Friday, June 27, 2014
MAXIMO ATAMBULISHWA RASMI YANGA,NA HUU NDIO MKATABA ALIOPEWA
Uongozi wa klabu ya Yanga umemtambulisha rasmi kwa waandishi wa habari Kocha mbrazil Marcio Marcel Maximo kama ndio
kocha atakayeweza kukinoa kikosi cha timu hiyo katika msimu ujao wa Ligi kuu Tanzania Bara.
kocha atakayeweza kukinoa kikosi cha timu hiyo katika msimu ujao wa Ligi kuu Tanzania Bara.
Utambulishwaji huo ulifanywa katika
makao makuu ya Klabu hiyo jijini Dar es salaam na kuuzuliwa na waandishi
wa habari wengi pamoja na wanachama waliokuwa nje kwa ajili ya
kumshuhudia kocha huyo.
Wakala aliyefahamika kwa jina moja la Ally ndiye aliyeweza kufanikisha mipango hiyo ya kumleta maximo.
"nawashukuru wana Yanga kwa uvumilivu wao kwani kwa miaka mitatu sasa nawasiliana na Marcio Maximo "
aliseama Ally na kuongeza kuwa mtazamo wa kocha huyo ni kuinua vipaji
na kuwataka wana Yanga wavumilie na kumpa muda kwa ajili ya kupata
mafanikio.
Naye Maximo amesema kuwa sio rahisi
kuipandisha timu ya Yanga na kupata mafanikio makubwa bali kwa
kushirikiana kila kitu kitafanikiwa.
"Wakati nakuja kwa mara ya kwanza
nilikuwa nasikia Yanga na Simba,lakini niliporejea tena kwa mara ya pili
sasa nasikia Azam, mbeya City na virabu vingine" alisema kocha huyo
huku akikubali kuwa upinzani ni mkubwa.
Kocha Marcio Maximo anaaza
kazi rasmi Siku ya Jumatatu na na atakuwa na msaidizi wake Leonardo
Neiva ambapo watajihusisha sana na Vijana pamoja na timu ya wakubwa.
BRAZIL KOMBE LA DUNIA 2014 HATUA YA 16 BORA DIMBANI KESHO.
Michuano ya Kombe la Dunia huko Brazil sasa zimeingia Hatua ya Mtoano na zipo Timu 16 zinazowania kutinga Robo Fainali.
KOMBE LA DUNIA
RAUNDI YA PILI YA MTOANO
Saa za Bongo
JUMAMOSI, JUNI 28, 2014 |
|||||
SAA |
MECHI NA |
MECHI |
UWANJA |
MJI |
|
19:00 usiku |
49 |
Brazil v Chile |
Mineirão |
Belo Horizonte |
|
23:00 usiku |
50 |
Colombia v Uruguay |
Maracanã |
Rio de Janeiro |
|
JUMAPILI, JUNI 29, 2014 |
|||||
SAA |
MECHI NA |
MECHI |
UWANJA |
MJI |
|
19:00 usiku |
51 |
Netherlands v Mexico |
Castelao |
Fortaleza |
|
23:00 usiku |
52 |
Costa Rica v Greece |
Pernambuco |
Recife |
|
JUMATATU, JUNI 30, 2014 |
|||||
SAA |
MECHI NA |
MECHI |
UWANJA |
MJI |
|
19:00 usiku |
53 |
France v Nigeria |
Nacional |
Brasilia |
|
23:00 usiku |
54 |
Germany v Algeria |
Beira-Rio |
Porto Alegre |
|
JUMANNE, JULAI 1, 2014 |
|||||
SAA |
MECHI NA |
MECHI |
UWANJA |
MJI |
|
19:00 usiku |
55 |
Argentina v Switzerland |
Corinthians |
Sao Paulo |
|
23;00 usiku |
56 |
Belgium v USA |
Fonte Nova
|
Salvador |
Sunday, June 15, 2014
STARS KWENDA BOTSWANA JUNI 24 KUJIWINDA DHIDI YA MSUMBIJI.
Wachezaji wote wa Taifa Stars waliruhusiwa kurejea makwao jana kwa ajili ya kujiandaa na safari hiyo na watakutana tena kesho.
Stars
inayofundishwa na Mholanzi, Mart Nooij itaondoka nchini Juni 27 kwenda
Gaborone, ambako itaweka kambi ya mazoezi hadi Julai 7 itakaporejea
nchini.
Taifa Stars itamenyana na Msumbiji ‘Mambas’ katika hatua ya mwisho ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani nchini Morocco baada ya kuitoa Zimbabwe juzi kwa jumla ya mabao 3-2, ikianza kwa ushindi wa 1-0 nyumbani na kumaliza kwa sare ya 2-2 juzi mjini hapa.
Mechi yake kwanza itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kati ya Julai 19 na 20 mwaka huu, wakati mechi ya marudiano itafanyika Msumbiji kati ya Agosti 2 na 3 mwaka huu.
Stars pia inatarajiwa kuwa na mchezo wa kujipima nguvu na Uganda kabla ya kumenyana na Msumbiji.
Taifa Stars itamenyana na Msumbiji ‘Mambas’ katika hatua ya mwisho ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani nchini Morocco baada ya kuitoa Zimbabwe juzi kwa jumla ya mabao 3-2, ikianza kwa ushindi wa 1-0 nyumbani na kumaliza kwa sare ya 2-2 juzi mjini hapa.
Mechi yake kwanza itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kati ya Julai 19 na 20 mwaka huu, wakati mechi ya marudiano itafanyika Msumbiji kati ya Agosti 2 na 3 mwaka huu.
Stars pia inatarajiwa kuwa na mchezo wa kujipima nguvu na Uganda kabla ya kumenyana na Msumbiji.
TFF YASIMAMISHA UCHAGUZI SIMBA YAITAKA UENDE KAMATI YA MAADILI.

Uchaguzi
Mkuu Simba ulipangwa kufanyika Juni 29 na uamuzi huu wa TFF uliotangazwa Leo
kwenye Mkutano wake na Wanahabari unaitaka Simba kuunda Kamati ya Maadili
ifikapo Juni 30 na Kamati hiyo ndio itakayoshughulikia masuala yote ya Maadili
kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu.
Uamuzi
huu wa TFF unaendelea kumweka Madarakani Mheshimiwa Ismail Aden Rage hadi hapo
Uchaguzi utakapofanyika baada ya Katiba yao kurekebishwa na kujumuisha Kamati
ya Maadili.
Uchaguzi
wa Simba umekumbwa na vuta nikuvute Klabuni hasa baada ya Mgombea Michael
Wambura kuenguliwa kugombea Urais na Kamati ya Uchaguzi ya Simba na yeye kukata
Rufaa TFF ambako Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, chini ya Mwenyekiti wake
Wakili Julius Lugaziya, ilimpitisha na kuamua aruhusiwe kugombea.
Hivi
karibuni, Yanga walipitisha uundwaji wa Kamati ya Maadili ya Klabu yao ili
kutii amri ya TFF kwenye Mkutano Mkuu wao huko Bwalo la Polisi –Oysterbay,
Jijini Dar es Salaam.
Lakini
hatua hiyo ililazimu Mkutano huo kumwongezea muda wa Mwaka mmoja Mwenyekiti wa
Klabu hiyo, Yusuf Manji, ili aweze kukamilisha masuala ya marekebisho ya Katiba
yao na kujumuisha Kamati ya Maadili na pia kuweza kuandaa Mkutano wa Uchaguzi
baada ya Katiba mpya kupitishwa na TFF.
Saturday, June 7, 2014
MASHABIKI WA YANGA MBEYA WAUTAKA UONGOZI WA YANGA KUMUELEZA MAXIMO KUZIBA PENGO LA KAVUMBAGU

Wakizungumza na mtandano wa mkali wa dimba kupitia sayari ya michezo wamesema kuwa kutokana habari zilizo tolewa katika Mkutano Mkuu wa marekebisho ya baadhi ya vipengele kwenye Katiba ya Yanga umefanyika na kumalizika salama na furaha kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi -Oysterbay huku wanachama wakipitisha kipengele cha kuundwa kwa kamati ya maadili.
katika kikao cha
wanachama wa club ya yanga kilicho fanyika Juni 1 mwaka huu uongozi wa yanga
Ulimtangaza kuwa Maximo kama kocha anayetarajiwa kuinoa Yanga.
Wamesema kuwa Maximo anatakiwa kutazama mchezaji sahihi atakae ziba pengo la mshambuliaji Didier Kavumbagu kwa ajili ya kuunda upya timu hiyo licha ya kuwa na Wachezaji wengi katika safu ya Ushambuliaji.
Kwa mujibu wa chanzo
cha karibu kutoka ndani ya yanga Taarifa zinasema mazungumzo na Kocha Maximo
yamefikia sehemu nzuri kwa ajili ya kuja Tanzania kuinoa Yanga SC.
TFF YATOA RAMBIRAMBI MISIBA YA KANALI MWANAKATWE NA GEBO PETER!
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha
aliyekuwa Katibu Mkuu wake (wakati huo ikiitwa FAT), Kanali mstaafu Ali
Hassan Mwanakatwe kilichotokea leo asubuhi (Juni 7 mwaka huu) katika
Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa binti wa marehemu, Sophia,
baba yake alianguka bafuni nyumbani kwake Mbezi Beach ambapo
alikimbizwa katika Hospitali ya Lugalo ambapo ndipo umauti ulipomfika
wakati madaktari wakimpatia matibabu.
Kanali Mwanakatwe alichaguliwa kuwa
Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) katika uchaguzi
uliofanyika mwaka 1993 mjini Kibaha mkoani Pwani.
Baada ya kuondoka FAT, aligombea nafasi
ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA)
na kufanikiwa kushinda katika uchaguzi uliofanyika mwaka 1997.
Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira
wa miguu nchini na Afrika kwa ujumla kwani, Kanali Mwanakatwen enzi za
uhai wake alitoa mchango mkubwa akiwa kiongozi, na mkufunzi wa utawala
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Pia aliwahi kuwa Kamishna
wa CAF.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu
Kanali Mwanakatwe, DRFA, na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na
kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha
msiba huo mzito.
Taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa
na familia yake nyumbani kwake Mbezi Beach karibu na hoteli ya Giraffe
wakati ndugu wakisubiriwa kutoka mikoani. TFF tunasubiri taratibu hizo
ili tujipange jinsi ya kushiriki katika msiba huo.
Sisi sote ni waja wake Mola. Hakika kwake tutarejea.
Subscribe to:
Posts (Atom)