Saturday, November 1, 2014

TANZANIA NA BURUNDI ZA SAINI MKATABA WA MIAKA 50 KUSAFIRISHA UMEME.

SERIKALI ya Tanzania na Burundi zimesaini mkataba wa miaka 50 wamakubaliano wa mradi wa pili wa kusafirisha umeme utakaozalishwa kwenye kituo cha Rusumo.
Awali Tanzania, Burundi na Rwanda zilisaini mkataba wa kwanza wa mradi wa kituo cha kuzalisha umeme cha rusumo chenye mega watt 80, kilichopo wilayani Ngara, Mkoani Kagera, mwaka 2013 ambacho kiligharimu takribani dola za kimarekani milioni 340 zilizotolewa na benki ya Dunia.
Akizungumza Dar es Salaam jana baada ya kusaini mkataba huo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa, Sospeter Muhongo, alisema mkataba huo umezihusisha nchi mbili ambapo alibainisha kuwa kupitia mradi huo ambao umeanza katika sehemu ya mwisho ya kutekeleza mradi wa kwanza ulioanza mwaka jana yapo baadhi ya maeneo nchini yatapata umeme.

Alisema kupitia mradi huo nchi itaweza kuimarisha grid ya Taifa na kupunguza tatizo la umeme kwenye maeneo mengi nchini.
Waziri Muhongo aliongeza kuwa pamoja na hatua hiyo pia kuitia mradi huo utaajiri wafanyakazi kutoka nchi zote tatu na hata wa mataifa mwengine ambapo alibainisha kuwa kwa sasa katika kituo cha mto rusumo wapo walioajiriwa kutoka nchi husika na miradi hiyo na mataifa mengine.

Kuhusu ujenzi wa mfumo wa usafirishaji umeme alisema kila nchi itajitegemea katika kusafirisha umeme na kubainisha kuwa Tanzania itajenga mfumo huo kuanzia miaka michache ijayo.

Hata hivyo Prof. Muhongo hakubainisha kiasi halisi kitakacho tumika kuendeshea mradi huo wa wamu ya pili

VPL:AZAM FC, YANGA ZAPIGWA KIMOJA, SIMBA YALE YALE.

MATOKEO:
Jumamosi Novemba 1
Kagera Sugar 0 Yanga 1
Coastal Union 1 Ruvu Shooting 0
Ndanda FC 1 Azam FC 0
Mtibwa Sugar 1 Simba 1
JKT Ruvu 1 Polisi Moro 2
Stand United 0 Prisons 1

MABINGWA wa Ligi Kuu Vodacom Azam FC Leo Wameambua kipigo cha pili mfululizo baada kuchalazwa1-0 na Ndanda FC huko Nangwanda, Mtwara.
Wikiendi iliyopita, Azam FC, wakiwa kwao Azam Complex, walichapwa 1-0 na Ruvu JKT.

Huko Kaitaba, Bukoba, Kager Sugar iliifunga Yanga Bao 1-0 kwa Bao la Paul Ngway la Dakika ya 52 na Yanga kumaliza Mechi hii wakiwa Mtu 10 baada Nahodha wao, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu kwa tuhuma za kucheza vibaya.
Nao Simba wameendeleza mwendo wao ule ule wa kutoka Sare Mechi zao zote za Ligi Msimu huu baada ya kutoka 1-1 na Mtibwa Sugar huko Jamhuri, Morogoro.
Simba walitangulia kufunga Dakika ya 35 kwa Bao la Kichwa la Joseph Owino na Mchezaji wa zamani wa Simba, Mussa Hassan Mgosi, kuiswazishia Mtibwa kwenye Dakika ya 58.
Huko Mkwakwani, Tanga, Coastal Union waliichapa Ruvu Shooting Bao 1-0 na kuchupa hadi Nafasi ya Pili.
Ligi hii inaendelea hapo Kesho huko Mkwkwani Tanga kwa Mechi kati ya Mgambo JKT v Mbeya City.

Wednesday, October 15, 2014

SIMBA YAENDELEA KUPOKEA KIPONDO BONDENI AFRICA YA KUSINI 2-0 DHIDI YA JOMO COSMOS

Wekundu wa Msimbazi Simba Sc imekamilisha mechi zake za kirafiki za kujipima nguvu katika kambi yake ya Afrika kwa kufungwa mabao 2-0 na Jomo Cosmos mjini Johannesburg jioni hii.

Pamoja na kufungwa na timu hiyo ya Daraja la Kwanza, inayomilikiwa na kufundishwa na gwiji wa soka Afrika Kusini, Jomo ‘Black Prince’ Sono, Simba SC ilicheza soka ya kuvutia.

katika kambi hiyo huo ni mtanange wa tatu kwa Simba SC katika kambi yake ya Afrika Kusini tangu iwasili Oktoba 8, mwaka huu kwa ajili ya maandalizi ya mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya mahasimu wao, Yanga SC Jumamosi wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Katika mchezo wake wa kwanza, Simba SC ililazimishwa sare ya bila kufungana na Orlando Pirates kabla ya kufungwa mabao 4-2 na Bidvest Wits, au Wits University.
Simba SC itaendelea na mazoezi kesho na inatarajiwa kurejea Dar es Salaam Ijumaa tayari kwa mchezo wa Jumamosi, unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini.

TAARIFA KUTOKA TFFUCHAGUZI MDOGO TPLB NOVEMBA 15

Mkutano Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) utafanyika Novemba 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo moja ya ajenda ni uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi moja ya uongozi kwenye bodi hiyo.
Nafasi hiyo ya ujumbe kwenye Kamati ya Uendeshaji ya TPLB iliyokuwa ikishikiliwa na Kazimoto Muzo imebaki wazi baada ya klabu yake ya Pamba ya Mwanza kushuka daraja kutoka la Kwanza hadi la Pili.
Hivyo, wagombea wa nafasi hiyo ni kutoka kwenye klabu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL). Klabu hizo zina nafasi mbili kwenye Kamati ya Uendeshaji ya TPLB ambapo nyingine inashikiliwa na Omari Mwindadi wa klabu ya Mwadui ya Shinyanga.

SDL WAONGEZEWA MUDA WA USAJILI
indexShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeongeza muda wa usajili wa wachezaji kwa timu za Ligi Daraja la Pili (SDL) kwa siku saba ambapo sasa utamalizika Oktoba 21 mwaka huu.
Awali usajili huo unaofanyika kwa njia ya mtandao (online) ulikuwa umalizike jana (Oktoba 14 mwaka huu), lakini ni klabu chache ndizo zilizoweza kusajili ndani ya muda uliopangwa.
Klabu ambazo hazijakamilisha shughuli hiyo ya usajili, zinatakuwa kukamilisha ndani ya siku hizo saba kwani TFF haitaongeza tena muda wa usajili. Vilevile klabu za SDL zinakumbushwa kuwasilisha majina ya viwanja vya nyumbani ambavyo timu zao zitatumia kwenye ligi hiyo.
TFF ilifanya mafunzo ya usajili kwa maofisa usajili wa klabu hizo Oktoba 6 na 7 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Timu za SDL zimegawanywa katika makundi manne ya timu sita zitakazocheza ligi kwa mtindo wa nyumbani na ugenini. Kundi A lina timu za Mpanda United ya Katavi, Ujenzi (Rukwa), Mvuvumwa FC (Kigoma), Mji Mkuu FC (Dodoma), Milambo (Tabora) na Singida United (Singida).
Kundi B ni Mbao FC (Mwanza), Bulyanhulu FC (Shinyanga), Eleven Stars (Kagera), JKT Rwamkoma (Mara), Pamba (Mwanza) na AFC (Arusha). Kundi C ni Navy, Mshikamano, Transit Camp na Abajalo za Dar es Salaam, Kiluvya United (Pwani) na Kariakoo (Lindi(.
Timu zinazounda kundi D ni Magereza (Iringa), Town Small Boys (Ruvuma), Njombe Mji (Njombe), Volcano FC (Morogoro), Wenda FC (Mbeya) na Mkamba Rangers (Morogoro).
MAREKEBISHO YA RATIBA FDL KUNDI A
Mechi nne za Kundi A la Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zimefanyiwa marekebisho ili kutoa fursa ya matumizi ya Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam.
Timu za African Lyon na Kimondo FC ambazo awali zilikuwa zicheze Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, sasa zitacheza Oktoba 26 mwaka huu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Nayo mechi ya Polisi Dar es Salaam na Majimaji ya Songea iliyokuwa ichezwe Oktoba 26 mwaka huu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, sasa itachezwa Oktoba 27 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.
Mechi ya Friends Rangers na Ashanti United iliyokuwa ichezwe Mabatini mkoani Pwani, Oktoba 26 mwaka huu, sasa itachezwa Uwanja wa Karume, Oktoba 28 mwaka huu.
Pia
 mechi ya Lipuli FC na JKT Mlale iliyokuwa ichezwe Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa, imesogezwa mbele kwa siku moja. Mechi hiyo sasa itachezwa Oktoba 26 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Tuesday, October 14, 2014

SIMBA KESHO KUONYESHANA KAZI NA JOMO COSMOS THN KURUDI DAR

Timu ya simba wekundu wa MSimba kesho inataraji kushuka dimba kupapatuana katika mechi yake ya mwisho ya kirafiki kesho dhidi ya Jomo Cosmos.

Mechi hiyo itapigwa jijini Johannesburg na baada ya hapo Simba itaanza safari ya kurejea jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi dhidi ya watani wake Yanga, Oktoba 18.
Wekundu hao tayari Simba wamecheza mechi mbili za kirafiki, dhidi ya Orlando Pirates ambayo ilitoka sare ya ya bila kufungana kabla ya kupata kipigo cha mabao 4-2 kutoka kwa Wits.

Wakati huo huo Katibu Mkuu wa zamani wa Simba, Kassim Dewji amewataka mashabiki wa Msimbazi kutotegemea mambo makubwa sana katika mechi yao ya Oktoba 18 dhidi ya Yanga.

Dewji ambaye yuko Johannesburg, Afrika Kusini ambako kikosi cha Simba kimeweka kambi, amesema bado kuna mambo mengi yanapaswa kubadilishwa.

KIINGILIO MECHI YA WATANI WA JADI YANGA NA SIMBA 7,000/-

Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Yanga na Simba itakayochezwa Jumamosi (Oktoba 18 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 7,000.

KUIONA SIMBA VS YANGA KIINGILIO KINAANZIA 7000
Washabiki watakaolipa kiingilio hicho ni wale watakaokaa viti vya rangi ya bluu na kijani ambavyo jumla yake ni 36,693 katika uwanja huo wenye viti 57,558. Viingilio vingine ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 kwa VIP B na C wakati VIP A itakuwa sh. 30,000.


Tiketi zitakazotumika kwenye mechi hiyo ni za elektroniki, na zimeanza kuuzwa jana (Oktoba 13 mwaka huu). Tiketi zinapatikana kwa mtandao wa M-PESA, CRDB Simbanking na maduka ya CRDB Fahari Huduma ambayo yapo zaidi ya mia moja sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Mechi hiyo namba 27 itakayochezeshwa na mwamuzi Israel Mujuni Nkongo akisaidiwa na John Kanyenye na Ferdinand Chacha itaanza saa 10 kamili jioni. Kamishna wa mechi hiyo ni Salum Kikwamba kutoka mkoani Kilimanjaro.

Washabiki wanatakiwa kununua tiketi mapema, kwani hazitauzwa uwanjani siku ya mechi. Milango yote ukiwemo ule wa upande wa Mbagala (Uwanja wa Ndani) itafunguliwa kwa ajili ya washabiki, na itakuwa wazi kuanzia saa 4 asubuhi.


Magari maalumu tu yenye stika ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia uwanjani kwa kupitia Barabara ya Mandela. Pia washabiki hawaruhusiwi kuingia uwanjani wakiwa na silaha, vitu vya vyuma na mabegi makubwa. Barabara ya kuingilia upande wa Chang’ombe itafungwa kwa watumiaji wa magari.