Friday, February 14, 2014

KIA WAJIPANGA KUKABILIANA NA DAWA ZA KULEVYA

                                                       Uwanja cha Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)
Uongozi wa Uwanja cha Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), umeahidi kuongeza jitihada za kupambana na usafirishaji wa dawa za kulevya kutokana maboresho yaliyofanyika katika kitengo cha usalama cha uwanja huo.

Tamko hilo limekuja siku chache baada ya Mtanzania Mastura Makongoro, mwenye hati ya kusafiria namba AB26695, kukamatwa na dawa za kulevya zinazodhaniwa kuwa ni aina ya cocaine zenye uzito wa kilo 4.8 akielekea nchini Ghana.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Fedha na Huduma za Kibiashara wa Kampuni ya Uendelezaji Viwanja (Kadco), Bakari Murusuri, ilisema uwanja huo umejidhatiti kupambana na usafarishaji wa dawa za kulevya kupitia hapo.

Murusuri alisema maofisa usalama wa uwanja huo Jumanne usiku wa manane  wiki hii, walimkamata mwanamke huyo wakati akisubiri kupanda ndege ya Shirikia la Ethiopia kuelekea Addis Ababa.

“Mizigo yote ya abiria imekuwa ikichunguzwa kwa umakini mkubwa katika sehemu ya kuchunguza mizigo na safari hii tumefanikiwa mzigo mmoja uligundulika kuwa na shaka na vitu vilivyokuwa ndani kwa kuonyesha dalili ya kuwa ni dawa za kulevya," alisema.

Aliongeza: “Baada ya kuuchunguza mzigo huo kwa umakini, iligundulika ulikuwa na dawa za kulevya ambazo zilifungwa juu na chini kabisa ya begi lake yenye uzito wa kilo 4.8.”

Alisema wakati wa uchunguzi, mwanamke huyo alikiri kuwa aliambatana na mwenzake raia wa Nigeria aliyemtaja kwa jina la Mike Nwankwo (41), ambaye alimsindikiza mpaka uwanjani na alikuwa ni miongoni mwa mtandao wa wasafirishaji wa dawa hizo.

“Jeshi la Polisi na walinzi wa usalama hapa uwanjani waliunganisha nguvu ili kumsaka mtu huyo na baadaye alikutwa kwenye maegesho ya magari akisubiri kuhakikisha kuwa mwanamke huyo ameondoka nchini,” aliongeza.

Murusuri alisema tangu Machi, 2013 mpaka sasa, uwanja huo wa ndege umefanikiwa kukamata watu tisa wakihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya na kuahidi kuwa uwanja huo sasa umejipanga kikamilifu kukabiliana na suala hilo.

“Tumeongeza ulinzi wa kutosha hapa KIA ili kuondoa mianya katika taratibu za kiusalama kwa upande wa mizigo na uchunguzi kwa ujumla.
Hili litatuwezesha kuhakikisha kuwa uwanja wetu wa ndege hauwi kitovu cha usafirishaji dawa za kulevya,” aliongeza.
Chanzo: Nipashe'.

Thursday, February 13, 2014

ENGLAND YAPOROMOKA VIWANGO VYA FIFA VS SPAIN 1

FIFA_LOGO_BESTShirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA leo limetoa Listi ya Ubora Duniani  huku Nchi 3 za Juu, Spain, Germany na Argentina, bado ziko pale pale na Portugal kupanda nafasi moja na kukamata Nambari ya 4 huku Tanzania ikipanda Nafasi mbili na kushika Nafasi ya 116.
Brazil, Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia hapo Juni, wamekwea Nafasi moja hadi Nafasi ya 9 lakini England imezidi kuporomoka na safari hii imeanguka Nafasi mbili na kuwa wa 15.
Nchi ya Afrika ambayo iko Juu kabisa ni Ivory Coast ambayo iko Nafasi ya 23 baada ya kuanguka Nafasi 6.
Listi nyingine ya Ubora itatolewa hapo Machi 13.
20 BORA:
1. Spain
2. Germany
3. Argentina
4. Portugal (+1)
5. Colombia (-1)
6. Switzerland (+2)
7. Uruguay (-1)
8. Italy (-1)
9. Brazil (+1)
10. Netherlands (-1)
11. Belgium
12. Greece
13. United States (+1)
14. Chile (+1)
15. England (-2)
16. Croatie
17. Bosnia-Herzegovina (+2)
18. Ukraine
18. France (+2)
20. Denmark (+5)

JESHI LA POLISI MKOANI SINGIDA LANASA PEMBE ZA NDOVU

Jeshi la polisi mkoani SINGIDA limekamata vipande 21 vya meno ya Tembo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 43.


Nyara hizo za serikali zimekamatwa katika  kijiji cha MWAMAGEMBE  wilayania MANYONI  zikisafirishwa kwenda ITIGI mkoani SINGIDA.



Vitendo vya ujangili vimeendelea kukithiri nchini ambapo Jeshi la POLISI Mkoani SINGIDA limemtia mbaroni  GEORGE JAMES kwa tuhuma za kukutwa na meno ya TEMBO yakiwa yamehifadhiwa katika mabegi mawili ya kusafiria.


Mtuhumiwa huyo alikamatwa katika kizuizi cha idara ya maliasili kilichoko katika kijiji UKIMBU ,kata ya MGANDU wilayania MANYONI akiwa katika gari aina ya TOYOTA HIACE lenye namba za usajili T797CQL akiwa amehifadhi men o hayo katika mabegi ya nguo.


Kamanda wa polisi mkoa wa SINGIDA ,GEOFREY KAMWELA amesema vipande hivyo 21 vina thmani ya zaidi ya shilingi milioni 43 na vyote vimehifadhiwa katika kituo cha polisi wilayani ITIGI.


vitendo vya ujangili wilayani MANYONI vimekuwa vikiongezeka ambapo mwaka 2013 askari mmoja wa jeshi  polisi alipoteza maisha katika mapambano na majangili wilayani humo.

SIMBA SC :MKUTANO MKUU WA KATIBA MACHI 16.

Mkutano Mkuu wa Marekebisho ya Katiba ya klabu ya Simba umepangwa kufanyika Machi 16 mwaka huu badala ya Machi 23 kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.
Uamuzi wa kurudisha nyuma tarehe ya mkutano huo ulifikiwa jana (Jumatano), katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya Klabu kilichokutana usiku Makao Makuu ya Klabu, Mtaa wa Msimbazi, jijini Dar es Salaam.

Kamati ya Utendaji ya Simba imefikia uamuzi huo kufuatia maelekezo kutoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), iliyowataka wanachama wake wote mpaka kufikia Machi 20 mwaka huu wawe wameshazifanyia marekebisho katiba zao kwa kuweka kipengele kinachoitambua Kamati za Maadili.

Simba ilipokea barua hiyo na kwa kuzingatia umuhimu huo Uongozi ukaamua kuifanyia kazi kwa kuitisha Mkutano Mkuu ambapo agenda itakuwa ni moja tu nayo ni marekebisho ya katiba.

Mbali na kipengele hicho mkutano huo pia utajadili mapendekezo yote ya marekebisho ya katiba yaliyowasilishwa kwa uongozi ili kujadiliwa na kutolewa maamuzi.

Uongozi wa Simba unawataka wanachama wake kujitokeza kwa wingi siku hiyo kushiriki katika zoezi hilo kwa maslahi ya klabu yao.

Kwa sasa uongozi unafanya mipango ya kutafuta mahali pazuri utakapofanyika mkutano huo na mara baada ya kupatikana basi uongozi utawatangazia wanachama wake.

Asha Muhaji

Ofisa Habari, Simba Sports Club

OKWI APATA KIBALI CHA FIFA KUKIPIGA YANGA

Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limeruhusu mshambuliaji Emmanuel Okwi kuichezea Yanga Taariifa za uhakika kutoka ndani ya TFF ambazo zimethibistishwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Mwesigwa Celestine zimesema kuwa Okwi sasa ni huru. 
Kweli hilo tumetaarifiwa lakini tutalizungumzia baadaye,” alisema.  
TFF ndiyo ilisimamisha usajili wa Okwi kwa madai ya kutaka ufafanuzi kutokana na kesi tatu za kimsingi kati ya Okwi, Etoile du Sahel. 
Sasa Okwi atakuwa huru kuanza kuitumikia Yanga ambayo imesamjili kwa dau la zaidi ya dola 100,000 (Sh milioni 160).

TWIGA STAR YAFIKA SALAMA LUSAKA ZAMBIA.

Kikosi cha wachezaji 19 wa Twiga Stars kimetua Lusaka, Zambia leo (Februari 13
mwaka huu) huku Kocha Mkuu Rogasian akiahidi ushindani kwenye mechi dhidi
ya wenyeji itakayochezwa Uwanja wa Nkoloma.
Kocha Kaijage aliwaambia waandishi wa habari kwenye Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Kenneth Kaunda mara baada ya kikosi chake kutua kwa ndege ya
Fastjet saa 3.30 asubuhi kwa saa za Zambia kuwa wamekuja kushindana, na si kushiriki.
Twiga Stars ambayo mara ya mwisho ilikutana na Zambia kwenye michuano ya
COSAFA miaka miwili iliyopita na kuibuka na ushindi imefikia hoteli ya Golden
Peacock, na katika uwanja wa ndege ilipokewa na viongozi wa Chama Soka
Zambia (FAZ) na Ofisa Ubalozi wa Tanzania nchini Zambia, Jeswald Majuva.
Timu hiyo leo saa 9 alasiri kwa saa za Zambia ambapo Tanzania ni saa 10 jioni
itafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Nkoloma ambao ndiyo utakaotumika kwa
mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) itakayochezwa kesho.
Wachezaji waliopo kwenye kikosi hicho ni Amina Ali, Anastazia Katunzi, Asha
Rashid, Donisia Minja, Esther Chabruma, Etoe Mlenzi, Everine Sekikubo, Fatuma
Issa, Fatuma Makusanya, Fatuma Mwisendi, Fatuma Omari, Happiness Mwaipaja,
Maimuna Mkane, Mwapewa Mtumwa, Sherida Boniface,Sophia Mwasikili, Therese
Yona, Vumilia Maarifa na Zena Said.

MESSI AWEKA REKODI FC BARCA JANA ATUPIA 1

Mshambuliaji mahiri wa argentina na club ya barcelona Lionel Messi amefanikiwa kuweka rekodi nyingine ya mabao wakati Barcelona ikitinga fainali ya Kombe la Hispania kuelekea mechi na Manchester City wiki ijayo Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Messi alifanikiwa kuifungia timu yake jana katika sare ya 1-1 na Real Sociedad na kufikisha mabao 335 hivyo kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika klabu hiyo ya Hispania.

Barca imeingia fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-1 baada ya awali kushinda 2-0 na sasa itakutana na Real Madrid katika mechi ya kuwania Kombe.
COPA del REY
NUSU FAINALI

{Saa za Bongo}

Marudiano

Jumanne Februari 11

Atletico de Madrid 0          Real Madrid CF 2 {0-5}

Jumatano Februari 12

Real Sociedad 1 FC Barcelona 1 {1-3}

FAINALI

Aprili 19

Real Madrid v Barcelona