Wednesday, April 2, 2014

UCL:MAN UNITED YAOMYESHA UBABE DHIDI YA BAYERN MUNICH.

MABINGWA watetezi ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich, jana Usiku wamefanikiwa kupambana na kupata Sare ya Bao 1-1 waliposhuka dimbani Uwanjani Old Trafford kupambana na Mabingwa wa England Man United katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na Bayern kumaliza Mtu 10 baada ya Kiungo wao mahiri, Bastian Schweinsteiger, kutolewa kwa Kadi Nyekundu kufuatia Kadi za Njano mbili.
Bayern walimiliki sana Mpira katika Kipindi cha Kwanza lakini ni Man United ndio waliokosa nafasi ya wazi wakati Danny Welbeck alipobaki yeye na Kipa Neuer na kujaribu kufunga kiufundi lakini Kipa huyo wa Germany akaokoa Bao la wazi.
Mapema kwenye Dakika ya 3, Welbeck alifanikiwa kufunga Bao safi lakini Refa Carlos Velasco Carballo kutoka Spain alilikataa na kuwaacha Wachambuzi wengi kukuna vichwa vyao kwanini Bao hilo lilikataliwa.
Hadi Mapumziko Mechi hii ilikuwa 0-0.
Kipindi cha Pili, Dakika ya 58, Man United walifunga Bao kwa Kichwa cha Nahodha wao Nemanja Vidic baada kuunganisha Kona ya Wayne Rooney.
Bayern walisawazisha katika Dakika ya 66 baada ya Krosi ya kumkuta Mario Mandzukic aliemsogezea Bastian Schweinsteiger na kufunga.
Katika Mechi ya Marudiano, mbali ya kumkosa Bastian Schweinsteiger pia itamkosa Javi Martinez baada Mchezaji huyo kuzoa Kadi ya Njano ambayo itamfanya akose Mechi ya Marudiano.
Timu hizi zitarudiana huko Allianz Arena Jijini Munich hapo Jumatano Aprili 9.
VIKOSI:
MANCHESTER UNITED: De Gea; Jones, Ferdinand, Vidic, Büttner; Valencia, Carrick, Fellaini, Giggs, Welbeck; Rooney
Akiba: Lindegaard, Hernandez, Nani, Young, Fletcher, Januzaj, Kagawa.
BAYERN MUNICH: Neuer; Rafinha, Boateng, Martinez, Alaba; Lahm; Robben, Kroos, Schweinsteiger, Ribéry; Muller
Akiba: Starke, Van Buyten, Mandzukic, Shaqiri, Pizarro, Gotze, Hojbjerg.
REFA: Carlos Velasco Carballo (Spain).
Robo Fainali
Mechi za Kwanza
Jumanne Aprili 1
Barcelona 1 Atletico Madrid 1
Manchester United 1 Bayern Munich 1
Katika mtanange mwingine usiku wa jana kwa mara ya 4 Msimu huu, Barcelona na Atletico Madrid zimetoka tena Sare ya bao 1-1 Uwanjani Nou Camp katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Licha ya Barca kutawala Kipindi cha Kwanza, hadi Mapumziko Bao zilikuwa 0-0 na kila Timu ilipata pigo baada kupata Majeruhi kwa Barca kulazimika kumtoa Pique na kumuingiza Bartra na Atletico kumtoa Diego Costa na Ribas Diego kuwa mbadala.
Kipindi cha Pili, Atletico walitangulia kuingia wavuni katika Dakika ya 57 kwa Bao la Ribas Diego na Neymar kusawazisha katika Dakika ya 71.
Timu hizi zitarudiana huko Estadio Vicente Calderon hapo Jumatano Aprili 9.
 VIKOSI:
BARCELONA: Pinto; Alves, Piqué, Mascherano, Alba; Busquets, Xavi; Cesc, Iniesta, Neymar; Messi
Akiba: Oier, Adriano, Song, Bartra, Sergi Roberto, Alexis, Pedro.
ATLÉTICO MADRID: Courtois; Juanfran, Godin Miranda, Filipe Luis; Tiago, Gabi; Arda Turan, Villa, Koke; Diego Costa
Akiba: Aranzubia, Alderweireld, Insua, Mario Suarez, Cristian Rodriguez, Sosa, Diego.
REFA: Felix Brych (Germany)
Jumatano Aprili 2
Real Madrid v Borussia Dortmund
Paris Saint-Germain v Chelsea
Marudiano
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Jumanne Aprili 8
Chelsea v Paris Saint-Germain
Borussia Dortmund v Real Madrid
Jumatano Aprili 9
-DROO YA NUSU FAINALI: 11 Aprili
-Mechi kuchezwa 22 & 23 Aprili na Marudiano 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
WASHINDI [Miaka ya karibu]:
MSIMU MSHINDI NCHI MSHINDI WA PILI NCHI GOLI
2012-13 Bayern Munich Germany Borussia Dortmund Germany 2-1
2011-12 Chelsea England Bayern Munich Germany 1-1 (4–3)
2010-11 Barcelona Spain Manchester United England 3-1
2009-10 Internazionale Italy Bayern Munich Germany 2-0
2008-09 Barcelona Spain Manchester United England 2-0
2007-08 Man United England Chelsea England 1-1 (6–5)
UEFA CHAMPIONZ LIGI
WAFUNGAJI BORA 2013/14:
C. Ronaldo-Real Madrid Goli 13
Zlatan Ibrahimovic-PSG Goli 10 [Penati 1]
Messi-Barcelona Goli 8 [Penati 2]
Diego Costa-Atletico Madrid Goli 7
Sergio Agüero-Manchester City Goli 6 [Penati 2]

Tuesday, April 1, 2014

NGORONGORO HEROES KWENDA NAIROBI.

Kikosi cha watu 27 wakiwemo wachezaji na benchi la ufundi cha timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) kinatarajia kuondoka keshokutwa (Aprili 3 mwaka huu) kwenda Nairobi, Kenya.
TFF_LOGO12Ngorongoro Heroes inayofundishwa na John Simkoko ipo kambini tangu Machi 23 mwaka huu kujiandaa kwa mechi dhidi ya Kenya (U20). Mechi hiyo ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri huo itachezwa Jumapili (Aprili 6 mwaka huu) saa 10 kamili jioni Uwanja wa Machakos ulioko kilometa 80 kutoka jijini Nairobi.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo (Aprili 1 mwaka huu), Kocha Simkoko amesema wachezaji wake wapo tayari kwa ajili ya mechi hiyo, na nia ni kupata matokeo mazuri kabla ya mchezo wa marudiano utakaochezwa nchini wiki tatu baadaye.
Kikosi cha Ngorongoro Heroes chenye wachezaji 20 na viongozi saba kitaondoka saa 4.30 asubuhi kwa ndege ya Kenya Airways. Msafara wa timu hiyo utaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Ayoub Nyenzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana.
Mechi hiyo itachezeshwa na waamuzi Abdoulkarim Twagiramukiza, Ambroise Hakizimana, Raymond Bwiliza na Louis Hakizimana wote kutoka Rwanda wakati Kamishna ni Maxwell Mtonga wa Malawi.
Ngorongoro Heroes itaagwa kesho (Aprili 2 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF.
MIKOA KUMI YATUMA WAWAKILISHI WAKE RCL
Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa kumi vimewasilisha majina ya mabingwa wao watakaoshiriki Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL).
Mabingwa hao ni Arusha (AFC), Kilimanjaro (Panone FC), Lindi (Kariakoo SC), Manyara (Tanzanite SC), Mara (JKT Rwamukoma), Morogoro (Volcano FC), Mtwara (Pachoto Shooting Stars), Pwani (Kiluvya United), Shinyanga (Bulyanhulu FC), Singida (Singida United) na Tanga (African Sports).
Mikoa ambayo haijawasilisha mabingwa wake ni Dar es Salaam, Dodoma, Geita, Iringa, Kagera, Katavi, Kigoma, Mbeya, Morogoro, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Simiyu na Tabora wakati mikoa ya Dodoma na Mwanza imeomba kuongezewa muda kutokana na sababu mbalimbali.
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliagiza kuwa mikoa yote iwe imemaliza ligi na kuwasilisha jina la bingwa wake Machi 30 mwaka huu.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

CAF KOMBE LA SHIRIKISHO: DROO RAUNDI YA MCHUJO YACHUKUWA NAFASI LEO

DROO ya Raundi ya Mchujo ya Mashindanoya CAF ya Kombe la Shirikisho imefanywa Leo huko Mjini Cairo, Misri na kuibua Mechi za mvuto ikiwemo Dabi ya Jiji la Bamako huko Nchini Mali.
Droo hii ilihusisha Timu 8 zilizoshinda Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Kombe la Shirikisho na Timu 8 zilizotolewa kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya CAF CHAMPIONZ LIGI.
Waliokuwa Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri, ambao walibwagwa na Al Ahly Benghazi ya Libya kwenye CAF CHAMPIONZ LIGI na kutupwa Kombe la Shirikisho, wamepangiwa kucheza na Klabu ya Morocco, Difaa El Jadida.
Dabi ya Jiji lCAF-LOGO14a Bamako, itahusisha Klabu za huko Nchini Mali, Real Bamako, iliyotokea CAF CHAMPIONZ LIGI, dhidi ya Djoliba.
Mechi za Raundi ya Mchujo zitachezwa Aprili 18 na Marudiano Wiki moja baadae na Washindi 8 wataingizwa kwenye Droo ya Makundi ambapo Makundi mawili ya Timu 4 kila moja yatapangwa.
CAF Kombe la Shirikisho
Raundi ya Mchujo
Al Ahly (Egypt) vs Difaa El Jadida (Morocco)
Real Bamako (Mali) vs Djoliba (Mali)
AC Leopards (Congo) vs Medeama (Ghana)
Kaizer Chiefs (South Africa) vs ASEC Mimosas (Cote d'Ivoire)
Coton Sport (Cameroon) vs Petro Luanda (Angola)
Horoya (Guinea) vs ES Tunis (Tunisia)
Sewe Sport (Cote d'Ivoire) vs Bayelsa United (Nigeria)
Nkana (Zambia) vs Bizertin (Tunisia).
**Mechi kuchezwa Aprili 18 na Marudiano Wiki moja baadae
**Washindi 8 kuingizwa Droo ya Kupanga Makundi mawili

UCL:KAZI IPO MAN UNITED VS BAYERN MUNICH,BARCA KUIKABIRI ATLETICO MADRID

ROBO FAINALI
Robo Fainali
Mechi za Kwanza
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Jumanne Aprili 1
Barcelona v Atletico Madrid
Manchester United v Bayern Munich
Leo Usiku Uwanja wa Old Trafford huko Jijini Manchester utashuhudia mtanange mkali kati ya Mabingwa wa England, Manchester United, na Mabingwa wa Ulaya, ambao pia ndio Mabingwa wa Germany, Bayern Munich, katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL.
Mara ya mwisho kukutana kwa Timu hizi kwenye Michuano ya Ulaya ni Mwaka 2010 wakati Bayern Munich ilipoitoa Man United kwenye Robo Fainali kwa Bao za Ugenini.
Safari hii, hali ipo tofauti kwani Man United wanaingia kwenye Mechi hii huku Wachambuzi wengi hawawapi matumaini makubwa ya kufanya viziru dhidi ya Bayern Munich inayosifiwa kuwa ndio Timu Bora Ulaya hivi sasa na Juzi ilitwaa tena Ubingwa wa Germany huku wakiwa na Mechi 7 mkononi wakati Man United wanasuasua kwenye Ligi Kuu England wakiwa Nafasi ya 7.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
ROBO FAINALI
Robo Fainali
Jumatano Aprili 2
Real Madrid v Borussia Dortmund
Paris Saint-Germain v Chelsea
Marudiano
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Jumanne Aprili 8
Chelsea v Paris Saint-Germain
Borussia Dortmund v Real Madrid
Jumatano Aprili 9
Bayern Munich v Manchester United
Atletico Madrid v Barcelona
-DROO YA NUSU FAINALI: 11 Aprili
-Mechi kuchezwa 22 & 23 Aprili na Marudiano 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
WASHINDI [Miaka ya karibu]:
MSIMU
MSHINDI
NCHI
MSHINDI WA PILI
NCHI
GOLI
2012-13
Bayern Munich
Germany
Borussia Dortmund
Germany
2-1
2011-12
Chelsea
England
Bayern Munich
Germany
1-1 (4–3)
2010-11
Barcelona
Spain
Manchester United
England
3-1
2009-10
Internazionale
Italy
Bayern Munich
Germany
2-0
2008-09
Barcelona
Spain
Manchester United
England
2-0
2007-08
Man United
England
Chelsea
England
1-1 (6–5)
UEFA CHAMPIONZ LIGI
WAFUNGAJI BORA 2013/14:
C. Ronaldo-Real Madrid Goli 13
Zlatan Ibrahimovic-PSG Goli 10 [Penati 1]
Messi-Barcelona Goli 8 [Penati 2]
Diego Costa-Atletico Madrid Goli 7
Sergio Agüero-Manchester City Goli 6 [Penati 2]

Monday, March 31, 2014

WANACHAMA TFF KUANDALIWA KATIBA MFANO YA MAREKBISHO.

TFF_LOGO12Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF imekutana Machi 30 mwaka huu kujadili utekelezaji wa maagizo ya TFF kwa wanachama wake kurekebisha Katiba zao ili ziendane na Katiba ya TFF pamoja na ile ya FIFA kabla ya Machi 30 mwaka huu.
Vyama vya mikoa Lindi na Dar es Salaam na Chama cha Mpira wa Miguu cha Wanawake (TWFA) viliomba kuongezewa muda wakati vingine vimeomba Katiba mama kama angalizo lao la mabadiliko hayo.  Klabu ya Simba Sports ndiye mwanachama pekee aliyewasilisha mabadiliko ya Katiba.  TFF inawapongeza viongozi na wanachama wa klabu hiyo kwa kufanya mkutano wao kwa utulivu.
Kamati itatangaza nyongeza ya muda wa kufanya mabadiliko hayo baada ya kuviandalia vyama vya mikoa na vyama shiriki katiba mfano kwa ajili ya kurahisisha shughuli hiyo.
Baada ya kupitia uamuzi wa wanachama  wa Simba S.C. Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imeamua ifuatavyo:
(i)           Kwa kuwa pendekezo la wanachama wa Simba kubadili kipengele na 26 kuhusu sifa za mgombea kinapingana na kipengele na 29 (4)  cha Katiba ya TFF, hivyo basi Kamati imeagiza kipengele cha Katiba ya Simba kibaki vilevile bila kubadilishwa.
(ii)         Vipengele vingine vyote vimepitishwa na vitapelekwa kwa Msajili wa Klabu na  Vyama vya Michezo kwa ajili ya kusajiliwa.
(iii)       Mchakato wa uchaguzi wa Klabu ya Simba uendelee kama ulivyopangwa wakizingatia uamuzi huu wa Kamati.  TFF inaitakia Klabu ya Simba uchaguzi mwema.
Pia Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imeshauri TFF kuwasiliana na FIFA kupata mwongozo kuhusu katazo la watu wenye rekodi ya kifungo kugombea.
TFF imepokea ushauri huo na itaufanyia kazi na kama kuna mabadiliko yoyote kiutaratibu yataanzia katika Katiba ya TFF kupitia Mkutano Mkuu.
RAMBIRAMBI MSIBA WA DK HEMED MZIRAY
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha daktari wa tiba ya michezo, Dk. Hemed Mziray kilichotokea juzi jijini Dar es Salaam.
Dk. Mziray ambaye alikuwa mfanyakazi wa Hospitali ya Manispaa ya Temeke na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Tiba ya Michezo Tanzania (TASMA) amesafirishwa kwenda kwao mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.
Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Dk. Mziray ameshirikiana na TFF na wadau wengine wa mpira wa miguu katika masuala ya tiba na uongozi.
Alikuwa kiungo kati ya Uwanja wa Taifa ambapo mechi za kimataifa, za ligi na za kirafiki zimekuwa zikichezwa na Hospitali ya Temeke kwa wagonjwa wanaohitaji huduma zaidi, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Dk. Mziray, TASMA na wafanyakazi wa Hospitali ya Temeke na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Pia TFF inatoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina
MECHI YA AZAM, SIMBA YAINGIZA MIL 26/-
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Azam na Simba iliyochezwa jana (Machi 30 mwaka huu) Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam imeingiza sh. 26,455,000.
Watazamaji 4,741 walikata tiketi kushuhudia pambano hilo ambapo Azam iliibuka na ushindi wa mabao 2-1. Viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.
Mgawanyo kwa mapato ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 4,035,508.47, gharama za kuchapa tiketi sh. 3,908,686 wakati kila klabu ilipata sh. 5,460,687.63.
Uwanja sh. 2,776,620.83, gharama za mechi sh. 1,665,972.50, Bodi ya Ligi sh. 1,665,972.50, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 832,986.25 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 647,878.19.