Thursday, July 4, 2013

HISPAIN BADO NAMBARI MOJA DUNIANI VIWANGO VYA FIFA

LICHA wa kutandikwa na Brazil katika  Michuano ya Kombe la Mabara hatua ya fainali Mabingwa wa Dunia Spain bado wameendelea kukamata Nambari moja katika Listi ya FIFA ya Ubora Duniani iliyotoka leo huku Brazil wakipanda Nafasi 13 na kushika Nafasi ya 9 lakini England  imeporomoka Nafasi 6 hadi kufikia Namba 15 na Tanzania imeshuka Nafasi 12 na sasa ipo ya 121.
Ivory Coast ndiyo Nchi ambayo iko juu kupita zote Afrika na inakamata Nafasi ya 13.
Brazil, ambao Jumapili iliyopita walitwaa Kombe la Mabara, wamerudi 10 Bora na sasa wapo Nafasi ya 9.
Listi nyingine itatolewa Agosti 8.
20 BORA:
Spain
Germany
Colombia (Imepanda Nafasi 4)
Argentina (Imeshuka 1)
5 Holland
Italy (Imepanda 2)
Portugal (Imeshuka 1)
Croatia (Imeshuka 4)
9 Brazil (Imepanda 13)
10 Belgium (Imepanda 2)
11 Greece (Imepanda 5)
12 Uruguay (Imepanda 7)
13 Ivory Coast
14Bosnia-Herzegovina (Imepanda 1)
15 England (Imeshuka 6)
16Switzerland (Imeshuka 2)
17 Russia (Imeshuka 6)
18 Ecuador(Imeshuka 8)
19 Peru (Imepanda 11)
20 Mexico (Imeshuka 3).