Thursday, May 15, 2014

TFF YASAINI MKATABA UDHAMINI SOKA LA WANAWAKE

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) hapa nchini limeendeleza kutunisha msuli baada ya jana kusaini mkataba na kampuni ya proin Promotions kwa ajili ya kudhamini mashindano ya Kombe la Taifa kwa wanawake yatakayofanyika kati ya mwezi Septemba na Oktoba mwaka huu.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kampuni hiyo, Johnson Rukaza, alisema kuwa makubaliano hayo waliyoingia na TFF yatakuwa ni ya miaka miwili na yatawagharimu zaidi ya Sh.
 milioni 150 ili kufanikisha michuano hiyoRukaza alisema kuwa kupitia mashindano hayo ya Kombe la Taifa wanaamini vipaji vya wachezaji wanawake vitaonekana na baadaye kuisaidia timu ya Taifa ya jinsia hiyo (Twiga Stars) kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa ambayo inashiriki.
Amesema kwamba wao wamefungua njia kudhamini mashindano hayo na wanawaomba makampuni na taasisi nyingine kujitokeza kudhamini mashindano hayo ikiwamo na vituo vya televisheni lengo likiwa ni kutangaza soka la wanawake.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi, alisema kuwa uongozi wake unawashukuru wadhamini hao wapya na inaahidi uongozi wake utahakikisha soka la wanawake linasonga mbele.
Malinzi amesema kwamba wanawaomba wazazi na walezi kuwaruhusu watoto wa kike kushiriki mchezo huo kwa sababu utawasaidia kiafya, kupata burudani na kuinua hali zao za kichumi pale watakapofanikiwa kupata klabu za kucheza.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Soka la Wanawake Tanzania (TWFA), Lina Kessy, alisema kwamba wanaamini sasa mpira wa wanawake utacheza na jana ilikuwa ni siku ya kihistoria kwenye medani ya mchezo huo kwa upande wa wanawake.
Kessy amesema kwamba TFF na TWFA itahakikisha jitihada za kusaka wadau wengine zinaendelea ili mchezo huo uchezwe sehemu zote hapa nchini.
Amesema kwamba zaidi ya mikoa 17 inatarajiwa kushiriki mashindano hayo ambayo mara ya mwisho yalifanyika mwaka 2008.

Tuesday, May 13, 2014

HASSAN DALALI AWAPA SOMO WANACHAMA WA MSIMBA SC


Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, Hassan Dalali, amewapa somo wanachama wa klabu hiyo kuwa makini katika kuelekea kwenye Uchaguzi huo.
Akizungumzia hilo jijini Dar es Salaam, Dalali alisema kuwa sio wote wanastahili ku
wa viongozi wa klabu hiyo kongwe ambayo kwa sasa imepoteza hadhi yake.
Alisema alipokuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, aliweza kuwaunganisha wana Simba, hivyo kunastahili kiongozi mwingine mwenye mfano wake.
“Hii Simba sasa imepoteza hadhi na heshima yake katika nyanja ya soka, hivyo lazima apatikane kiongozi imara na mwenye uwezo wa kuitumikia usiku na mchana.
“Tunahitaji kupata viongozi makini hivyo siku ya Uchaguzi na wakati huu lazima tuwapime wagombea wote kwasababu tunawajua vizuri,” alisema.
Kwa mujibu wa Dalali, baadhi ya wagombea hawana hadhi na uwezo wa kuwa rais wa kwanza wa klabu hiyo, kutokana na fikra zao kuwa fupi.

MAN UNITED WATOLEA MACHO DIEGO COSTA WENGINE WATAFUATA

KLABU ya Manchester United imepiga hatua katika harakati zake za kusaka za kuimarisha kikosi chake baada ya kwenda kuwatazama Diego Costa na Ander Herrera mwishoni mwa wiki.
Baada ya kutolewa kwenye Kombe la FA na Swansea, kipigo ambacho ni mwendelezo wa msimu mbaya United, kocha David Moyes amesema kwamba kuna jitihada za dhati klabu hiyo ya Old Trafford kusajili wachezaji. 
Amekuwa akisaka beki wa kushoto, kiungo na mshambuliaji Ulaya mzima.
Mlengwa mkuu: Manchester United inataka kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid, Diego Costa
Flying high: Diego Costa and Atletico hit the top of La Liga after beating Malaga 1-0Diego Costa aliiwezesha Atletico kupanda kileleni mwa La Liga baada ya kuifunga Malaga 1-0

Msaka vipaji mkuu wa United, Robbie Cooke alimshuhudia mchezaji wa bei ghali Costa akicheza dakika zote 90 huku Atletico Madrid ikishinda 1-0 dhidi ya Malaga Jumamosi.
Koke – mchezaji ambaye United wamekuwa wakihusishwa naye lakini hawana nia ya kumsajili mwezi huu – alifunga bao pekee kwenymchezo huo.
Cooke alikuwa mmoja wa watu wa benchi la Ufundi walioambatana na Moyes kutua Old Trafford wakitokea Everton na mpango huo ulimfanya asafiri kutoka pwani ya kusini ya Hispania hadi kaskazini mwa San Sebastian, kumuangalia mchezaji wa Atletico Bilbao, Herrara akicheza mechi ya kipigo cha 2-0 kwa Real Sociedad.
Costa, ambaye pia alitakiwa na Liverpool Agosti mwaka jana na hivi karibuni amekuwa akihusishwa na kuhamia Chelsea na Arsenal, amekuwa mmoja wa washambuliaji gumzo Ulaya msimu huu, baada ya kufunga mabao 19 katika mechi 18 na kuisaidia timu yake kuwa mpinzani mkuu wa Barcelona katika mbio za ubingwa wa La Liga.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aliyekataa ofa ya uraia wa Hispania mwaka jana ili aichezee Brazil katika Kombe la Dunia, nchi yake halisi aliyozaliwa, alisaini Mkataba mpya na Atletico ili kumzuia kwenda Liverpool, lakini anaweza kuuzwa kwa Pauni Milioni 31.

DIEGO COSTA KUELEKEA STAMFORD BRIDGE MAPEMA JUNI


Klabu ya Chelsea imekubali kutoa kiasi cha pauni milioni 32 kwa Atletico Madrid kwaajili ya kukamilisha dili la kumsajili mshambuliji mahiri,Diego Costa.
Costa ambaye amekuwa muhimili mkubwa kwa klabu hiyo ya Uhispania ikiwa na uwezo wa kuchukua La Liga na Ligi ya mabingwa barani Ulaya mpaka sasa, amekuwa akihusishwa na kuhamia London huku Jose Mourinho akihitaji mshambuliaji hatari zaidi.
Mourinho alisisitiza mara baada ya mchezo wa mwisho wa ligi kuu ya Uingereza kuwa alikuwa na malengo ya kufanya usajili mkubwa sana Stamford Bridge katika kipindi cha soko la usajili haraka iwezekanavyo.
Dili la Costa halitarajiwi kutangazwa rasmi mpaka ifikapo mapema mwezi Juni mara baada ya michezo miwili mikubwa ambayo nyota huyo anapambana kuweza kuwa fiti kuisaidia timu yake.
Costa alipata majeraha ya misuli na alikosa mchezo waliotoka sare ya 1-1 dhidi ya Malaga Jumapili,mchezo ambao iwapo Atletico wangeshinda wangekuwa
tayari wametwaa taji la La Liga msimu huu.
Atletico watasafiri mpaka Camp Nou kupambana na Barcelona siku ya Jumapili katika mchezo ambao utaamua kombe linaenda wapi na siku saba baadae watakutana na wapinzani wao wa Jiji,Real Madrid kwenye fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya itakayopigwa Lisbon.
Chelsea walimaliza msimu wa 2013/14 katika nafasi ya tatu,pointi nne nyuma ya Manchester City na pointi mbili nyuma ya Liverpool huku rekodi yao ya kufunga magoli ikionekana ndiyo sababu ya kushindwa kwao kupata taji.
Kikosi cha darajani kilifunga magoli 71 ukilinganisha na magoli 102 ya Man City na 101 ya Liverpool na mchezaji mmoja pekee ndiye alikuwa
mhimili ambaye ni kiungo mshambuliaji Eden Hazard akifunga magoli 14.
Samuel Eto’o,Fernando Torres na Demba Ba walifunga jumla ya magoli 19 pekee wote kati yao hivyo kumshawishi Mourinho kutumia pesa nyingi kwaajili ya kupata saini ya mchezaji kama Costa ambaye amefunga magoli 27 kwenye michezo 33 ya La Liga msimu huu.

KOCHA TIM SHERWOOD ATUPIWA VIRAGO SPURS

KOCHA Tim Sherwood amefukuzwa Tottenham Hotspur kiasi cha miezi sita tang aanze kazi White Hart Lane.
Sherwood alirithi mikoba ya Andre Villas-Boas Desemba kwa Mkataba wa miezi 18, lakini ameshindwa kuingia katika msimu wa pili na klabu hiyo.
Tetesi za kuondolewa kwa Sherwood zilianza mwezi uliopita, na hatimaye Mwenyekiti Daniel Levy kutafuta mtu mwingine mwafaka zaidi.
Sherwood ameshinda mechi 14 kati ya 28 akiwa kazini, akitoa safe nne na kufungwa 10, Spurs ikimaliza katika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi, ikizidiwa pointi 10 na Arsenal iliyomaliza nafasi ya nne.
Mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 45 anaweza kupewa ofa mara moja kurejea kurejea klabu ya Daraja la kwanza, Brighton baada ya Oscar Garcia kujiuzulu baada ya kufungwa katika mechi ya Nusu Fainali ya mchujo dhidi ya Derby.

KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS VS ZIMBAMBWE SH. 5,000/-

Mkutano wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na wenyeviti wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kupata maoni yao juu ya changamoto zilizojitokeza katika ligi hiyo umefanyika juzi (Mei 11 mwaka huu).
Klabu za VPL zilizohudhuria mkutano huo n
i Azam, Coastal Union, JKT Ruvu, Mbeya City, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Polisi Morogoro, Ndanda FC, Ruvu Shooting, Stand United na Tanzania Prisons.
Simba na Yanga hazikuhudhuria mkutano huo,na wala klabu hizo hazikutoa udhuru wowote wa kutokuwepo.
Maazimio ya mkutano huo ni kuwa kwa misimu mitatu ijayo kuanzia msimu wa 2014/2015 klabu zimekubaliana ziruhusiwe kusajili wachezaji watano wa kigeni. Kamati ya Utendaji ya TFF itatoa uamuzi wa mwisho juu ya suala hilo katika kikao chake kijacho.
Pia klabu hizo zimekubali timu zao za U20 kuanzia msimu ujao zicheze ligi ya mkondo mmoja. Hata hivyo, utekelezaji wa hilo utategemea na upatikanaji wa mdhamini wa ligi hiyo ambapo TFF inafanya jitihada za kumpata mdhamini huyo.
Vilevile Mwenyekiti wa Kamati ya Mpira wa Miguu wa Wanawake, Lina Kessy amezishauri klabu za VPL kuanzisha timu za wanawake, ambapo klabu hizo zimesema zitaufanyia kazi ushauri huo.

KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS 5,000/-
Kiingilio cha chini cha mechi ya kwanza ya raundi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika 2015 nchini Morocco kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zimbabwe (Mighty Warriors) itakayochezwa Jumapili (Mei 18 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000.
Washabiki watakaolipa kiingilio hicho ni kwa wale watakaokaa kwenye viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. 
Kwa upande wa VIP B na C kiingilio kitakuwa sh. 10,000 wakati kwa VIP A itakuwa ni sh. 20,000.
Tiketi zinatarajiwa kuanza kuuzwa siku moja kabla ya mechi hiyo katika vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam, na uwanja siku ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ikiwa chini ya Kocha Mart Nooij inatarajia kurejea jijini Dar es Slaam kesho (Mei 14 mwaka huu) kutoka Mbeya kuendelea na maandalizi ya kuikabili Zimbabwe.

RAMBIRAMBI MSIBA WA MKUFUNZI KASINDE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Mkufunzi wa waamuzi nchini, Omari Kasinde kilichotokea jana (Mei 12 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Mbali ya kuwa Mkufunzi, Kasinde ambaye anazikwa leo (Mei 13 mwaka huu) mchana katika Makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam pia alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati iliyopita ya Waamuzi ya TFF iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Kapteni mstaafu Stanley Lugenge.
Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu nchini kwani, Kasinde enzi za uhai wake alitoa mchango mkubwa katika mchezo huu tangu akiwa mwamuzi na baadaye mkufunzi na kiongozi..
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Kasinde, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), na Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF

Monday, May 12, 2014

STARS, ZIMBABWE KUUMANA DAR JUMAPILI

Mechi ya kwanza ya raundi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika 2015 nchini Morocco kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zimbabwe (Mighty Warriors) itafanyika Jumapili (Mei 18 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
UWANJA_WA_TAIFA_DAR
Awali mechi hiyo tulipanga ichezwe Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya kwa nia ya kuhakikisha mikoa yote ya Tanzania inapata fursa ya kuwa mwenyeji wa mechi za kimataifa.
Ili Uwanja wa Sokoine uweze kuchezwa mechi za kimataifa za mashindano, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) lilituma Mkaguzi (inspector) wake kwenye uwanja huo Jumamosi (Mei 10 mwaka huu) ambapo imeamua kuwa marekebisho yanayofanyika hayatamalizika katika muda stahili, hivyo mchezo huo kutochezwa Sokoine.
Tunatoa mwito kwa wamiliki wote wa viwanja kuwasiliana na TFF ili Idara ya Ufundi iwaelekeze maboresho ya kufanya ili viwanja vingi iwezekanavyo viweze kukidhi viwango vinavyotakiwa na CAF na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Taifa Stars ambayo ilikuwa kambini mkoani Mbeya itarejea Dar es Salaam keshokutwa (Mei 14 mwaka huu) kujiandaa kwa mechi hiyo.
BONIFACE WAMBURA 
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (T