Howard Webb Mwamuzi wa
Uingereza amedai kuwa waamuzi wana imani kubwa na mfumo mpya wa
teknologia ya kompyuta katika mstari wa goli ambao utatumika katika
michuano ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil. Hakuna
bao lolote kati ya mabao 68 yaliyofungwa katika michuano ya Kombe la
Shirikisho lililohitaji teknologia hiyo ambayo ndio ilikuwa imeanza
kutumika kwa mara ya kwanza kwenye michuano hiyo. Lakini
Webb aliwaambia waandishi wa habari jijini Rio de Janeiro kwamba
uhakika wa mfumo huo unawapa faida kubwa na waamuzi wana imani kwa kiasi
kikubwa na mfumo huo ambao umefungwa na kampuni ya Kijerumani
iliyoshinda zabuni hiyo ya GoalControl. Webb
amesema hawana shaka na uthabiti wa mfumo huo na umeonekana kufanya
kazi vyema hivyo anadhani utaendelea kufanya kazi hata katika michuano
ya Kombe la Dunia mwakani. Webb
ambaye alichezesha mchezo wa fainali kati ya Kombe la Dunia mwaka 2010
kati ya Hispania na Uholanzi nchini Afrika Kusini ni mmoja katika orodha
ya waamuzi 52 ambao watachujwa kwa ajili ya michuano hiyo mwakani.
Tuesday, July 2, 2013
UNDER-20 KOMBE LA DUNIA: RAUNDI YA MTOANO KUANZA KUTIMUA VUMBI
Kazi ipo Kweli Kweli Katika Hatua ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Mashindano
ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Vijana chini ya Miaka 20, U-20,
yanayochezwa huko Nchini Turkey itaanza kutimua vumbi leo Jumanne julai 2 kwa Mechi 4
na Jumatano Mechi za mwisho 4.
RAUNDI YA MTOANO TIMU 16
Jumanne Julai 2
[Istanbul]
Spain v Mexico [Saa 12 Jioni]
Nigeria v Uruguay [Saa 3 Usiku]
[Gaziantep]
Greece v Uzbekistan [Saa 12 Jioni]
France v Turkey [Saa 3 Usiku]
Jumatano Julai 3
[Saa 12 Jioni]
Portugal v Ghana [Kayseri]
Croatia v Chile [Bursa]
[Saa 3 Usiku]
Colombia v Colombia [Trabzon]
Iraq v Paraguay [Antalya]
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Washindi wa Raundi hii watatinga Robo
Fainali na Afrika imebakiza Timu mbili, Nigeria na Ghana, baada Mali na
Egypt kutolewa hatua za Makundi.
RATIBA:
RAUNDI YA MTOANO TIMU 16
37 02/07 18:00 Istanbul Spain v Mexico
38 02/07 18:00 Gaziantep Greece v Uzbekistan
39 02/07 21:00 Istanbul Nigeria v Uruguay
40 02/07 21:00 Gaziantep France v Turkey
41 03/07 18:00 Kayseri Portugal v Ghana
42 03/07 18:00 Bursa Croatia v Chile
43 03/07 21:00 Trabzon Colombia v Colombia
44 03/07 21:00 Antalya Iraq v Paraguay
ROBO FAINALI
45 06/07 18:00 Rize W40 v W38
46 06/07 21:00 Bursa W39 v W37
47 07/07 18:00 Kayseri W44 v W43
48 07/07 21:00 Istanbul W41 v W42
NUSU FAINALI
49 10/07 18:00 Bursa W45 v W48
50 10/07 21:00 Trabzon W47 v W46
MSHINDI WA TATU
51 13/07 18:00 Istanbul L49 v L50
FAINALI
52 13/07 21:00 Istanbul W49 v W50
MWAMBUSI ASEMA TUPO TAYARI KWA LIGI KUU TZ BARA MSIMU UJAO.
Baada ya kumalizika kwa msimu wa ligi kuu tanzania bara kila timu imejipanga sawasawa katika harakati za usajili pamoja na maandalizi Kabambe
ya msimu mpya wa ligi kuu unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 24
mwaka huu.
Ambapo timu mpya katika ligi kuu na kipenzi kwa wakazi wa jiji la mbeya Mbeya City ya jijini Mbeya
wameanza kujiweka chimbo kujifua chini ya kocha wao mkuu Juma Mwambusi.
Akizungumza na mkali wa dimba Kocha Mwambusi amesema wachezaji kutoka
mikoani wameanza kuwasili kuanzia jana, huku akitanabaisha kuwa anajipanga
kuongeza wachezaji wachache katika kikosi chake alichotoka nacho ligi
daraja la kwanza msimu uliopita.
“Wachezaji
wengi ni walewale, nina mpango wa kuongeza nyota wachache, wengi
nitawapandisha kutoka kikosi B, lakini wachezaji wengi waliopandisha
timu ligi kuu nimewaacha ila kuna nafasi chache nitaziba hivi karibuni”.
Alisema Mwambusi.
Mwambusi
amesema katika kikosi chake hana tabia ya kuwapa majina wachezaji kwa
kuwapa uhakika wa namba, kwani falsafa yake ni kuchezesha wachezaji wote
bila kujali majina yao.
Kuhusu
kusajili wachezaji wenye uzoefu mkubwa na mikikimikiki ya ligi kuu,
Mwambusi alisema hana mpango wa kusajili wakongwe kutokana na kikosi
chake kuwa na vijana wengi ambao wanafanya vizuri.
“Mbeya
City ina kikosi bora cha vijana, ninavyozungumza hapa kipo mkoani
Iringa wilaya ya Mufindi kushiriki michuano ya kombe la Muungano
Mufindi, ni kikosi kizuri sana, kinaongozwa na kocha wangu msaidizi Maka
Mwalwisyi ambaye anafanya kazi nzuri. Ni matumaini yangu hawa vijana ni
msingi mkubwa wa klabu yangu na watapewa nafasi”.
Mwambusi
alisema kikosi chake kinahitaji kujifua kwa nguvu kuhimili mitanannge
ya ligi kuu, kwani ligi ya Tanzania bara imekuwa na ushindani mkubwa
sana.
“Ligi
imebadilika sana, niliifundisha Prisons miaka ya nyuma, sasa naona
mambo yamebadilika sana, lakini nina uhakika kwa uzoefu wangu
nitajipanga vizuri na kupambana hadi mwisho”. Alisema Mwambusi.
Mbeya
City ni miongoni mwa timu tatu zilizopanda ligi kuu soka Tanzania bara
msimu ujao, wakati nyingine ni Maafande wa Rhino Rangers ya Tabora, na
Ashanti United ya Dar es salaam.
Msimu
uliopita timu tatu za Africa Lyon ya Dar es salaam, Toto Africans ya
Mwanza na Polisi Morogoro zilishuka daraja na sasa zinaendelea na
mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi daraja la kwanza.
SERENA WILLIAMS ATOLEWA NJE KATIKA TENESI MICHUANO YA WIMBLEDON
MWANADADA nyota dunia katika
tenisi kutoka Marekani, Serena Williams ametolewa nje katika michuano ya
Wimbledon baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Sabine Lisicki wa
Ujerumani kwa 6-2 1-6 6-4. Williams
ambaye mbali na kupewa nafasi kubwa ya kunyakuwa taji hilo pia alikuwa
bingwa mtetezi wa michuano hiyo aliyonyakuwa mwaka jana. Kwa
upande mwingine bingwa wa zamani wa michuano hiyo Petra Kvitova
alifanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo baada ya
kumgaragaza Carla Suarez wa Hispania kwa 7-5 6-3. Mashindano
ya Wimbledon mwaka huu yamekuwa sio mazuri kwa nyota wengi wanaoshika
nafasi za juu katika orodha za ubora wa mchezo huo duniani baada ya
Maria Sharapova anayeshika namba mbili kuenguliwa katika mzunguko wa
pili huku Victoria Azarenka anayeshika namba tatu yeye akijitoa baada ya
kupata majeraha.
Saturday, June 29, 2013
ARSENAL WAMTAKA KIPA JULIO CESAR WA QPR ILIYOSHUKA DARAJA"

Arsene Wenger anataka kipa mzoefu atengeneze ushindani kwa Lukasz Fabianski na Wojciech Szczesny.
Mazungumzo
baina ya wawakilishi wa Cesar na viongozi wa Gunners tayari
yamefanyika, lakini hayajamalizika kwa kuwa kipa huyo yupo kwenye
majukumu ya kimataifa.

ARSENAL sasa inatarajiwa kumaliza dili hilo mara moja tu, baada ya
kubainika Roma ya Italia nayo imeingia kwenye mbio za kuwania saini ya
Cesar.
Kipa
huyo wa kimataifa wa Brazil ambaye yupo huru kuondoka Loftus Road
kufuatia kushuka kwa QPR hadi Championship, anataka kubaki London ambako
amezoea maisha tangu awasili msimu uliopita akitokea Inter Milan.
Na
The Gunners – ambayo inatumai kukamilisha pia usajili wa Gonzalo
Higuain wiki ijayo, baada ya kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti
kufungua njia kwa mshambuliaji huyo kuondoka Hispania – inajiamini dili
hilo litakamilishwa baada ya Fainali ya Kombe la Mabara Jumapili.
Wenger
alitaka kusajili kipa wa Stoke, Asmir Begovic na wa Liverpool, Pepe
Reina lakini, licha ya kuwa na fungu la bajeti ya usajili la Pauni
Milioni 70, kocha huyo wa Arsenal ameona hana sababu ya kutumia fedha
nyingi kwa ajili ya kipa.
Rangers
itasikiliza ofa ya kiasi cha Pauni Milioni 2 kwa Cesar, wakati mshahara
wake wa Pauni 70,000 kwa wiki halitakuwa tatizo kwa The Gunners, ambayo
imetuma waangalia vipaji wake nchini Brazil kumuangalia Cesar
anachokifanya katika Kombe la Mabara.
Pamoja
na mpango wa kuwasajili Cesar na Higuain, The Gunners pia wanataka
kumsajili beki wa Swansea, Ashley Williams na kiungo wa Everton,
Marouane Fellaini. Lakini masuala ya kifedha yanatia saka kama Arsenal itaweza kusajili wachezaji wote hao.
Hadi
sasa, Arsenal imegoma kumpa Fellaini mshahara wa Pauni 100,000 kwa wiki
na pia imeshindwa kufika dau la Pauni Milioni 24 za kumnunua.

MBEYA MWENYEJI WA NETIBOLI TENA KWA MARA YA PILI MFULULIZO".
Jiji la Mbeya kwa
mara ya pili mfululizo,litakuwa mwenyeji wa ligi kuu ya
Netiboli taifa ambapo naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
Philip Mulugo anatarijiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi kuanzia
Agosti 24 hadi Septemba 7.
Mwenyekiti
wa chama cha Netiboli Mkoa wa Mbeya, Mary Mung’ong’o ameumabia mtandao
huu kuwa ligi hiyo inafanyika kwa mara nyingine kutokana na ombi la
Waziri Mulugo kwa vile ligi hiyo haikuwa imefana, hivyo akaiomba CHANETA
kuwapa Mbeya fursa nyingine ya uwenyeji.
Alisema
maandalizi ya ligi yameanza na kusema zinahitajika sh milioni 16
kufanikisha na kuongeza kuwa hadi sasa, hawajajua timu ngapi zitashiriki
kutokana na jukumu hilo kuwa chini ya Chama cha Netiboli Tanzania
(CHANETA).
Hata
hivyo, mwenyekiti huyo ametoa wito kwa viongozi wa ngazi mbalimbli
wakiwemo wadau wenye mapenzi na mchezo kutoka mkoani hapa kujitoa kwa
hali na mali kuyafanikisha ili yawe chachu ya kukua kwa mchezo huo
nchini kwa maslahi ya vijana na taifa.
Aidha, mwenyekiti huyo alitamtambulisha Nwaka Mwakisu kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano hayo.
Akizungumzia
mashindano hayo, Mwakisu alisema ni fursa kwa watu wa Mbeya kujitangaza
kibiashara kupitia mchezo huo na kufuta makosa yaliyofanyika mwaka
jana.
Alisema
katika kufakisha mashindano hayo, nguvu ya pamoja inahitajika kuanzia
viongozi wa kisiasa, serikari na vyombo vya habari.
MBASPO FC YATWAA UBINGWA WA AIRTEL RISING KWA MKOA WA MBEYA"
Mbaspo
walianza mbio zao za kutwaa ubingwa kwa kutoshana nguvu ya 3-3 dhidi ya
Mbosa siku ya Jumatatu Juni 24 kabla ya kufanya mauaji makubwa ya 6-0
dhidi ya timu dhaifu ya Mbeya Sekondari siku ya Jumanne. Michezo yote
imefanyika kwenye uwanja wa Magereza jijini Mbeya.
Mbosa
walifikisha point nne juzi Jumatano walipoitandika Mbeya Sekondari 3-0
hivyo kumaliza wakiwa na point nne na magoli sita wakati wapinzani wao
Mbaspo wakifikisha jumla ya magoli tisa ya kufunga. Katika mechi ya
juzi, magoli ya Mbosa yalitiwa kwenye kamba na Michael Mwashilanga,
Riziki Juma na Julius Landa.
Wakati
huo huo, chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mbeya kimetangaza kikosi cha
wachezaji 18 kuuwakilisha mkoa huo kwenye michuano ya Taifa ya Airtel
Rising Stars inayoanza kutimua vumbi kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya
Karume jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 2.
Wachezaji
hao ni Ismail Yesaya, Emmanuel Alex, Gift Sanga, Jackson Mwaibambe,
Boaz Mwangole, Costa Sanga, Seif Zubery, Stanley Angelo, Enock Sikaonga,
Kaunda Malata, Joel Kasimila, Hamprey Nyeo, Elia Salengo, Peter Noah,
Emmaneul Mtimbi, Michael Bosco, Richard Kalinga na Zamoyoni Mwashambwa.
Katika
mkoa wa Morogoro, mji kasoro bahari, timu ya Moro Kids imetoka sare ya
bila kufungana na Techfort katika mchezo wa kushambuliana kwa zamu
uliopigwa kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Morogoro juzi Jumatano
na kushuhudiwa na mashabiki wengi wa mji huo
Airtel
Rising Stars vile vile imeanza kutimua vumbi katika jiji la Mwanza
ambapo timu ya Marsh Athletical imedhihirisha umwambe wake katika soka
baada ya kuifunga Nyamagana United 2-0 kwenye uwanja mkongwe wa
Nyamagana.
Timu
za mikoa zimepangwa kuanza kuwasili jijini Dar es Salaam mwishoni mwa
wiki tayari kwa ajili ya kindumbwe ndumbwe cha Airtel Rising Stars ngazi
ya taifa katika uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. Wachezaji 16
watachaguliwa wakati wa mashindano hayo ili kuunda timu
itakayoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa ya Airtel
Rising Stars. Nchi mwenyeji wa michuano hiyo itatangazwa baadaye mwezi
ujao.
Subscribe to:
Posts (Atom)