GIGGS NAYE AWA KOCHA MCHEZAJI SAFU YA BENCH LA UFUNDI.
KLABU ya Manchester United imemtangaza kiungo wake mkongwe Ryan Giggs kuwa kocha mchezaji wa klabu hiyo. Giggs
mwenye umri wa miaka 39, aliongeza mkataba wa mwaka mmoja Machi mwaka
huu na sasa ataunganisha na majukumu yake mapya yA Kocha mchezaji wa kikosi cha kwanza cha United. Katika
taarifa yake Moyes amesema amefurahishwa na Giggs kuikubali nafasi hiyo
ya kuwa mchezaji na pia kocha na uzoefu wake wakipindi kirefu utasaidia
kuifanya United kuendeleza ubora wake. Giggs
ambaye ni raia wa Wales alianza kuchomoza katika timu ya wakubwa ya
United mwaka 1991 na kufanikiwa kushinda mataji 13 ya Ligi Kuu nchini
Uingereza, manne ya Kombe la FA na medali mbili za Ligi ya Mabingwa
Ulaya.
RYAN GIGGS NA MAN U
-UMRI: 39
-MECHI: 941
-MAGOLI: 168
-MATAJI YA LIGI: 13
-FA CUP: 4
-LIGI CUP: 4
-UEFA CHAMPIONZ LIGI: 2