Thursday, July 4, 2013

WACHINA WAKABIDHI UWANJA WA TAIFA KWA SERIKALI.

UWANJA_WA_TAIFA_DARSerikali ya Tanzania hatimaye imekabidhi Uwanja wa Taifa wa Jijini Dar es Salaam na wachina ikiwa ni awamu ya Kwanza.
Makabidhiano hayo ya Uwanja huo uliochukua Miaka 7 kujengwa yalifanyika Jana kwa kutia saini na kubadilishana Vyeti kati ya Balozi wa China Nchini Tanzania, Li Youqing, na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Sihaba Mkinga.
Akizungumza, Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dr. Fenella Mukangara, aliishukuru China kwa msaada wao mkubwa wa Fedha na Ujenzi.
Pia, Waziri Mukangara, alisifu Usimamizi wa China wa Uwanja huo tangu ujenzi ulipokamilika na tangu Uwanja huo ulipofunguliwa rasmi hapo Tarehe 25 Februari 2009 na Rais wa zamani wa China, Hu Jintao, na Rais Jakaya Kikwete.
Uwanja wa Taifa, unaochukua Washabiki 60,000 wote wakiwa Vitini, umegharimu Shilingi Bilioni 56 na kati ya hizo China ilitoa Bilioni 33.4 na Tanzania ilitoa Fedha zilizobaki.
Uwanja huu ni wa kisasa na upo katika Viwango vinavyokubalika na FIFA na Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki.
Serikali imedokeza kuwa hivi sasa wapo kwenye mazungumzo ya kutafuta Fedha ili kugharamia Ujenzi wa Awamu ya Pili na inatarajiwa Serikali ya China itahusishwa na pia Mkandarasi aliejenga Awamu ya Kwanaza, Beijing Construction Engineering Company Limited, ndio watashughulikia Awamu hii.
Baada ya kukamilika kwa Ujenzi wa Awamu ya Pili, Tanzania itakuwa iko tayari kuwa Mwenyeji wa Mashindano makubwa ya Michezo ya kila aina.