Monday, March 24, 2014

EL_CLASSICO-MACHI_23WAKALI wa Spain, Real Madrid na Barcelona, walishuka Jana Usiku katika dimba la uwanja Estadio Santiago Bernabeu naBarcelona kuibuka kidedea kwa Bao 4-3 huku Lionel Messi akipiga Hetitriki, Penati 3 zikifungwa na, kama kawaida, Kadi Nyekundu kwa Sergio Ramos.
MAGOLI:
Real Madrid 3
-Dakika ya 20 & 24  Karim Benzema
-Dakika ya 55 Ronaldo [Penati]
FC Barcelona 4
-Dakika ya 7  Andres Iniesta
-Dakika ya 42, 65 & 84 Lionel Messi [Penati 2]
Licha ya ushindi huo, Atletico Madrid ndio wako kileleni wkifuatiwa na Real Madrid na Barca wapo Nafasi ya 3, Pointi 1 nyuma ya Real na Atletico.
Huko Spain, Timu zikifungana Pointi, kinachohesabiwa ni Matokeo ya Mechi zao, Uso kwa Uso, ni si Magoli na kama hilo litafungana ndio Magoli huhesabiwa.
LA LIGA
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Atletico de Madrid
29
22
4
3
66
21
45
70
2
Real Madrid CF
29
22
4
3
80
30
50
70
3
FC Barcelona
29
22
3
4
85
25
60
69
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Barca ndio waliotangulia kufunga kwa Bao la Iniesta na Real kujibu kwa Bao mbili za Karim Benzema na kisha Messi akasawazisha na Gemu kuwa 2-2 hadi Haftaimu.
Ndipo Kipindi cha Pili zikaja Penati 3, nyingine za utata, wakati Ronaldo alipofunga Bao la 3 kwa Penati, Messi kusawazisha kwa Penati na kisha kufunga Bao la ushindi kwa Penati zikiwa zimebaki Dakika 6.
VIKOSI:
REAL MADRID [Mfumo: 4-3-3]:
Lopez,
Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo;
Xabi Alonso, Luka Modric, Di Maria
Gareth Bale, Karim Benzema, Cristiano Ronaldo,
Akiba: Casillas,  Varane, Fábio Coentrão, Nacho, Morata,  Isco,  Illarramendi
BARCELONA [Mfumo: 4-3-3]:
Valdes,
Jordi Alba, Pique,Mascherano, Alves
Xavi, Iniesta, Busquets,
Messi, Neymar, Fabregas,
Akiba: Pedro, Sánchez, Pinto Colorado, Bartra, Song, Adriano, Sergi
Refa:  Alberto Undiano Mallenco
WATAZAMAJI: 85,454
LA LIGA
Uso kwa Uso
26/10/13, 18:00 FC Barcelona 2-1 Real Madrid
02/03/13, 16:00 Real Madrid 2-1 FC Barcelona
07/10/12, 19:50 FC Barcelona 2-2 Real Madrid
21/04/12, 20:00 FC Barcelona 1-2 Real Madrid
10/12/11, 22:00 Real Madrid 1-3 FC Barcelona
16/04/11, 22:00 Real Madrid 1-1 FC Barcelona
29/11/10, 21:00 FC Barcelona 5-0 Real Madrid
10/04/10, 22:00 Real Madrid 0-2 FC Barcelona
29/11/09, 19:00 FC Barcelona 1-0 Real Madrid
02/05/09, 20:00 Real Madrid 2-6 FC Barcelona
13/12/08, 22:00 FC Barcelona 2-0 Real Madrid
07/05/08, 22:00 Real Madrid 4-1 FC Barcelona
23/12/07, 19:00 FC Barcelona 0-1 Real Madrid
10/03/07, 22:00 FC Barcelona 3-3 Real Madrid
22/10/06, 21:00 Real Madrid 2-0 FC Barcelona
01/04/06, 22:00 FC Barcelona 1-1 Real Madrid
19/11/05, 20:00 Real Madrid 0-3 FC Barcelona
10/04/05, 19:00 Real Madrid 4-2 FC Barcelona
20/11/04, 22:00 FC Barcelona 3-0 Real Madrid
25/04/04, 19:30 Real Madrid 1-2 FC Barcelona

Friday, March 21, 2014

MAN UNITED YAPANGWA NA BAYERN MUNICH ROBO FAINALI CHAMPIONS LEAGUE


Mechi za Robo Fainali kuchezwa Apirili 1 & 2, Marudiano Aprili 8 & 9
Droo ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI iimefanyika huko Nyon, Uswisi na Mabingwa Watetezi Bayern Munich watakutana na Mabingwa wa England, Manchester United, na Mechi ya Kwanza kuchezwa Old Trafford Aprili 1 au 2.
Chelsea watakuwa Ugenin kucheza na Paris Saint-Germain.
Barcelona wataanza kwao Nou Camp kwa kucheza na wenzao wa Spain Atletico Madrid.
Real Madrid wataanza Nyumbani Santiago Bernabeu kwa kucheza na Klabu ya Germany Borussia Dortmund.
Mechi za Marudiano zitachezwa Wiki moja baadae.
Barcelona v Atletico Madrid
Real Madrid v Borussia Dortmund
Paris St Germain v Chelsea
Manchester United v Bayern Munich
Mechi kuchezwa April 1/2 and April 8/9

VPL, LIGI KUU VODACOM YANGA KUIKABILI RHINO YA TABORA


YANGA, RHINO KUCHEZA TABORA VPL
Yanga inaumana na Rhino Rangers katika moja kati ya mechi mbili za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitakazochezwa wikiendi hii katika miji miwili tofauti.
Mechi hiyo itafanyika kesho (Machi 22 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, mjini Tabora ambapo kiingilio kitakuwa sh. 5,000 kwa jukwaa kuu na sh. 3,000 mzunguko.
Nayo JKT Ruvu itakuwa mwenyeji wa Mbeya City katika mechi itakayochezwa kesho Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Jumapili) kwa mechi nne ambapo Simba itacheza na Coastal Union katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Azam itaoneshana kazi na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Azam Complex. Mechi hizo mbili zitakuwa ‘live’ kupitia Azam Tv.
Mechi nyingine za Jumapili ni Mgambo Shooting dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, wakati Ruvu Shooting na Ashanti United zitapimana ubavu kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Azam FC
20
12
8
0
27
44
2
Yanga SC
19
11
7
1
29
40
3
Mbeya City
21
10
9
2
10
39
4
Simba SC
21
9
9
3
17
36
5
Kagera Sugar
21
8
8
5
3
32
6
Ruvu Shooting
20
7
7
6
-4
28
7
Coastal Union
21
5
11
5
1
26
8
Mtibwa Sugar
21
6
8
7
-1
26
9
JKT Ruvu
21
8
1
12
-13
25
10
Prisons FC
20
3
10
7
-4
19
11
Mgambo JKT
20
4
6
10
-17
18
12
Ashanti United
21
4
6
11
-18
18
13
JKT Oljoro
21
2
9
10
-16
15
14
Rhino Rangers
21
2
7
12
-14
13
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano Machi 26
Mgambo JKT v Azam FC
Yanga v Tanzania Prisons
Jumamosi Machi 29
Ashanti United v JKT Oljoro
Jumapili Machi 30
Mbeya City v Tanzania Prisons
Kagera Sugar v Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar v Coastal Union
JKT Ruvu v Rhino Rangers
Azam FC v Simba
Mgambo JKT v Yanga
KIKOSI KAZI KUSHUGHULIKIA TIKETI ZA ELEKTRONIKI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na benki ya CRDB zimeunda kikosi kazi (task force) kwa ajili ya kushughulikia matumizi ya tiketi za elektroniki ambayo yalisimamishwa kutoka na changamoto mbalimbali zilizokuwa zimejitokeza.
TFF na CRDB zimefanya kikao cha pamoja jana (Machi 20 mwaka huu) kuhusu masuala ya tiketi za elektroniki na kukubaliana kuunda kikosi kazi hicho kwa ajili ya uboreshaji matumizi ya mfumo huo.
Kikosi kazi hicho kitakuwa na wajumbe kutoka TFF na CRDB. Kwa upande wa TFF wajumbe wake ni Mkurugenzi wa Sheria na Uanachama, Evodius Mtawala, Ofisa Habari na Mawasiliano, Boniface Wambura na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Silas Mwakibinga.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi ametoa shukrani za kipekee kwa Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dr. Charles Kimei ambaye alihudhuria binafsi kwenye kikao akiongoza timu yake.
Malinzi amesema ni imani ya TFF kuwa mfumo wa tiketi za elektroniki ndiyo mkombozi wa ulinzi wa mapato milangoni, na anaamini kwa pamoja TFF na CRDB zitafanikisha matumizi hayo ya tiketi za elektroniki.

Thursday, March 20, 2014

CAF CHAMPIONZ LIGI: RAUNDI YA MTOANO TIMU 16 MOTO IJUMAA

Michuano Mikubwa ya Klabu Barani Afrika, CAF CHAMPIONZ LIGI, Ijumaa yanaingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ili kupata Timu 8 ambazo zitaingia kwenye Droo kupanga Makundi mawili ya Timu 4 kila moja.
Mabingwa Watetezi, Al Ahly ya Misri, ambao Raundi iliyopita waliwatoa Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga, kwa Mikwaju ya Penati baada kwenda Sare ya Jumla ya Bao 1-1 katika Mechi mbili, wataanza kucheza Ugenini huko Libya na Klabu ya Al Ahli – Benghazi.
Nao TP Mazembe ya Congo DR, Klabu yenye Mastraika wawili Mashujaa wa Tanzania, Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta, itakuwa Ugenini huko Ivory Coast kucheza na Sewe Sport.
Mechi nyingine zenye mvuto ni ile kati ya Nkana FC ya Zambia na Magwiji wa Egypt, Al Zamalek itakayochezwa huko Zambia..
Klabu nyingine ya Congo DR ni AS Vita ambayo itakuwa Nyumbani kucheza na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.
Marudiano ya Mechi ya Raundi hii ni Wikiendi ya Machi 28.
CAF CHAMPIONZ LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
[Saa za Bongo]
Ijumaa Machi 21
16:00 Al Ahli - Benghazi – Libya v Al Ahly - Egypt     
16:00 Nkana FC – Zambia v Al Zamalek - Egypt
19:30 AS Bamako – Mali v Espérance Sportive de Tunis – Tunisia
Jumapili Machi 23
16:30 AS Vita Club - Congo, DR v Kaizer Chiefs - South Africa
16:50 AC Leopards de Dolisie – Congo v Al-Hilal - Sudan
19:00 Sewe Sport - Ivory Coast v TP Mazembe - Congo, DR
19:30 Horoya Athlétique Club – Guinea v Club Sportif Sfaxien - Tunisia
21:15 Entente Sportive de Sétif - Algeria v Coton Sport FC - Cameroon

Wednesday, March 19, 2014

CHELSEA YAIZIBUA GALATASARAY 2-MTUNGI.

Club ya soka ya Chelsea imefanikiwa kuichalaza Timu ya  Galataray ya Uturuki kwa mabao 2-0 katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwenye UWanja wa Stamford Bridge London.

Mabao ya Chelsea yaliwekwa kimiani  na Samuel Eto’o na beki Garry Cahill na kuipa Chelsea ushindi wa jumla ya mabao 3-1 baada ya kutoka sare ya bao 1-1 jijini Istambul katika mechi ya kwanza.
UEFA CHAMPIONZ LIGI

Raundi ya Mtoano ya Timu 16

MARUDIANO MATOKEO.

Jumanne Machi 18

Chelsea FC 2 Galatasaray Spor Kulübü 0 [3-1]

Real Madrid CF 3 Schalke 1 [9-2]

RATIBA MECHI ZA LEO:

Jumatano Machi 19

22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg [4-2]

22:45Man United v Olympiacos CFP [0-2].

Tuesday, March 18, 2014

DROGBA KUFUMUA NYASI STAMFORD BRIDGE.

Mshambuliaji Mahiri wa Galatasaray ya Uturuki, akiwa na wenzake amefanya mazoezi kwenye Uwanja wa Stamford Bridge unaotumiwa na Chelsea. 
Mara tu baada ya mazoezi, Drogba amesema yuko tayari kwa ajili ya mechi ya leo dhidi ya kikosi hicho cha Jose Mourinho katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
"Nimerudi tena hapa, kwangu ni sehemu bora na yenye kumbukumbu nyingi sana. Lakini kama ni mechi, niko tayari," alisema Drogba.
Katika mechi ya kwanza jijini Istambul, timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1. Hivyo jibu litatapikana leo.
UEFA CHAMPIONZ LIGI

Raundi ya Mtoano ya Timu 16

RATIBA

MARUDIANO

[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]

[Saa za Bongo]

Jumanne Machi 18

22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü [1-1]

22:45 Real Madrid CF v Schalke 04 [1-6]

Jumatano Machi 19

22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg [4-2]

22:45 Manchester United v Olympiacos CFP [0-2]

31 WAITWA NGORONGORO HEROES KUIKABILI KENYA.

Wachezaji 31 wameteuliwa kujiunga na timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) kwa ajili ya michuano ya Afrika ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Senegal.
Ngorongoro Heroes itakayokuwa chini ya Kaimu Kocha John Simkoko akisaidiwa na Mohamed Ayoub inaingia kambini kesho (Machi 19 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa mechi ya kwanza dhidi ya Kenya itakayochezwa kati ya Aprili 4-6 jijini Nairobi.
Kikosi kinachounda timu hiyo ambayo itarudiana na Kenya kati ya Aprili 25-27 mwaka huu jijini Dar es Salaam kinajumuisha pia baadhi ya wachezaji walioonekana katika mpango wa ung’amuzi wa vipaji kwa ajili ya maboresho ya Taifa Stars.
Wachezaji walioitwa ni makipa Aishi Manula (Azam), Hamad Juma Hamad (Scouting- Temeke), Manyika Peter Manyika (Scouting- Ilala) na Mwinyi Hassan Hamisi (Mtende, Zanzibar).
Mabeki wa pembeni ni Ayoub Semtawa (Coastal Union), Edward Charles (JKT Ruvu), Frank Linus Makungu (Scouting- Rukwa), Gabriel Gadiel Michael (Azam), Hussein Mkongo (Ashanti United) na Ibrahim Said Mohamed (Chuoni, Zanzibar). Mabeki wa kati ni Bashiru Ismail (Tanzania Prisons), Faki Rashid Hakika (Ashanti United) na Pato Ngonyani (Majimaji).
Viungo ni Ally Nassoro (Coastal Union), Bryson Raphael (Azam), Farid Musa (Azam), Hamid Mohamed (Mbeya City), Hassan Mbande (Mtibwa Sugar), Ibrahim Mohamed Ibrahim (Scouting- Ilala), Idd Seleman (Ashanti United), Mohamed Issa Juma (Acudu, Afrika Kusini), Muhsin Ally Muhsin (Scouting- Kinondoni), Seleman Magoma (Scouting- Ruvuma) na Tumaini John (Scouting- Mwanza).
Washambuliaji ni Ally Salum Kabunda (Ashanti United), Ibrahim Hamad Hilika (Zimamoto, Zanzibar), Jafari Mwambusi (Mbeya City), Kelvin Friday (Azam), Ramadhan Bilal (Mlale JKT), Salum Abdilah Mineli (Ndanda) na Sibiank Lambard (Tanzania Prisons).