Monday, February 17, 2014
WENGER AMJIBU MBWATUKAJI MOURINHO
KAKA ASEMA NI MCHEZA NA MCHEZAJI BORA CRISTIANO RONALDO
KIUNGO Mahiri wa klabu ya AC
Milan ya Italia, Kaka amebainisha kuwa Lionel Messi na Zinedine Zidane
ni wachezaji bora aliokutana nao na kudai kuwa Cristiano Ronaldo ndio
mchezaji bora kabisa kuwahi kucheza naye. Kiungo huyo wa kimataifa wa
Brazil, amewahi kukutana na Messi mara kadhaa wakati akicheza Real
Madrid ambako alikuwa akicheza sambamba na Ronaldo. Kaka aliandika
katika ukurasa rasmi wa twitter wa Milan wakati akijibu maswali ya
mashabiki ambapo amesema wachezaji bora aliowahi kucheza dhidi yao ni
Zidane na Messi huku akimtaja Ronaldo kama mchezaji bora aliyewahi
kucheza naye. Kaka pia alimtaja Paulo Maldini kama beki bora kabisa
duniani kuwahi kucheza naye kabla hajaondoka Milan kwenda Madrid.
TPS KUWAWEZESHA WASICHANA WALIOKOSA FURSA

Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), imeahidi kuchangia Sh. milioni 1.7 kwa ajili ya kitengo cha wasichana waliokosa fursa.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa TPSF, Godfrey Simbeye, aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitengo hicho kilichopo chini ya usimamizi wa Chama cha Wanawake Wafanyabiashara, kazi za mikono na nguo. (Tahowete).
Simbeye alisema atakwenda kuwaombea fedha hizo TPSF ili kuwasaidia wasichana hao watano katika shule ya ushonaji na kuongeza kuwa wajasiriamali wangewezeshwa kwa kuwa wakifanya biashara wanaweza na bila kuwezeshwa hawawezi kufanya jambo lolote.
Aidha alisema serikali ina mpango wa kuanzisha miradi ambayo wanataka iwawezeshe wanawake,.
Mwenyekiti wa Tawohate, Anna Matinde, alisema chama hicho kinasaidia jamii hasa wasichana wanaomaliza masomo na kukosa ajira, pamoja na wale wanaonyanyasika kijamii kwa kuanzisha miradi ambayo wasichana hao waliokatiza masomo waweze kuendelea na masomo.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa TPSF, Godfrey Simbeye, aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitengo hicho kilichopo chini ya usimamizi wa Chama cha Wanawake Wafanyabiashara, kazi za mikono na nguo. (Tahowete).
Simbeye alisema atakwenda kuwaombea fedha hizo TPSF ili kuwasaidia wasichana hao watano katika shule ya ushonaji na kuongeza kuwa wajasiriamali wangewezeshwa kwa kuwa wakifanya biashara wanaweza na bila kuwezeshwa hawawezi kufanya jambo lolote.
Aidha alisema serikali ina mpango wa kuanzisha miradi ambayo wanataka iwawezeshe wanawake,.
Mwenyekiti wa Tawohate, Anna Matinde, alisema chama hicho kinasaidia jamii hasa wasichana wanaomaliza masomo na kukosa ajira, pamoja na wale wanaonyanyasika kijamii kwa kuanzisha miradi ambayo wasichana hao waliokatiza masomo waweze kuendelea na masomo.
Chanzo:
Nipashe
Sunday, February 16, 2014
JUVE WAJIHAKIKISHIA UBINGWA WAKO JUU POINTI 12 MBELE YA AS ROMA
JUVENTUS Mabingwa wa Italy wakiwa katika dimba la Nyumbani wamefanikiwa kuichapa Timu ya Chievo Verona
Bao 3-1 Mabao ya Kwadwo Asamoah, Mchezaji kutoka Ghana, na Claudio
Marchisio pamoja na Fernando Llorente huku Chievo Verona ikijipatia Bao moja baada ya Juve kujifunga wenyewe wakati
Stefan Lichtsteiner akiwa katika harakati za kuokoa na Mpira kumgonga Martin Caceres na kutinga wavuni
Jumamosi Februari 15
ACF Fiorentina 1 Inter Milan 2
[Saa za Bongo]
Calcio Catania 3 SS Lazio 1
Atalanta BC 0 Parma FC 4
Juventus FC 3 AC Chievo Verona 1
Cagliari Calcio 1 AS Livorno Calcio 2
Genoa CFC 3 Udinese Calcio 3
US Sassuolo Calcio 0 SSC Napoli 2
2245 AS Roma v UC Sampdoria
Jumatatu Februari 17
2245 Hellas Verona FC v Torino FC
NA | TIMU | P | W | D | L | F | A | GD | PTS |
1 | Juventus FC | 24 | 20 | 3 | 1 | 59 | 19 | 40 | 63 |
2 | AS Roma | 22 | 15 | 6 | 1 | 45 | 11 | 34 | 51 |
3 | SSC Napoli | 24 | 15 | 5 | 4 | 49 | 27 | 22 | 50 |
4 | ACF Fiorentina | 24 | 13 | 5 | 6 | 43 | 26 | 17 | 44 |
5 | Inter Milan | 24 | 10 | 9 | 5 | 42 | 28 | 14 | 39 |
6 | Parma FC | 23 | 9 | 9 | 5 | 36 | 27 | 9 | 36 |
7 | Hellas Verona | 23 | 11 | 3 | 9 | 39 | 37 | 2 | 36 |
8 | Torino FC | 23 | 8 | 9 | 6 | 36 | 30 | 6 | 33 |
9 | AC Milan | 24 | 8 | 8 | 8 | 37 | 35 | 2 | 32 |
LA LIGA-REAL MADRID YAINYUKA GETAFE CF NYUMBANI 3-0
Ambapo hapo Jana, fc Barcelona waliifumua Rayo Vallecano Bao 6-0 na Atletico Madrid waliichapa Real Valladolid Bao 3-0.
RATIBA
Jumamosi Februari 15
Atletico de Madrid 3 Real Valladolid 0
Levante 1 UD Almeria 0
FC Barcelona 6 Rayo Vallecano 0
Villarreal CF 0 Celta de Vigo 2
Jumapili Februari 16
Granada CF 1 Real Betis 0
Getafe CF 0 Real Madrid 3
2100 Athletic de Bilbao v RCD Espanyol
2300 Sevilla FC v Valencia
Jumatatu Februari 17
2400 Malaga CF v Real Sociedad
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA |
TIMU |
P |
W |
D |
L |
F |
A |
GD |
PTS |
1 |
FC Barcelona |
24 |
19 |
3 |
2 |
69 |
17 |
52 |
60 |
2 |
Real Madrid CF |
24 |
19 |
3 |
2 |
68 |
24 |
44 |
60 |
3 |
Atletico Madrid |
24 |
19 |
3 |
2 |
59 |
16 |
43 |
60 |
4 |
Athletic Bilbao |
23 |
13 |
5 |
5 |
42 |
28 |
14 |
44 |
5 |
Villarreal CF |
24 |
12 |
4 |
8 |
44 |
29 |
15 |
40 |
6 |
Real Sociedad |
23 |
10 |
7 |
6 |
42 |
34 |
8 |
37 |
7 |
Sevilla FC |
23 |
8 |
7 |
8 |
42 |
41 |
1 |
31 |
8 |
Valencia |
23 |
9 |
4 |
10 |
36 |
35 |
1 |
31 |
TAMBWE JEZI NAMBA 17 NA MABAO 17 MSIMBAZI SIMBA SC
kutokana katika mechi 23 alizoichezea Simba SC hadi sasa za
mashindano yote na kirafiki, amefunga mabao 17.
Kwa sasa, Tambwe ndiye mchezaji anayeongoza kwa mabao katika
Ligi Kuu, akiwa amefunga mabao 15 na anafuatiwa kwa mbali na mshambuliaji wa
AzamFC, Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast, mwenye mabao
10.
Tambwe amekuwa kipenzi cha wana Msimbazi kutokana na kuweza
pia kutikisa nyavu za mahasimu, Yanga SC katika mechi mbili mfululizo
baina ya timu hizo.
Tambwe alikuja Simba SC kwa pamoja na Mrundi mwenzake, beki
Gilbert Kazewakitokea wote Vital’O msimu huu, baada ya kung’ara katika
Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame nchini Sudan wakiiwezesha
klabu yao kutwaa taji la michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika
historia yake.
Hata hivyo, Kaze amepoteza namba katika kikosi cha kwanza
tangu ujio wa kocha Mcroatia, Zdravko Logarusic, ambaye amekuwa akimpanga
beki Mkenya, Donald Mosoti aliyetokea naye Gor Mahia ya Kenya.
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
MTOTO ALIYETAMBULIKA KWA JINA LA
FRED ROBERT (08) MWANAFUNZI WA DARASA LA PILI KATIKA SHULE YA MSINGI
MBALIZI NA MKAZI WA MBALIZI ALIFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA
NA PIKIPIKI ISIYOFAHAMIKA NAMBA ZAKE ZA USAJILI WALA DEREVA WAKE.
TUKIO HILO LILITOKEA MNAMO TAREHE 15.02.2014 MAJIRA YA SAA 13:00HRS MCHANA HUKO MBALIZI WILAYA YA MBEYA VIJIJINI.
CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI WA PIKIPIKI HIYO. DEREVA ALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO, JUHUDI ZA KUMTAFUTA ZINAENDELEA.
MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI TEULE YA IFISI. KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI ROBERT MAYALA ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI ALIPO MTUHUMIWA WA TUKIO HILI AZITOE KWA JESHI LA POLISI ILI AKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
TUKIO HILO LILITOKEA MNAMO TAREHE 15.02.2014 MAJIRA YA SAA 13:00HRS MCHANA HUKO MBALIZI WILAYA YA MBEYA VIJIJINI.
CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI WA PIKIPIKI HIYO. DEREVA ALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO, JUHUDI ZA KUMTAFUTA ZINAENDELEA.
MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI TEULE YA IFISI. KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI ROBERT MAYALA ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI ALIPO MTUHUMIWA WA TUKIO HILI AZITOE KWA JESHI LA POLISI ILI AKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
JESHI LA POLISI LINAWASHIKILIA WATU WAWILI WAKIWA NA SILAHA [PISTOL] BILA KIBALI.
JESHI LA POLISI
MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WAWILI 1. JACKSON MWAKALUNGWA (24) NA
2. SAIKO WAILODI (35) DEREVA WOTE WAKAZI WA MLOWO WAKIWA NA SILAHA AINA
YA PISTOL ILIYOTENGENEZWA KIENYEJI NA INAYOTUMIA RISASI ZA SHOTGUN.
WATUHUMIWA HAO WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 14.02.2014 MAJIRA YA SAA 14:25HRS MCHANA HUKO KATIKA KIJIJI CHA MAHENGE WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA.
MTUHUMIWA JACKSON MWAKALUNGWA ALIKAMATWA AKIWA NDANI YA GARI AINA YA TOYOTA HIACE AKIELEKEA WILAYA YA MBARALI KUFANYA UHALIFU NA ALIKIRI KUAZIMISHWA SILAHA HIYO NA MTUHUMIWA ALIYEMTAJA KWA JINA LA SAIKO WAILODI. TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYWA ILI WATUHUMIWA WAFIKISHWE MAHAKAMANI.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI ROBERT MAYALA ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUJIMILIKISHA SILAHA BILA KIBALI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA.
AIDHA ANATOA WITO KWA JAMII KUTOA TAARIFA KWA JESHI LA POLISI ZA MTU/WATU WANAOWATILIA MASHAKA AU PINDI WAONAPO VIASHIRIA VYA WATU KAMA HAO KATIKA MAENEO YAO ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
WATUHUMIWA HAO WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 14.02.2014 MAJIRA YA SAA 14:25HRS MCHANA HUKO KATIKA KIJIJI CHA MAHENGE WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA.
MTUHUMIWA JACKSON MWAKALUNGWA ALIKAMATWA AKIWA NDANI YA GARI AINA YA TOYOTA HIACE AKIELEKEA WILAYA YA MBARALI KUFANYA UHALIFU NA ALIKIRI KUAZIMISHWA SILAHA HIYO NA MTUHUMIWA ALIYEMTAJA KWA JINA LA SAIKO WAILODI. TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYWA ILI WATUHUMIWA WAFIKISHWE MAHAKAMANI.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI ROBERT MAYALA ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUJIMILIKISHA SILAHA BILA KIBALI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA.
AIDHA ANATOA WITO KWA JAMII KUTOA TAARIFA KWA JESHI LA POLISI ZA MTU/WATU WANAOWATILIA MASHAKA AU PINDI WAONAPO VIASHIRIA VYA WATU KAMA HAO KATIKA MAENEO YAO ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
Signed by:
[ROBERT MAYALA – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
Subscribe to:
Posts (Atom)