENAL WAMTAKA KIPA JULIO CESAR WA QPR ILIYOSHUKA DARAJA"

Wanted: Julio Cesar is set to join Arsenal following Queens Park Rangers' relegation to the Championship WASHIKA Bunduki wa jiji London Club ya Arsenal itaangalia uwezekano wa kukamilisha usajili wa kipa namba wa Brazil na klabu ya Queens Park Rangers, Julio Cesar baada ya Kombe la Mabara.
Arsene Wenger anataka kipa mzoefu atengeneze ushindani kwa Lukasz Fabianski na Wojciech Szczesny.
Mazungumzo baina ya wawakilishi wa Cesar na viongozi wa Gunners tayari yamefanyika, lakini hayajamalizika kwa kuwa kipa huyo yupo kwenye majukumu ya kimataifa.
Wanted: Julio Cesar is set to join Arsenal following Queens Park Rangers' relegation to the Championship
ARSENAL sasa inatarajiwa kumaliza dili hilo mara moja tu, baada ya kubainika Roma ya Italia nayo imeingia kwenye mbio za kuwania saini ya Cesar.
Kipa huyo wa kimataifa wa Brazil ambaye yupo huru kuondoka Loftus Road kufuatia kushuka kwa QPR hadi Championship, anataka kubaki London ambako amezoea maisha tangu awasili msimu uliopita akitokea Inter Milan.
Na The Gunners – ambayo inatumai kukamilisha pia usajili wa Gonzalo Higuain wiki ijayo, baada ya kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti kufungua njia kwa mshambuliaji huyo kuondoka  Hispania – inajiamini dili hilo litakamilishwa baada ya Fainali ya Kombe la Mabara Jumapili.
Wenger alitaka kusajili kipa wa Stoke, Asmir Begovic na wa Liverpool, Pepe Reina lakini, licha ya kuwa na fungu la bajeti ya usajili la Pauni Milioni 70, kocha huyo wa Arsenal ameona  hana sababu ya kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kipa.
Rangers itasikiliza ofa ya kiasi cha Pauni Milioni 2 kwa Cesar, wakati mshahara wake wa Pauni 70,000 kwa wiki halitakuwa tatizo kwa The Gunners, ambayo imetuma waangalia vipaji wake nchini Brazil kumuangalia Cesar anachokifanya katika Kombe la Mabara.
Pamoja na mpango wa kuwasajili Cesar na Higuain, The Gunners pia wanataka kumsajili beki wa Swansea, Ashley Williams na kiungo wa Everton, Marouane Fellaini. Lakini masuala ya kifedha yanatia saka kama Arsenal itaweza kusajili wachezaji wote hao.
Hadi sasa, Arsenal imegoma kumpa Fellaini mshahara wa Pauni 100,000 kwa wiki na pia imeshindwa kufika dau la Pauni Milioni 24 za kumnunua.
Missing out? Arsenal look set to be priced out of moves for Marouane Fellaini and Ashley Williams (below) Amekosekana? Arsenal inataka kuwasajili Marouane Fellaini

MBEYA MWENYEJI WA NETIBOLI TENA KWA MARA YA PILI MFULULIZO".

Jiji la Mbeya kwa mara ya pili mfululizo,litakuwa mwenyeji wa ligi kuu ya Netiboli taifa ambapo  naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo anatarijiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi kuanzia Agosti 24 hadi Septemba 7.
Mwenyekiti wa chama cha Netiboli Mkoa wa Mbeya, Mary Mung’ong’o ameumabia mtandao huu kuwa ligi hiyo inafanyika kwa mara nyingine kutokana na ombi la Waziri Mulugo kwa vile ligi hiyo haikuwa imefana, hivyo akaiomba CHANETA kuwapa Mbeya fursa nyingine ya uwenyeji.
Alisema maandalizi ya ligi yameanza na kusema zinahitajika sh milioni 16 kufanikisha na kuongeza kuwa hadi sasa, hawajajua timu ngapi zitashiriki kutokana na jukumu hilo kuwa chini ya Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA).
Hata hivyo, mwenyekiti huyo ametoa wito kwa viongozi wa ngazi mbalimbli wakiwemo wadau wenye mapenzi na mchezo kutoka mkoani hapa kujitoa kwa hali na mali kuyafanikisha ili yawe chachu ya kukua kwa mchezo huo nchini kwa maslahi ya vijana na taifa.
Aidha, mwenyekiti huyo alitamtambulisha Nwaka Mwakisu kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano hayo.
Akizungumzia mashindano hayo, Mwakisu alisema ni fursa kwa watu wa Mbeya kujitangaza kibiashara kupitia mchezo huo na kufuta makosa yaliyofanyika mwaka jana.
Alisema katika kufakisha mashindano hayo, nguvu ya pamoja inahitajika kuanzia viongozi wa kisiasa, serikari na vyombo vya habari.

MBASPO FC YATWAA UBINGWA WA AIRTEL RISING KWA MKOA WA MBEYA"

Kama kawaidaTimu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Mbaspo imefanikiwa kuwa mabingwa wa Airtel Rising Stars mkoa wa Mbeya baada ya kukusanya pointi nne sawa na mahasimu wao Mbosa fc lakini wakiwa na magoli mengi ya kufunga. Timu ya Mbeya Secondari haikupata hata pointi moja katika michuano hiyo ya kusaka vipaji

Mbaspo walianza mbio zao za kutwaa ubingwa kwa kutoshana nguvu ya 3-3 dhidi ya Mbosa siku ya Jumatatu Juni 24 kabla ya kufanya mauaji makubwa ya 6-0 dhidi ya timu dhaifu ya Mbeya Sekondari siku ya Jumanne. Michezo yote imefanyika kwenye uwanja wa Magereza jijini Mbeya.
Mbosa walifikisha point nne juzi Jumatano walipoitandika Mbeya Sekondari 3-0 hivyo kumaliza wakiwa na point nne na magoli sita wakati wapinzani wao Mbaspo wakifikisha jumla ya magoli tisa ya kufunga. Katika mechi ya juzi, magoli ya Mbosa yalitiwa kwenye kamba na Michael Mwashilanga, Riziki Juma na Julius Landa.
Wakati huo huo, chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mbeya kimetangaza kikosi cha wachezaji 18 kuuwakilisha mkoa huo kwenye michuano ya Taifa ya Airtel Rising Stars inayoanza kutimua vumbi kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 2.

Wachezaji hao ni Ismail Yesaya, Emmanuel Alex, Gift Sanga, Jackson Mwaibambe, Boaz Mwangole, Costa Sanga, Seif Zubery, Stanley Angelo, Enock Sikaonga, Kaunda Malata, Joel Kasimila, Hamprey Nyeo, Elia Salengo, Peter Noah, Emmaneul Mtimbi, Michael Bosco, Richard Kalinga na Zamoyoni Mwashambwa. 

Katika mkoa wa Morogoro, mji kasoro bahari, timu ya Moro Kids imetoka sare ya bila kufungana na Techfort katika mchezo wa kushambuliana kwa zamu uliopigwa kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Morogoro juzi Jumatano na kushuhudiwa na mashabiki wengi wa mji huo
Airtel Rising Stars vile vile imeanza kutimua vumbi katika jiji la Mwanza ambapo timu ya Marsh Athletical imedhihirisha umwambe wake katika soka baada ya kuifunga Nyamagana United 2-0 kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana.
Timu za mikoa zimepangwa kuanza kuwasili jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki tayari kwa ajili ya kindumbwe ndumbwe cha Airtel Rising Stars ngazi ya taifa katika uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. Wachezaji 16 watachaguliwa wakati wa mashindano hayo ili kuunda timu itakayoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars. Nchi mwenyeji wa michuano hiyo itatangazwa baadaye mwezi ujao.