Sunday, June 1, 2014

MKUTANO MKUU WA YANGA SC SAFIIII WAFANYIKA BILA BUDHABU YOYOTE

Mkutano Mkuu wa marekebisho ya baadhi ya vipengele kwenye Katiba ya Yanga umefanyika na kumalizika salama na furaha kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi -Oysterbay huku wanachama wakipitisha kipengele cha kuundwa kwa kamati ya maadili.
Mwenyekiti wa klabu ya Yanga SC Yusuf Manji amewaongoza wanachama hai wapatao 1,560 kupitisha kipengele hicho kipya kwa ajili ya maslahi na faida ya Wana Yanga kwani bila kufanya hivyo timu isingeweza kuruhusiwa kushiriki Ligi Kuu msimu ujao.
Aidha katika mkutano huo Manji amewatoa hofu wanachama kwa kuwaambia kuwa usajili unaendelea kufanyika na nafasi zilizobakia ni nne tu hivyo pindi utakapokamilika basi wataweka wazi kila kitu.
Kuhusu nafasi ya Kocha Mkuu Manji amesema Kamati ya Mashindano imemkabidhi mapendekezo yao na kwa sasa yupo kwenye mazungumzo na Marcio Maximo aliyewahi kuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa Tanzania kuja kukinoa kikosi cha Jangwani.
Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini Mama Fatma Karume aliongoza kikao cha waachama kilichomuomba Bw Manji kuendelea na uongozi ambapo mwenyeikti alitoka nje na kamati yake ya utendaji na pindi waliporejea walikubali ombi hilo na kusema watafuata taratibu za kikatiba.
Mwisho kupitia mkutano mkuu wa leo wa wanachama umeazimia kuwaongezea muda wa mwaka mmoja Mwenyekiti Yusuf Manji pamoja na Makamu wake Clement Sanga ili waweze kukamilisha masuala ya katiba na kuweza kuandaa mkutano wa uchaguzi baada ya katiba kupitishwa na TFF.

STARS MAMBO SAFI JIJINI HARARE, WAINYAMAZIMA ZIMBABWE KWAO NA KUSONGA MBELE AFCON

Taifa stars ya Mart Nooij itakabiliana na Msumbiji katika mchezo wa mwisho wa mtoano kuwania kupangwa hatua ya makundi kusaka tiketi ya fainali za mataifa ya Afrika mwakani nchini Morroco.
Hii imetoAFCON_2015_LOGO-MOROCCOkana na sare ya 2-2 waliyopata jioni hii dhidi ya wenyeji wao, timu ya taifa ya Zimbabwe.
Zimbabwe walioripotiwa kuwafanyia hujuma vijana wa Tanzania wameambulia patupu leo hii baada ya kuoneshwa soka safi na vijana wa Tanzania.
Haikutegemewa kuwa mechi ya mabao mengi kiasi hiki, lakini Zimbabwe ndio walianza kuamsha `mizimu` ya vijana wa Taifa stars waliokuwa wanamtazama kiongozi wao wa msafara, Rais wa TFF, Jamal Malinzi akiwa jukwaani.
Bao la dakika ya 10 walilopata Zimbabwe kupitia kwa Phiri Danisa  liliwashitua mashabiki wa Tanzania, lakini nahodha wa Taifa Stars, Nadir Haroub Canavaro katika dakika ya 21 aliwazisha bao hilo na kuufanyaubao wa matangazo kusomeka 1-1 mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika.
Wakati Zimbabwe wakiwa katika presha ya kusaka bao la pili, dakika ya 46 kipindi cha pili walifanya makosa na Thomas Emmanuel Ulimwengu hakufanya makosa na kuwaadhibu goli la pili.
Dakika ya 55 kipindi hicho cha pili, Katsande Willard  aliifungia Zimbabwe bao la pili la kusawazisha.
Baada ya hapo mpira ulianza kuchezwa kwa timu zote kutafuta mabao zaidi, lakini wenyeji ndio walikuwa kwenye presha kubwa zaidi kwasababu tayari Stars walikuwa na mtaji wa mabao zaidi.
Taifa stars ya Mart Nooij ilionesha kiwango safi na upinzani mkubwa ugenini na kuwafurahisha watanzania wachache waliokuwa uwanjani na waliokuwa wanaangalia kupitia televisheni.
Haikuwa kazi nyepesi kwa vijana wa Tanzania kuwafunga Zimbabwe, lakini jitihada kubwa walizofanya na kutambua kuwa mamilioni ya watanzania wapo nyuma yao, ilitosha kuwapa morali kubwa.
http://dailynews.co.tz/images/STARSULIMWENGUU.jpgMechi ya kwanza ambayo Stars ilishindi bao 1-0 uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, tatizo kubwa lilionekana katika safu ya kiungo, lakini leo vijana walijidhatiti na kuonesha kandanda zuri.
Canavaro amekuwa kiongozi wa kuigwa kwani alionesha ushupavu wa kuwaelekeza njia wenzake ikiwemo kufunga bao muhimu la kusawazisha.
Beki kazi yake ni kulinda, inapofika wakati anafunga, basi amejiongezea majukumu kwa lengo la kuisaidia timu yake ipate mafanikio.
Kuwa nahodha sio kuvaa kitambaa tu bali ni pamoja na kuisaidia timu kama wanavyofanya akina Sergio Ramos.
 Kazi nzuri Nadir Haroub `Canavaro`.
Ulimwengu ni mchezaji wa TP Mazembe. Kuna faida ya kuwa na wachezaji wa kimataifa kama yeye. Kudhihirisha umuhimu wake, alifunga bao safi na kuwavusha watanzania hatua inayofauta. Kazi nzuri kijana.
Kwa matokeo ya leo, Taifa stars imefuzu hatua ya mwisho ya mtoano kwa wastani wa mabao 3-2 kuwania kupangwa hatua ya makundi kusaka tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika.
Hii inatokana na ushindi wa bao 1-0 iliopata uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam katika mchezo wa kwanza na matokeo ya 2-2 mjini Harare jioni hii.
Kwa maana hiyo, Taifa Stars inajiandaa kuutafuna mfupa wa Msumbiji katika hatua ya mwisho ya mtoano.
Msumbiji walifuzu hatua hiyo kwa wastani wa mabao 5-0 baada ya juzi kutoka suluhu ya bila kufungana na Sudan Kusini Ugenini, wakati waliibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 mjini Maputo.
Msumbiji wana historia ya kuwaharibia Taifa stars katika michezo muhimu ya mashindano, hivyo ni jukumu la wachezaji na kocha Nooij kupanga mikakati kabambe ya kuwanyamazisha `Mamba hao weusi`.
Mechi nyingine iliyomalizika jioni hii ni baina ya Lesotho na Liberia na kushuhudia Lesotho wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0.
 

Kikosi chaTaifa Stars; Deo Munishi ‘Dida’, Shomary Kapombe, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Mwinyi Kazimoto, Simon Msuva/Said Mourad dk78, Amri Kiemba/Frank Domayo dk62, John Bocco, Thomas Ulimwengu/Mrisho Ngassa dk88 na Erasto Nyoni.
Jumapili Juni 1
Zimbabwe 2 Tanzania 2 [2-3]
Lesotho 2 Liberia 0 [2-1]
14:30 Congo v Namibia [0-1]
15:00 Benin v Sao Tome And Principe [2-0]
15:00 Chad v Malawi [0-2]
16:00 Equatorial Guinea v Mauritania [0-1]
 Nchi ambazo zimeingia Makundi moja kwa moja: Nigeria, Ghana, Ivory Coast, Zambia, Burkina Faso, Mali, Tunisia, Algeria, Angola, Cape Verde, Togo, Egypt, South Africa, Cameroon, DR Congo, Ethiopia, Gabon, Niger, Guinea, Senegal and Sudan.
 KUNDI F
-Zambia
-Cape Verde
-Niger
-Taifa stars vs Msumbiji

Mechi ya kwanza 18–20 Julai
 mechi ya pili1–3 Agosti

Thursday, May 29, 2014

FABIANSKI AKUBALI KUTUA SWANSEA CITY

GOLIKIPA wa Arsenal, Lukasz Fabianski amekubali kujiunga na Swansea City wakati mkataba wake na klabu hiyo utakapomalizika mwezi ujao. Golikipa huyo wa kimataifa wa Poland alikataa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo ili kumzuia asiondoke na sasa ameamua kuhamia katika Uwanja wa Liberty unatumiwa na Swansea. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao, Arsenal walithibitisha kuondoka kwake na kumshukuru golikipa huyo kwa mchango wake aliotoa katika kipindi ch
ote alichokuwepo na kumtakia kila la kheri huko anapokwenda. Golikipa huyo mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na Arsenal akitokea Legia Warsaw mwaka 2007 na kucheza mechi 78 katika kikosi cha kwanza katika mashidano toka alipojiunga nao.

ARSENAL MORATA KINDA MSHAMBULIAJI WA MADRID MWENYE UMRI WA MIAKA 21.

MAOFISA wa klabu ya Arsenal, wamesafiri kwenda Hispania kwa matumaini ya kumamilisha dili kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata. Mshambuliaji huyo amekuwa akiwindwa na Arsene Wenger kwa muda mrefu na klabu imeamua kuanza harakati za kumsajili nyota huyo mwenye miaka 21 mapema, kwani Juventus nao pia wanamuwinda.
Madrid wako tayari kumuuza lakini wanatarajiwa kusisitiza kutaka dau lao walilomnunulia kitu ambacho kinaonekana kitakuwa kigingi kikubwa kwa timu zinazomuhitaji. Arsenal walijaribu kumsajili kinda huyo wa kimataifa wa Hispania majra ya kiangazi mwaka jana na safari hii wanaamini uhakika wa kupata namba katika kikosi cha kwanza atakaoupata utawasaidia kumvutia kwao. Morata amefunga mabao tisa katika mechi 28 alizocheza akiwa na Madrid msimu huu na alitokea benchi katika mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya uliofanyika Jumamosi na kuisadia timu yake kuisambaratisha Atletico Madrid. Arsenal pia wanamtaka mshambuliaji mwingine wa Madrid Karim Benzema lakini Carlo Ancelotti anamtaka nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa kusaini mkataba mpya na timu hiyo.

CECAFA NILE BASIN CUP MBEYA CITY ROBO FAINALI KUUMANA NA WAKALI KUTOKA UGANDA

Timu ya Soka ya Mbeya city katika hatua ya Robo fainali itashuka dimbani kuonyeshana kazi na wababe kutoka Uganda, Victory University katika Robo Fainali ya michuano ya Nile Basin Jumamosi ya Mei 31, Uwanja wa Khartoum Sudan.
Hiyo itakuwa robo Fainali ya kwanza siku hiyo itakayoanza Saa 11:30 jioni na kufuatia na mchezo mwingine kati ya wenyeji El Ahli Shandi dhidi ya Malakia ya Sudan Kusini.
Awali, kesho zitachezwa Robo Fainali mbili za kwanza kati ya AFC Leopards ya Kenya na Defence  ya Ethiopia Saa 11:30 kabla ya wenyeji El Merreikh kuumana na Academie Tchite ya Burundi.
Mbeya City ilitinga Robo Fainali za michuano ya Nile Basin inayoendelea nchini Sudan kufuatia sare ya bila kufungana na Enticelles ya Rwanda usiku wa jana Uwanja wa Khartoum.
Matokeo hayo yanaifanya Mbeya City imaliz
e na pointi nne baada ya mechi tatu, ikiwa katika nafasi ya pili nyuma ya AFC Leopards ya Kenya walioongoza kundi kwa pointi zao tisa.
Enticelles imemaliza nafasi ya pil
i kwa pointi zake mbili na Academie Tchite ya Burudi imemaliza mkiani mwa Kundi B kwa pointi moja iliyovuna kwenye sare na timu ya Rwanda.
Michuano hii inayoshirikisha mabingwa wa Kombe la FA au washindi wa pili wa Ligi Kuu za nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), inafanyika kwa mara ya kwanza mwaka huu, Sudan wakiwa wenyeji wa kwanza.
CECAFA imeanzisha mashindano hayo kwa lengo la kuongeza changamoto kwa klabu za ukanda wake. 
MSIMAMO WA:
KUNDI ‘A’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
Al-Merreikh
3
2
1
0
7
2
+5
7
Victoria University
3
2
1
0
4
0
+4
7
Malakia
3
1
0
2
5
5
0
3
Police
3
0
0
3
0
9
-9
0
KUNDI ‘B’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
AFC Leopards
3
3
0
0
5
1
+4
9
Mbeya City
3
1
1
1
4
4
0
4
AcademieTchite
3
1
1
2
3
4
-1
3
Entincelles
3
0
0
2
0
3
-3
1
KUNDI ‘C’

P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts.
Al-Shandy
2
2
0
0
4
1
+3
6
Defence
2
1
1
0
2
3
-1
3
Dkhill
2
0
0
2
2
4
-2
0
ROBO FAINALI
TAREHE
M/No.
MECHI
MAHALA
SAA
30/05/14
16
AFC Leopards Vs Defence
MERREIKH
6:30pm

17
Al-MerreikhVs AcademieTchite
MERREIKH
8:30pm





31/05/14
18
Victoria University Vs Mbeya City
MERREIKH
5:30pm

19
Ahly Shandi Vs Malakia
MERREIKH
8:00pm





NUSU FAINALI
Jumatano Juni 2
[20]. Mshindi 16 Vs Mshindi 17
[21]. Mshindi 18 Vs Mshindi 19
Jumatano Juni 4
Mshindi wa Tatu
22]. Aliefungwa 20 Vs Aliefungwa 21
FAINALI[
23] Mshindi 20 Vs Mshindi 21