VICTORIA
UNIVERSITY wamefanikiwa kuwa Mabingwa wa Mashindano mapya ya CECAFA NILE BASIN CUP
baada kuichapa AFC Leopards ya Kenya Bao 2-1 katika Fainali iliyochezwa
huko Khartoum International Stadium Jijini Khartoum Nchini Sudan hapo
Jana.
Haya ni Mashindano ya kwanza kabisa ya
Kombe hilo yaliyoshindaniwa na Klabu kadhaa toka Nchi za Afrika
Mashariki na ya Kati ambao ni Wanachama wa CECAFA.
Kwa ushindi huo, Victoria University pia
wamejinyakulia Donge nono la Dola 30,000 na ni baraka kwa Klabu changa
iliyoshiriki michuano ya CECAFA kwa mara ya kwanza kabisa.
Victoria University ndio waliowatoa
Wawakilishi wa Tanzania Bara, Mbeya City, kwenye Robo Fainali baada ya
kuwafunga Bao 1-0 kwa Bao la Penati.
Kwa kuwa Washindi wa Pili, AFC Leopards walipewa Dola 20,000.
MAGOLI:
Victoria University 2
-Odongo Mathew Dakika ya 29
-Mutyaba Muzamir 90+2
AFC Leopards 1
-Ikene Austin Dakika ya 45
Nao, Timu ya Sudan, Al Shandy, ilinyakua
Dola 10,000 kwa kumaliza Washindi wa Tatu baada ya kuifunga Academie
Tchite ya Burundi Bao 4-1.
Klabu zilizoshiriki muchuano hii ni:
KUNDI A
-Polisi [Zanzibar]
-Victoria University Uganda]
-Malakia [South Sudan]
Al Merreikh [Sdan]
KUNDI B
-Mbeya City [Tanzania Bara]
-AFC Leopards [Kenya]
-Academie Tchite [Burundi]
-Enticelles [Rwanda]
KUNDI C
-Defence [Ethiopia]
-Dkhill FC [Djibouti]
-Al Shandy [Sudan]






