Baadhi ya wanachama
wa Simba walienda mahakama kuu wakihitaji chombo hicho cha dola kusimamisha uchaguzi
wa Simba unaotarajia kufanyika juni 29 mwa
ka huu.
ka huu.
Sababu ya wanachama
hao ilikuwa ni kupinga maamuzi ya kamati ya uchaguzi ya Simba, chini ya
mwenyekiti wake, Wakili Damas Daniel Ndumbaro, kuliengua jina la aliyekuwa
mgombe wa Urais, Michael Wambura kwa mara ya pili.
Hata hivyo, suala la
wanachama kupelekea suala la michezo katika mahakama ya kawaida ilikuwa ni
hatari zaidi kwa klabu ya Simba kwasababu sheria za mpira ziko wazi na
hairuhusiwi kupeleka mambo ya mpira mahakama za dola.
FIFA wanataka masuala
ya mpira yasuluhishwe katika mifumo yake ya haki na si vinginevyo.
Kupeleka mambo ya
mpira mahakama za kawaida ilikuwa moja ya sababu iliyokuwa na nguvu kumuengua
Wambura kwa mara ya kwanza.
Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa
vyombo vya habari na katibu mkuu wa Simba, Kamwaga jioni ya leo imesema kamati
ya Uchaguzi ya Simba SC imesema kuwa inapenda kuwaalika wanachama wote wa Simba
katika Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Klabu uliopangwa kufanyika Keshokutwa
Jumapili, Juni 29 mwaka huu, katika Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi,
Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Kamwaga alifafanua kuwa katika uchaguzi huo, jumla
ya wagombea 27 wanatarajiwa kushiriki na Kamati ya Uchaguzi imeazimia kwamba
suala la muda litazingatiwa sana safari hii kutokana na ukweli wa kuwepo kwa
wagombea wengi.


