Marion Bartoli mwanadada nyota katika
tenisi, amefanikiwa kushinda taji lake la kwanza la
michuano ya Grand Slam baada ya kumchalaza Sabine Lisicki wa Ujerumani
kwa seti 6-1 6-4 kwenye mchezo wa fainali ya michuano ya Wimbledon. Bartoli
ambaye anashika namba 15 katika orodha za ubora kwa upande wanawake
alitumia dakika 30 pekee kushinda seti ya kwanza wakati mpinzani wake
Lisicki akionekana kushindwa kumudu vishindo katika fainali yake ya
kwanza ya Grand Slam. Akihojiwa
mara baada ya mchezo huo Bartoli amesema haamini kama amenyakuwa taji
hilo na alikuwa akijisikia kucheza kwa kiwango chake cha juu huku kila
kitu alichofanya kikimuendea sawa. Michuano
hiyo inaendelea tena baadae kwa mchezo wa fainali kwa upande wa wanaume
ambapo Andy Murray wa Uingereza anayeshika namba mbili katika orodha za
ubora atachuana na Novak Djokovic wa Serbia anayeshika namba moja
katika orodha za ubora.
Sunday, July 7, 2013
HISPAIN YATOLEWA NJE MASHINDANO YA VIJANA FIFA U-20" LEO GHANA VS CHILE


>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
MATOKEO MENGINE"
ROBO FAINALI
France 4 Uzbekistan 0
Magoli:
*Yaya Sanogo (dk31')
*Paul PogbaP (dk35' Penati)
*Florian Thauvin (dk43' Penati)
*Kurt Zouma (dk64')
Uruguay 1 Spain 0
Goli:
*Felipe Avenatti (dk103’)
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>Hivyo sasa kwa ushindi huo Uruguay katika hatua ya Nusu Fainali watashuka dimbani kupepetana na Mshindi wa Mechi ya Iraq vs South Korea.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
RATIBA ROBO FAINALI LE; JULAI 7
[Saa 12 Jioni]
Kayseri
Iraq v South Korea
[Saa 3 Usiku]
Istanbul
Ghana v Chile
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Katika Robo Fainali nyingine iliyochezwa jana Timu ya Taifa ya France
ilifanikiwa kutinga hatua ya Nusu Fainali baada ya kuilaza Uzbekistan kwa Bao 4-0 hivyo sasa kwa matokeo hayo France itacheza na Mshindi kati ya Ghana vs Chile.
Bao za France zilifungwa na Yaya Sanogo, Paul Pogba, Florian Thauvin naKurt Zouma.
RATIBA/MATOKEO:
ROBO FAINALI
06/07 France 4 Uzbekistan 0
06/07 Uruguay 1 Spain 0
07/07 muda 18:00 Iraq v South Korea
07/07 muda 21:00 Ghana v Chile
NUSU FAINALI
10/07 18:00 Bursa France vs Ghana or Chile
10/07 21:00 Trabzon Uruguay vs Iraq or South Korea
MSHINDI WA TATU
Tarehe 3/07 18:00 Uwanja Istanbul Kulingana na matokea
FAINALI
Tarehe 13/07 21:00 Uwanja Istanbul
World Youth Championship{Bingwaaaaaa}
TUKUMBUKE WASHINDI WALIOPITA:
2011 Brazil
2009 Ghana
2007 Argentina
2005 Argentina
2003 Brazil
2001 Argentina
1999 Spain
1997 Argentina
1995 Argentina
1993 Brazil
1991 Portugal
1989 Portugal
1987 Yugoslavia
1985 Brazil
1983 Brazil
1981 Germany
1979 Argentina
1977 U.S.S.R.
BOLT ATUMA SALAMU KWA WAPINZANI WAKE BAADA YA KUIBUKA NA USHINDI.
Usain Bolt Mwanariadha nyota wa
mbio fupi kutoka Jamaica,ametuma salamu kwa wapinzani wake
baada ya kufanikiwa kuibuka na ushindi katika mbio za mita 200 za Diamond League
zilizofanyika jijini Paris kwa kutumia muda wa sekunde 19.73 ukiwa ni
muda wa haraka zaidi kwa mwaka huu. Bolt
ambaye anashikilia rekodi ya dunia katika mbio hizo alifabnikiwa mbio
kirahisi na kuuzidi muda wa haraka zaidi uliowekwa kwa mwaka huu na
Tyson Gay wa Marekani mwezi mmoja kabla ya mashindano ya riadha ya dunia
yatakayofanyika jijini Moscow, Urusi. Akihojiwa
mara baada yam bio hizo Bolt amesema anajisikia vyema kwa kushinda mbio
hizo lakini bado bado ana kazi ya kufanya kuhakikisha anakuwa katika
kiwango chake ifikapo michuano ya dunia. Nafasi
ya pili katika mbio hizo ilikwenda kwa Warren Weir wa Jamaica
aliyetumia muda wa sekunde 19.92 huku nafasi ya tatu ikienda kwa
Christophe Lemaitre wa Ufaransa aliyetumia muda wa sekunde 20.07.
Thursday, July 4, 2013
ROONEY ATAKIWA KUWA SILISHA BARUA KWA MAN U
MSHAMBULIAJI Wayne Rooney atatakiwa
kuwasilisha barua ya maandishi ya kuomba kuondoka ikiwa anataka kuachana
na Manchester United.
Mpachika mabao huyo wa Old Trafford,
alirejea mazoezini jana huku mustakabali wake ukiwa bado haueleweki.
Imefahamika hakuwa na Mkutano mahsusi na kocha mpya David Moyes juu ya
suala lake.
Hilo linaweza kutokea katika kituo cha
mazoezi cha klabu, Carrington leo. Wawili hao walizungumza jana, lakini
si kwa muda mrefu na msimamo wa United kwake bado haujabadilika.
Hajielewi: Mustakabali wa Wayne Rooney bao haueleweki licha ya jana kurejea mazoezini
Wamesema mshambuliaji huyo wa England
hauzwi. Kuhusu tetesi za wapinzani wao katika Ligi Kuu, Arsenal kutaka
rasmi kumsajili tangu wiki iliyopita, United bado haijawasiliana na
yoyote anayemtaka Rooney.
Sakata hili linaweza kugeuka tu iwapo
mshambuliaji mwenyewe ataamua kulazimisha kuondoka. BIN ZUBEIRY
iliandika mwishoni mwa msimu uliopita kwamba, Rooney aliomba kuondoka
kwa kocha aliyestaafu, Sir Alex Ferguson.
Ombi la kuondoka litamaanisha Rooney
hatadai chochote katika Mkataba wake wa miaka miwili uliobakia ambao
alikuwa analipwa Pauni 250,000 kwa wiki.
Huku Moyes akitarajiwa kuzungumza na Waandishi wa Habari kwa mara ya kwanza kesho, ufafanuzi utakuja muda si mrefu.
Wakati huo huo, mchezaji mwenzake wa
zamani Rooney, Mreno Cristiano Ronaldo ameendelea kuweka wazi juu
mapenzi yake na United. Mshambuliaji huyo wa Real Madrid amesema jana
kwamba anataka kurudi Ligi Kuu, lakini hakusema lini.
"Nalikosa kweli soka la England. Kwangu
ilikuwa moja ya miaka bora katika maisha yangu ya soka wakati nipo huko
Manchester United. Ni klabu ambayo bado ipo moyoni mwangu. naikosa kweli
kweli. Lakini kwa sasa maisha yangu yapo Hispania. Nafurahia kucheza
huko pia. Mustakabali hatuwezi kuujua,"alisema Ronaldo.
ISCO ASEMA LENGO KUU NI KUISAIDIA MADRID KUTWAA UEFA

GIGGS NAYE AWA KOCHA MCHEZAJI SAFU YA BENCH LA UFUNDI.

RYAN GIGGS NA MAN U
-UMRI: 39
-MECHI: 941
-MAGOLI: 168
-MATAJI YA LIGI: 13
-FA CUP: 4
-LIGI CUP: 4
-UEFA CHAMPIONZ LIGI: 2
HISPAIN BADO NAMBARI MOJA DUNIANI VIWANGO VYA FIFA
Ivory Coast ndiyo Nchi ambayo iko juu kupita zote Afrika na inakamata Nafasi ya 13.
Brazil, ambao Jumapili iliyopita walitwaa Kombe la Mabara, wamerudi 10 Bora na sasa wapo Nafasi ya 9.
20 BORA:
1 Spain
2 Germany
3 Colombia (Imepanda Nafasi 4)
4 Argentina (Imeshuka 1)
5 Holland
6 Italy (Imepanda 2)
7 Portugal (Imeshuka 1)
8 Croatia (Imeshuka 4)
9 Brazil (Imepanda 13)
10 Belgium (Imepanda 2)
11 Greece (Imepanda 5)
12 Uruguay (Imepanda 7)
13 Ivory Coast
14Bosnia-Herzegovina (Imepanda 1)
15 England (Imeshuka 6)
16Switzerland (Imeshuka 2)
17 Russia (Imeshuka 6)
18 Ecuador(Imeshuka 8)
19 Peru (Imepanda 11)
20 Mexico (Imeshuka 3).
Subscribe to:
Posts (Atom)